Japan: Dar could become an Industrial Hub

Japan: Dar could become an Industrial Hub


uh Yeah Tumezichoka hizo PIKIPIKI za KICHINA Majina Shida kuyataja... Spear Parts kila siku ni NYINGINE no STABLE MARKET... Nyingi ni BURE CCM affiliation...

Wakati unazichoka za mchina leta basi za kwako kwani za mataifa mengine ubavu wa kuzinunua huna hizo za mchina za 1.5 mil.unalia lia utaweza kununua pikipiki ambayo pikipiki 1 ni mil 12.au unaleta story za vijiwe va pombe.
 
Ujapani hawawezi kuja kujenga Kiwanda cha kutengeza Magari TZ leo hii hata iweje!
Na sababu ni rahisi sana hakuna hayo mazingira ya kuruhusu Viwanda vya namna hiyo, kuanzia Umeme, Maji, Wataalamu waliobobea kwenye huo Ufundi kuanzia Mafundi Mchundo mpaka Wahandisi wa Umeme, Magari, hakuna Nchini mwetu.
Tanzania nzima labda kuna Mtu mmoja au wawili wenye utalamu wa mambo Chuma (Metallurgy) na hao wote kama wapo watakuwa hawajasoma TZ...

Hizo Nchi ulizozitaja za Asia zilizopata huo Uwekezaji ktk Ujapani au sehemu nyingine Duniani ni kwamba zilishafanya hayo mambo kwanza na ndio ikawa Rahisi kwa Wawekezaji kuja, sasa Ujapani au nchi nyingine yoyote ile haiwezi kuja kukufundishia Wahandisi, kuja kukujengengea Miundo Mbinu ya Umeme wa Uhakika, kukujengea Miundo mbinu ya Maji ya Uhakika, kukujengea na kukuimarishia Miundo mbinu ya Bandarini na kuhakikisha Ufanisi upo na kuondoa wizi...

Nitakupa Mfano mdogo sana, Kiwanda cha Chuma cha MM Steel Mikocheni kikiwashwa sehemu nyingine zinakosa umeme wa uhakika sasa sembuse hicho cha Magari?

Hakuna Mtu atakaye tujengea Viwanda, Hilo ni Jukumu Letu sisi Wenye Nchi!


Unayosema ni kweli. Lakini mimi nafikiri hizi nchi nyingi zilizoendelea hususani Japani kwa sasa zinatatizo la Raw Materials hasa chuma na wamekuwa wakiagiza kutoka nchi. Kama watakuwa wameona kuwa gharama za kuagiza ni kubwa option ya kuanzisha kiwanda cha chuma na kutengeza bidhaa mbali mbali za magari katika nchi nyingine inawezekana. Hapa wenyewe wanachojali ni kukuza uchumi wao wala si kwamba watusaidie kuendelea.

Kuhusu watalaam wa chuma ambacho ndo backborn ya viwanda kwa sasa hatuna wa kutosha. Tanzania hakuna chuo kinachotoa B.Sc in Metallurgist "physical metallurgy", ila wapo wachache waliosoma nje hasa Germany. Ila kama waJapani watakuwa wameamua lazima watakua na experts wakuanza nao na baadae waTz wenye watachua nafasi.



 
Wakati unazichoka za mchina leta basi za kwako kwani za mataifa mengine ubavu wa kuzinunua huna hizo za mchina za 1.5 mil.unalia lia utaweza kununua pikipiki ambayo pikipiki 1 ni mil 12.au unaleta story za vijiwe va pombe.

Ubaya za KICHINA Unazilipia kwa kuiuza NCHI yako kwao... ANGALIA KARIAKOO.. Wachina wapo hadi Mama ntilie... Malaya wako hadi wa kichina... yaani wanachukua njia kuu na njia ndogo za kutupatia pesa...

Sasa Dada zetu wanaofanya biashara ya kujiuza watakwenda wapi Jamani? Bado wamejaribu kutumia Madawa ya kichina ya kujichubua; kuongeza ------; Pua; Visigino... Haviwezi kurudi kama zamani --- Halafu hao wanakuja wa KICHINA

Hauoni kuwa ni SHAMBULIO LA HATARI????
 
Naona tunashangilia lakini ni lazima tuelewe hii ni mipango tu hatujaona hizo investment bado. Kuhusu hao wanaotaka tutengeneze magari wateja wako wapi Tanzania ina magari yasiozidi milioni mbili mengi ya mashirika ya uma na serikali hayatoshi hata tukichanganya na majirani. Kitu kingine hatuna wafanyakazi wenye utaalamu wa kutosha kujenga viwanda vya magari. Hivyo tusitegemee magari kutengenezwa Tanzania. Ni wape mfano mdogo State ya California pekee ina magari millioni 32 ambayo ni zadi ya mara 16 ya magari yote Tanzania!!
 
Back
Top Bottom