Michael Mkwanzania
Member
- Jun 8, 2016
- 83
- 648
Jana Leo na Kesho, mstari mrefu wa mafanikio kwa mtanzania /muafrika mweusi.
“I write nikiwa inspired” niliandika kwenye makala yangu ya kwanza.
Kuna swali ime ni inspire, imenisikitisha, imenipa uzuni, kwa jinsi gani mtu mweupe, the white man, amefanikiwa kuua uwezo wa wengi sana kujiamini na kuweza kwenda mbele, swali linauliza: Je, mungu kaumba baadhi ya wanadamu kwa upendeleo wa akili na maarifa?
Nikiisoma nakaribia hadi kutapika, kwa kua mtu mweusi kaandika hii. Na anazidi danganya na kupeleka mbele mfumo uliotengenezwa na watu weupe, wa kuua, kurudisha nyuma, kuchochea na kufanya wanadamu wadhani kwamba ukizaliwa na ngozi ambayo ni nyeusi we si mwanadamu kamili na inabidi utawaliwe.
Kwanza nikajua kama utani flani hivi, ila nikaingia kwenye comments na wengi wanakubaliana nae.
Mimi sio mwana historia, kuna mengi sijui bado na najifunza kila siku, kama kuna fact nimekosea ntakubali kuelezewa Zaidi na kukosolewa.
Soma Hii Polepole na Kwa makini sana, systems(mifumo ya dunia) hazitaki ujue Zaidi. Rudi usome tena, click link zote kuthaminisha (ni ndefu kidogo).
Jana
Ninaposema jana namaanisha historia, the past, vitu gani ambavyo vimetuleta hadi kufikia hapa tulipo, maana hauwezi, akili haitokuja kufunguka kama hujaisoma historia.
Kwenye report yangu ya form 4, history ndo somo pekee ambalo nilipata F. Sikua na hamu nayo, sikuipa a second thought, nilifikiri tu kwamba mambo yashapita, mimi kukariri miaka na majina na matukio itanisaidia nini. Fast forward miaka kumi mbele, hamna kitu ninachopenda kisoma kama historia. Natafuta vitabu vya researchers wa african history, natafuta makala, video, audio kuelewa kwanini leo ipo hivi ili kesho niifanye tafauti, na huu ndio umuhimu wa jana, umuhimu wa historia.
Mifumo inakwambia kwamba, ohh we ni maskini, na vyote ni juu yako, fanya kazi kwa bidii, usipofanikiwa, ukifa bila kufanikiwa, vyote ni juu yako, ambacho hawataki kukubaliana nacho ni kwamba kilichofanyika jana, ndicho kinachowafanya watu wawe hivi leo, ndicho inachofanya kesho yetu isije kwa manufaa.
Tuchukulie mfano, jana mtu alikuja na tofali akakuvunja miguu, alafu leo mnaanza kwenye mstari mmoja kushindana kukimbia, mnaanza wote, wewe unajivuta kwa nguvu zako zote, yeye anakimbia haraka alafu anakucheka, “muone huyo mtu hawezi kukimbia vizuri” anasema.(ngoja nikuchoree mstari wa kwanza).
Unaweza usiamini kwamba hicho ndo sababu mamilioni ya watu weusi ni maskini hadi leo na watazidi kua maskini kesho, lakini ngoja niendelee, ngoja nikuchoree mistari, let me connect the dots.
FACTS
FACTS
Jana, Mwaka 1960 Congo ilipopata uhuru kutoka kwa Belgium, wananchi wa congo waliomaliza chuo kikuu walikua 16 tu kati ya watu milioni 14. Leo congo ipo vitani, Belgium uchumi wake unafanya vizuri tu. (Tukumbuke kwamba walidai wanakuja leta maendeleo na kuwekeza mifumo yao)
Jana tarehe 29 february mwaka 1906, miaka 112 tu iliyopita, nkosi mputa gama, magodi mbano, njorosa mbano, zinanimoto gama, fratera gama, mtepa hawayi gama, mtekateka tawete, majiyakuhanga komba, moambalioto soko, songea mbano na mputa mkuzo gama walinyongwa pamoja na watu zaidi ya laki 3 kuuwawa kwaajili ya kupigania uhuru wa watanganyika kutoka kwa wajerumani.
Hawa watu walijua kwamba wazungu hawa ambao muuliza swali amesema basically ni wametengenezwa tofauti na mungu na wemepewa vya ziada ni waongo, ni watu wabaya ambao wanaua na kubaka, na kuchukua rasilimali, na kudanganya kua wanafanya mazuri huku watu wanaowafanyia mazuri maisha yao yanaenda chini, ukiwasifia wajerumani kwa ku invent chochote kabla ya Mtanzania, hawa watu wote waliokufa kutupigania wanakugeuzia mgongo huko walipo.
Kosa kubwa tunalozidi fanya ambalo mimi mwenyewe personally najaribu kuachana nalo ni slave mentality ama akili za utumwa ambazo bado zinaendelea kututawala.
SLAVE MENTALITY ni nini? Akili za utumwa ni nini?
Akili za utumwa ni kukubaliana na kusheherekea kitu chochote ambacho tulipewa jana kipindi cha utumwa, na kuchukua na kukubaliana navyo kama vyetu. Sito taja ni vingapi ambavyo tumepewa, maana vitu vingine ni nyeti sana na vimeshatuingia na kua foundation za wengi, so ili kuepuka na akili za utumwa, jiulize sasa hivi ni kitu gani unachokubaliana nacho ambacho tulipewa na mkoloni.
Jana Wakoloni walikubaliana (walidanganyana) kwamba muafrika hajielewi, muafrika hana uwezo wa kuendelea, muafrika hana akili, muafrika inabidi atawaliwe ili achangie na aweze endeleza mifumo ya dunia. Na wakaja na dini zao, vitabu vyao, na kuua, kubaka, kutesa kwa mda mrefu, hapa tanzania wakoloni kutoka magharibi kwa miaka zaidi ya 500, generation/ vizazi zaidi ya 8 vili chukuliwa kwamba sio watu, hawana uwezo, hawa ni babu na bibi zetu(hapa hatujaongelea wakoloni kutoka mashariki).
Kipindi chote hiki wakoloni nchini kwao wanajenga, wanasoma, wana innovate, wana tunga, wanafundishana, wanafanya kazi pamoja ili kukuza uchumi wao.
Wajerumani ndio waliofanya ukatili mkubwa sana kipindi cha maji maji rebellion, Tanganyika, na mengine mengi tu walifanya kwenye nchi zingine afrika.
August 4, 1905, kinjekitile alinyongwa ili kutishia mtu yoyote kujifanya kwamba anapigania haki za wa Tanganyika. Sijui kwanini hatuna siku ambayo tunapumzika na kusherekea ujasiri wake, alionganisha watu wote waachane na tofauti zao na kupigania uhuru wa Mtanganyika, na kuanzisha maji maji rebellion.
Walichokifanya jana ndicho kimetuweka hapa leo.
Makala ninayoijibu imeandikwa na mtu ambae bado ana akili za utumwa.
Kutoka miaka ya 1400 hadi kuja kufikia 1961, nchi hii yetu ilipokuja kupata uhuru tulikua tupo kwenye kipindi cha ukoloni, tulivunjwa miguu kwa miaka Zaidi ya 500, na leo wanatwambia tukimbie, tushindane tuone nani ambae anaweza fika mwisho wa kwanza. Tusisahau historia, msatari wa kwanza huo nimekuchorea kutoka jana hadi leo.
Leo
Uongo mkubwa wa leo ni kwamba mtu yeyote anaweza akawa tajiri kwenye mifumo hii, uongo mkubwa wa leo ni kwamba akifanya kazi kwa bidii mtu yoyote anaweza kujikwamua kutoka kwenye umaskini, uongo mkubwa wa leo ni kwamba watu ambao ni maskini ni maskini kwa kua hawajafanya kazi kwa bidii. uongo mkubwa wa leo ni kwamba mimi na wewe tulikua, na wengi wetu wenye ngozi kama zetu watazidi kua maskini kwa ajili hatuna uwezo wa kufikiria kama watu wenye ngozi tofauti na zetu.
Hela ni nini? Zinapatikanaje? Zinatengenezwa vipi? Mtu akifa anamuachia nani? Hela zipo ngapi duniani? Benki zinafanya vipi kaizi? kwanini thamani ya hela inapanda na kushuka? kwanini hata kama nchi ina rasilimali nyingi wananchi wake bado maskini?
Ukifanya uchunguzi unaweza jibu maswali yote hayo juu, na ukishayajibu, ujiunge kwenye upande wa kushangaa ni jinsi gani mifumo ya dunia ilivyowekwa kumfanya mtu mweusi abaki maskini.
Leo hii kuna lodge ngorongoro, ambayo ina milikiwa na watu wenye ngozi nyeupe ili watu wengine wenye ngozi nyeupe wakija kufanya utalii hela zao zinazunguka kati yao, serikali inakata makato lakini majority of pesa inarudi kwao, haiendi kuzunguka kwa wananchi ambao hali zao ni za kati, wala wenye maisha ya chini. Kwenye pita zangu nmekutana na watu wawili ambao budget yao ya wiki hapa nchini ni takriban milini 20 za kitanzania.
Leo hii, nchi tajiri zinakuja kusaidia africa na kutangaza kwamba wanasaidia Nchi za Afrika, wanaleta bilioni kadhaa, lakini kwa mifumo walioiweka rasilimali wanazozitoa kwenye nchi za Afrika zina thamani ya Trilioni kadhaa, lakini kupitia mifumo kama Trade mispricing, kwamba receipt ambazo zinalipwa sio za kweli na haziendani kabisa na maliasili ambazo wanachukua, na kulipia bei ndogo sana kwa ajili ya maliasili za kutengeneza mabilioni, jiulize ni mfumo gani ambao una panga bei ya thamani za rasilimali?
Na swali lingine la kujiuliza ni kwamba leo hii thamani ya hela ni nini? Dollar za kimarekani 9,400 ni sawa na million 20 na za kitanzania, tumefikaje hapa leo hii?
Leo ni maswali tu sana sana, kwa kua leo hali iliyopo inabidi itufanye either tubadili mifumo ili mtu mweusi aweze fanikiwa, ama tukubaliane na mifumo.
Turudi jana Tena (tutafika kesho ngoja kidogo).
-Tunaambiwa jana kwamba muafrika hakua na uwezo wa kufikiria, tunaambiwa. Tunaambiwa uongo, what are the facts, ukweli ni nini? Jana ilikuaje? Turudi nyuma, kabla ya ukoloni, turudi nyuma Zaidi, historia ambayo hata mashuleni kufundishwa ni ngumu, hivi jiulize kabla ya ukoloni, wa afrika walikuaje, waligundua nini, walikua wanafikiria nini, Afrika mashariki ilikuaje, kabla hawajachora mistari kugawana vipande vya afrika ambavyo leo tunaita mipaka, kabla hawajaanza kutujaza na akili za utumwa ilikuaje?
Industrial revolution, yaani kipindi cha viwanda kuanza, kimejengwa na damu na jasho la mtu mweusi, kila nchi ambayo ilianza kufanikiwa kwenye miaka ya 1760 kwenda 1800 hivi ni nchi za wakoloni. Ni nini Kilichokua kinaendelea Tanganyika kipindi ambacho industrial revolution kinaanza kwenye nchi za magharibi?
Kipindi cha miaka hiyo, kiliitwa the scramble for afrika yaani nchi za afrika zimefanywa kama biskuti hivi ambazo wamepewa watoto wa darasa la kwanza kugawana, Germany, british, france, Belgium, Portugal, Italy nchi zote hizi na zingine zimefaidika kwa damu na jasho la watu weusi, kisha leo tunashindana kwenye uwanja mmoja.
Ukisema mtu mweusi hana akili ya kufikiria kama mtu mweupe, mamilioni ya watu, waliokufa na kuuliwa ambao labda wangekuja kua madaktari, wana sayansi na vingine vingi ambavyo watu ambao maisha yao yamekatwa wanakugeuzia mgongo.
Textile, nguo hizi ndio ilikua viwanda vya kwanza kufanikiwa, na vilifanikiwa vipi? Kwa kuwaweka watu weusi kwenye mashamba yao ili kuwapatia pamba na vitu vingine, mashamba ya kwenye colony zao, mashamba ambayo wamechukua watumwa kuwarudisha kwao, mashamba ambayo damu zimetoka za watu weusi.
Kutoka Wikipedia:
“The Industrial Revolution marks a major turning point in history; almost every aspect of daily life was influenced in some way. In particular, average income and population began to exhibit unprecedented sustained growth”
Facts
Hii video ndefu sana, ila ukiiangalia yote utafaidika sana na historia.
Robin walker ni mwana historia, ambae ana institution inayo fanya uchunguzi wa historia ya afrika, na wanagundua vitu vipya kila siku, historia ya kweli sio ambayo tunaambiwa na wakoloni kila siku.
Ndani yake kwenye dakika ya 21 hivi, Robin walker anasema kwamba
“Kilwa was considered one of the most beautiful and well constructed cities of the world” anasema
Mji wa kilwa ulijengwa karne ya kumi, yani 900 AD na kisha kuongezewa karne ya 15, miaka ya 1400 hivi, kabla ya wakoloni kuja, kabla hawajasema kua wa Afrika wote wanaishi kama wanyama tu hawana maendeleo, na inabidi kutawaliwa, miaka Zaidi ya 400 kabla hawajaanza kuja kuua na kufanya watu wawe watumwa.
Miaka ya 1200 hivi, karne ya 13, east Africa walikua wamejenga vyoo, na majengo ambayo Miaka Zaidi ya 600 kabla wakoloni hawajaja, civilization ilikua inafanya kazi vizuri kabisa, tulikua na majengo ambayo magharibi wanayaota. Mji wa lamu, ambao upo Kenya, unasemekana ulijengwa miaka ya 1370.
Waswahili walikua watu mahiri sana, Swahili settlement zilijenga na ku innovate mambo mengi sana ambayo yanafichwa na historia, historia inayofundishwa ni version ya mkoloni, kwamba civilization afrika ilianza kipindi ambacho walikuja wao, miaka ya 1700-1800 hivi. Ni uongo mtupi. Jana haikua hivyo jana na juzi yetu wameifuta ili kutengeneza leo ambayo tunaamini ka mtu mweupe ana uwezo Zaidi yetu, tupilia mbali mtu yoyote ataewaza hivi, mgeuzie mgongo leo kabla hatujaenda kukutana na mababu zetu waliokua na akili kuliko hawa watu waliokuja kuwauwa na kuwalzimisha kujiunga nao na kuwapa rasilimali kwa kutumia mdomo wa bunduki.
Leo
Leo tunakubaliana kwamba ngozi nyeupe ina uwezo wa kufikiria kuliko watu wenye ngozi nyeusi, kweli akili za utumwa zimefanikiwa kujengwa na wakoloni.
Leo nusu ya cobalt, maliasili ambayo inatumika kutengeneza simu hizi, ambazo dunia nzima tunatumia inatoka congo, inatoka afrika, na wananchi wa congo ni maskini wanaambiwa kwamba hawana uwezo wa kufikiria kama mkoloni, DRC inabidi iwe kama sio nchi tajiri namba moja basi iwe kwenye top 3, maana ndipo wenye upatikanaji mkubwa wa cobalt, copper, diamond, tantalum (inapatikana kwenye simu, computer, dvd player, video games na vingine) na tin, kwanini na vyote hivi Congo sio tajiri, Mifumo ama systems.
Leo tunajaribu na tunakubaliana kwamba tunaweza kua kama Steve Jobs, Mark zuckerberg, Bill Gates ana wengine wambao ni watu wenye ngozi ambazo sio nyeusi, wakati apple inazidi kua tajiri, wakati wakiingi congo wananyonya maliasili ambazo wanaenda kutengenezea Iphones kisha wanarudi kutuuzia hukuhuku afrika, wakati most computers ambazo zinatumia windows zinatumia mali asili za afrika, na badala ya kulipa thamani yake kweli wenyewe wanalipa visenti ili kwenda kuuza bidhaa zao mamilioni. Wamefanikiwa kutengeneza thamani kwa ajili ya kipindi cha ukoloni, na leo vitu vinavyotoka kwa vina thamani kuliko vinavyotoka kwetu.
Leo Hii ukoloni haujaisha, na tusipo amka, kesho haitakua nzuri kabisa.
Uwongo mkubwa wa leo ni kwamba hela ikienda kwa mtu mmoja, hiyi hiyo inaweza kwenda kwa mtu mwingine na yeyote akifanya kazi anaweza kua tajiri kama billgates, thamani haipo hivyo huu ni uongo.
Hivi apple, iphone? jana babu zenu wamebaka, wameua, mmechukua watu weusi kwenda kutengeneza mifumo yenu kurahisisha na kuendeleza uchumi, jana mmefanya watu wawe watumwa, jana mme fanya watu waishi chini ya ukoloni, leo hii mnalipa vi centi ili kupata maliasili, watoto wadogo wanachimba haya madini mnayotumia, na nyie mnatengeneza mabilioni kuuza simu, na kweli dunia nzima tunaangalia apple kama watu wanaotengeneza hela kimaadili?
Na hizi sio siri, ukisearch google ama youtube unaona yanayoendelea. Sio siri, yote yapo wazi.
Hivi battery za simu zote zingetengenezwa Congo, na magari yanayotumia battery yange tengenezwa Congo, alafu nchi ambazo zingenunua hizi simu na magari walipe thamani yenyewe kabisa, congo ingekua maskini, hivi kama kampuni kuchukua cobalt kuweka kwenye battery zake ingebidi ilipe thamani kubwa, la sivyo ijenge viwanda vyake nchini humo ama iwekeze nchini, kuna mtu angepigana unadhani, kuna vita ingetokea?
Hakuna vita Afrika ambayo haijasababishwa na wakoloni kuanzisha, au kusababisha na kuchochewa na mmarekani, and that is fact.
Misaada wanayofanya ni ujinga mtupi.
Watu milioni 13 wanahitaji misaada congo leo, ndio vichwa vya habari vinavyosema leo, lakini hatu address lasirimali wanazochukua, walizochukua, na watazozidi chukua kila siku, aisee mkolini amefanikiwa kusukuma hoja zake kwenye akili za watu.
Eti leo, wanataka okoa wakongo kutoka vitani, vita ambazo wamezitengeneza wenyewe.
Hela zozote wanazotoa wasiziite msaada, nchi yoyote ambayo imeshirika kwenye ukoloni inahitaji kusema kwamba wanalipa walivyoiba, sio msaada.
Ukinivunga miguu leo, alafu kesho unaambia ndugu zangu kwamba eti ohh, namsaidi kwa kumpeleka hospitali, hapana, haunisaidii, unalipa ulichofanya, na nikipona, tutaonana kesho.
Main Thing/kitu muhimu cha kujua na kuelewa kabla ya kwenda kesho.
Na nili comment hili kwenye makala nnayoijibu, everything is gradual, inabidi tuanze A ili kufika B, ndipo tutapoweza fika K, hadi W.
Sio Mtu mmoja ambae anaweza kufikiria kila kitu, mark zuckerberg alitumia PHP kutengeneza facebook kwa idea ambayo aliiba kutoka kwa watu walioitunga, PHP ilibidi itengenezwe kwanza na watu wengine, na lugha ambayo miaka mingi sana imejengwa polepole, je ni kweli wa afrika tulishindwa kutengeneza lugha za programming kabla ya wakoloni?
Hapana, PHP imetengenezwa mwaka 1994, na watu ambao baba zao na bibi zao hawajapitia utumwa na ukoloni.
Hivi watu wote waliouliwa na kuteswa na kubakwa, unadhani hata mmoja wao alikua hana uwezo wa kuja kupata mtoto au mjukuu ambae angekuja kutengeneza lugha ya programming?
unadhani kama mda wote huo watu wangekua hawakimbii na hawaogopi kuuliwa, wanapeleka watoto wao shule, na wanafundishana na kufanya kazi pamoja, na ukiweka rasilimali zote tulizonazo, mkoloni angetufukia? Hapana, na wote wanajua hili ndio maana mifumo bado ipo na inafanya kazi hadi leo, na wamefuta historia kabla ya ukoloni.
Lugha ya kwanza ya kutengenezea program (programing languages) iliyotumika na ilitengenezwa mwaka 1954, unajua nini kilikua kinaendea Tanganyika mwaka huu? Mwalimu Julius Nyerere na Oscar Kambona ndipo walipo igeuza TAA(Tanganyika Afrika Assosication) kua TANU (Tanganyika African National Union), hapa hata uhuru bado.
“Leo hii tunajaribu kukimbia the same race, baada ya historia yote hiyo, tunataka watu wetu washinde OSCARS ama watengeneze kitu cha kushindana na facebook, ama washinde miss world, tunataka watu wetu waweze shindana na mtu mweupe kwenye mifumo ambayo imejengwa kumfaidisha mtu mweupe”.
Swali la kijinga ambalo watu watauliza ni hili hapa
Kama mifumo imejengwa kumfaidisha mtu mweupe kwa nini kuna dangote na matajiri wengine weusi?
Jibu la kwanza -> Ili wachace wawe matajiri, wengi inabidi wawe maskini, na kuna matajiri wachache sana weusi, ambao wanafaidisha mifumo bado, dunia imekubaliana kwamba wachache wengi inaobidi wawe maskini ni watu weusi.
Jibu la pili – Hela za matajiri weusi wote zinaenda wapi? Mtu akinunua Ford, Audi, Porsche, Volkswagen, BMW, Mercedes benz na magari mengine mengi,wanatengeneza hela kutoka kwa watu weusi, wanaende kuwarudishia hela watu ambao babu zao waliuwa watanganyika Zaidi ya laki tatu na kuiba maliasili nyingi sana ili wenyewe waweze kwanza fika kipindi ambacho wantengeneza magari haya.
So ukiota kua tajiri ili ununue Mercedes, ujue watu laki tatu na Zaidi waliouwawa wana kugeuzia mgongo huko walipokua.
Wajerumani walianza kutengeneza automotives magari na vingine, kwenye miaka ya 1860, unafahamu nini kilikua kinaendelea Tanganyika/ east Afrika mwaka 1860? Watu walikua wanagombania na kugawana hii mipaka ya east afrika, wa Portugal waka nyanganywa na Waarabu, Germany na British wanagombania kugawana na kuchora mipaka ili watawale kila mtu na sehemu zake.
Tuzoom kidogo msatari wetu
MATAJIRI WEUSI WACHACHE WAMETENGENZWA ILI KWANZA TUAMINI KWAMBA WOTE TUNA UWEOZO SAWA NA MIFUMO IPO SAWA, PILI ILI WAKUSANYE HELA VIZURI NA KUWARUDISHIA WENYE NGOZI NYEUPE.
ILI KUTENGENEZA HELA INABIDI UTENGENEZE THAMANI, ILA UKIWA MWEUSI THAMANI YAKO HAITHAMINIWI NA WATU WALIOTENGENEZA MIFUMO INAYOELEZEA THAMANI NI NINI.
Aisee, watu wamepotea sana, comment kama hii hapa chini.
Na ukizingatia Tanzania ndipo mifupa ya binadamu wa kale kabisa ilipopatikana, inasikitisha.
Kama mungu unaemtaja hapo na unamuamini kweli yupo, ni kweli wenye upendo na Amani, basi amesha walaani sana wakoloni kwa waliofanya, na yupo upande wetu tuweze fanya kesho ambayo hawakuwai iwaza.
KESHO
Mfumo wa capitalism (ubepari) ndio imetuleta hapa tulipo.
Kesho ya hivi tunaifanyaje? Kesho ambayo afrika ndio bara la kwanza kwa kila sector, kesho ambayo nywele na ngozi za watu weusi za watoto wetu zinapendwa na kukubalika kama zilivyo, kesho ambayo afrika inarudi kua wakwanza kama ilivyotakiwa iwe, Sina majibu yote, nitaandika nyingine kujaribu address kesho lakini kama umeisoma na umeelewa na una cha kuchangia, tafadhali changia, nakubali nikosolewe ila tafadhli weka link kama unasema kitu, usichangie kama hauna facts, hiyo ndio njia nyingine wametushika akili, kukubaliana na vitu bila kuwa na ukweli, bila kua na facts.
Kesho ni kuangalia makosa yote yaliyofanyika. Kujadili na kuweza kukua, bila hivyo sidhani kama tutaweza epuka vikwazo ambavyo hatuvioni vilivyowekwa na wakoloni.
We have to reckon with our history, there is no other way around it.
“I write nikiwa inspired” niliandika kwenye makala yangu ya kwanza.
Kuna swali ime ni inspire, imenisikitisha, imenipa uzuni, kwa jinsi gani mtu mweupe, the white man, amefanikiwa kuua uwezo wa wengi sana kujiamini na kuweza kwenda mbele, swali linauliza: Je, mungu kaumba baadhi ya wanadamu kwa upendeleo wa akili na maarifa?
Nikiisoma nakaribia hadi kutapika, kwa kua mtu mweusi kaandika hii. Na anazidi danganya na kupeleka mbele mfumo uliotengenezwa na watu weupe, wa kuua, kurudisha nyuma, kuchochea na kufanya wanadamu wadhani kwamba ukizaliwa na ngozi ambayo ni nyeusi we si mwanadamu kamili na inabidi utawaliwe.
Kwanza nikajua kama utani flani hivi, ila nikaingia kwenye comments na wengi wanakubaliana nae.
Mimi sio mwana historia, kuna mengi sijui bado na najifunza kila siku, kama kuna fact nimekosea ntakubali kuelezewa Zaidi na kukosolewa.
Soma Hii Polepole na Kwa makini sana, systems(mifumo ya dunia) hazitaki ujue Zaidi. Rudi usome tena, click link zote kuthaminisha (ni ndefu kidogo).
Jana
Ninaposema jana namaanisha historia, the past, vitu gani ambavyo vimetuleta hadi kufikia hapa tulipo, maana hauwezi, akili haitokuja kufunguka kama hujaisoma historia.
Kwenye report yangu ya form 4, history ndo somo pekee ambalo nilipata F. Sikua na hamu nayo, sikuipa a second thought, nilifikiri tu kwamba mambo yashapita, mimi kukariri miaka na majina na matukio itanisaidia nini. Fast forward miaka kumi mbele, hamna kitu ninachopenda kisoma kama historia. Natafuta vitabu vya researchers wa african history, natafuta makala, video, audio kuelewa kwanini leo ipo hivi ili kesho niifanye tafauti, na huu ndio umuhimu wa jana, umuhimu wa historia.
Mifumo inakwambia kwamba, ohh we ni maskini, na vyote ni juu yako, fanya kazi kwa bidii, usipofanikiwa, ukifa bila kufanikiwa, vyote ni juu yako, ambacho hawataki kukubaliana nacho ni kwamba kilichofanyika jana, ndicho kinachowafanya watu wawe hivi leo, ndicho inachofanya kesho yetu isije kwa manufaa.
Tuchukulie mfano, jana mtu alikuja na tofali akakuvunja miguu, alafu leo mnaanza kwenye mstari mmoja kushindana kukimbia, mnaanza wote, wewe unajivuta kwa nguvu zako zote, yeye anakimbia haraka alafu anakucheka, “muone huyo mtu hawezi kukimbia vizuri” anasema.(ngoja nikuchoree mstari wa kwanza).
Unaweza usiamini kwamba hicho ndo sababu mamilioni ya watu weusi ni maskini hadi leo na watazidi kua maskini kesho, lakini ngoja niendelee, ngoja nikuchoree mistari, let me connect the dots.
FACTS
- Takribani miaka 200 tu iliyopita, kama generation tatu tu hadi kufikia tulipo hapa, nchi Tajiri zilikua zinautajiri mara tatu tu Zaidi ya nchi maskini.
- Baada ya miaka ya ukoloni kuisha kwenye miaka ya 1960 hivi, miaka ambayo wazazi wetu wengi walikuepo nchi tajiri zikawa tajiri Zaidi ya mara 35.
- Na hivi leo Nchi Tajiri zimepita nchi maskini kwa Zaidi ya mara 80.
FACTS
Jana, Mwaka 1960 Congo ilipopata uhuru kutoka kwa Belgium, wananchi wa congo waliomaliza chuo kikuu walikua 16 tu kati ya watu milioni 14. Leo congo ipo vitani, Belgium uchumi wake unafanya vizuri tu. (Tukumbuke kwamba walidai wanakuja leta maendeleo na kuwekeza mifumo yao)
Jana tarehe 29 february mwaka 1906, miaka 112 tu iliyopita, nkosi mputa gama, magodi mbano, njorosa mbano, zinanimoto gama, fratera gama, mtepa hawayi gama, mtekateka tawete, majiyakuhanga komba, moambalioto soko, songea mbano na mputa mkuzo gama walinyongwa pamoja na watu zaidi ya laki 3 kuuwawa kwaajili ya kupigania uhuru wa watanganyika kutoka kwa wajerumani.
Hawa watu walijua kwamba wazungu hawa ambao muuliza swali amesema basically ni wametengenezwa tofauti na mungu na wemepewa vya ziada ni waongo, ni watu wabaya ambao wanaua na kubaka, na kuchukua rasilimali, na kudanganya kua wanafanya mazuri huku watu wanaowafanyia mazuri maisha yao yanaenda chini, ukiwasifia wajerumani kwa ku invent chochote kabla ya Mtanzania, hawa watu wote waliokufa kutupigania wanakugeuzia mgongo huko walipo.
Kosa kubwa tunalozidi fanya ambalo mimi mwenyewe personally najaribu kuachana nalo ni slave mentality ama akili za utumwa ambazo bado zinaendelea kututawala.
SLAVE MENTALITY ni nini? Akili za utumwa ni nini?
Akili za utumwa ni kukubaliana na kusheherekea kitu chochote ambacho tulipewa jana kipindi cha utumwa, na kuchukua na kukubaliana navyo kama vyetu. Sito taja ni vingapi ambavyo tumepewa, maana vitu vingine ni nyeti sana na vimeshatuingia na kua foundation za wengi, so ili kuepuka na akili za utumwa, jiulize sasa hivi ni kitu gani unachokubaliana nacho ambacho tulipewa na mkoloni.
Jana Wakoloni walikubaliana (walidanganyana) kwamba muafrika hajielewi, muafrika hana uwezo wa kuendelea, muafrika hana akili, muafrika inabidi atawaliwe ili achangie na aweze endeleza mifumo ya dunia. Na wakaja na dini zao, vitabu vyao, na kuua, kubaka, kutesa kwa mda mrefu, hapa tanzania wakoloni kutoka magharibi kwa miaka zaidi ya 500, generation/ vizazi zaidi ya 8 vili chukuliwa kwamba sio watu, hawana uwezo, hawa ni babu na bibi zetu(hapa hatujaongelea wakoloni kutoka mashariki).
Kipindi chote hiki wakoloni nchini kwao wanajenga, wanasoma, wana innovate, wana tunga, wanafundishana, wanafanya kazi pamoja ili kukuza uchumi wao.
Wajerumani ndio waliofanya ukatili mkubwa sana kipindi cha maji maji rebellion, Tanganyika, na mengine mengi tu walifanya kwenye nchi zingine afrika.
August 4, 1905, kinjekitile alinyongwa ili kutishia mtu yoyote kujifanya kwamba anapigania haki za wa Tanganyika. Sijui kwanini hatuna siku ambayo tunapumzika na kusherekea ujasiri wake, alionganisha watu wote waachane na tofauti zao na kupigania uhuru wa Mtanganyika, na kuanzisha maji maji rebellion.
Walichokifanya jana ndicho kimetuweka hapa leo.
Makala ninayoijibu imeandikwa na mtu ambae bado ana akili za utumwa.
Kutoka miaka ya 1400 hadi kuja kufikia 1961, nchi hii yetu ilipokuja kupata uhuru tulikua tupo kwenye kipindi cha ukoloni, tulivunjwa miguu kwa miaka Zaidi ya 500, na leo wanatwambia tukimbie, tushindane tuone nani ambae anaweza fika mwisho wa kwanza. Tusisahau historia, msatari wa kwanza huo nimekuchorea kutoka jana hadi leo.
Leo
Uongo mkubwa wa leo ni kwamba mtu yeyote anaweza akawa tajiri kwenye mifumo hii, uongo mkubwa wa leo ni kwamba akifanya kazi kwa bidii mtu yoyote anaweza kujikwamua kutoka kwenye umaskini, uongo mkubwa wa leo ni kwamba watu ambao ni maskini ni maskini kwa kua hawajafanya kazi kwa bidii. uongo mkubwa wa leo ni kwamba mimi na wewe tulikua, na wengi wetu wenye ngozi kama zetu watazidi kua maskini kwa ajili hatuna uwezo wa kufikiria kama watu wenye ngozi tofauti na zetu.
Hela ni nini? Zinapatikanaje? Zinatengenezwa vipi? Mtu akifa anamuachia nani? Hela zipo ngapi duniani? Benki zinafanya vipi kaizi? kwanini thamani ya hela inapanda na kushuka? kwanini hata kama nchi ina rasilimali nyingi wananchi wake bado maskini?
Ukifanya uchunguzi unaweza jibu maswali yote hayo juu, na ukishayajibu, ujiunge kwenye upande wa kushangaa ni jinsi gani mifumo ya dunia ilivyowekwa kumfanya mtu mweusi abaki maskini.
Leo hii kuna lodge ngorongoro, ambayo ina milikiwa na watu wenye ngozi nyeupe ili watu wengine wenye ngozi nyeupe wakija kufanya utalii hela zao zinazunguka kati yao, serikali inakata makato lakini majority of pesa inarudi kwao, haiendi kuzunguka kwa wananchi ambao hali zao ni za kati, wala wenye maisha ya chini. Kwenye pita zangu nmekutana na watu wawili ambao budget yao ya wiki hapa nchini ni takriban milini 20 za kitanzania.
Leo hii, nchi tajiri zinakuja kusaidia africa na kutangaza kwamba wanasaidia Nchi za Afrika, wanaleta bilioni kadhaa, lakini kwa mifumo walioiweka rasilimali wanazozitoa kwenye nchi za Afrika zina thamani ya Trilioni kadhaa, lakini kupitia mifumo kama Trade mispricing, kwamba receipt ambazo zinalipwa sio za kweli na haziendani kabisa na maliasili ambazo wanachukua, na kulipia bei ndogo sana kwa ajili ya maliasili za kutengeneza mabilioni, jiulize ni mfumo gani ambao una panga bei ya thamani za rasilimali?
Na swali lingine la kujiuliza ni kwamba leo hii thamani ya hela ni nini? Dollar za kimarekani 9,400 ni sawa na million 20 na za kitanzania, tumefikaje hapa leo hii?
Leo ni maswali tu sana sana, kwa kua leo hali iliyopo inabidi itufanye either tubadili mifumo ili mtu mweusi aweze fanikiwa, ama tukubaliane na mifumo.
Turudi jana Tena (tutafika kesho ngoja kidogo).
-Tunaambiwa jana kwamba muafrika hakua na uwezo wa kufikiria, tunaambiwa. Tunaambiwa uongo, what are the facts, ukweli ni nini? Jana ilikuaje? Turudi nyuma, kabla ya ukoloni, turudi nyuma Zaidi, historia ambayo hata mashuleni kufundishwa ni ngumu, hivi jiulize kabla ya ukoloni, wa afrika walikuaje, waligundua nini, walikua wanafikiria nini, Afrika mashariki ilikuaje, kabla hawajachora mistari kugawana vipande vya afrika ambavyo leo tunaita mipaka, kabla hawajaanza kutujaza na akili za utumwa ilikuaje?
Industrial revolution, yaani kipindi cha viwanda kuanza, kimejengwa na damu na jasho la mtu mweusi, kila nchi ambayo ilianza kufanikiwa kwenye miaka ya 1760 kwenda 1800 hivi ni nchi za wakoloni. Ni nini Kilichokua kinaendelea Tanganyika kipindi ambacho industrial revolution kinaanza kwenye nchi za magharibi?
Kipindi cha miaka hiyo, kiliitwa the scramble for afrika yaani nchi za afrika zimefanywa kama biskuti hivi ambazo wamepewa watoto wa darasa la kwanza kugawana, Germany, british, france, Belgium, Portugal, Italy nchi zote hizi na zingine zimefaidika kwa damu na jasho la watu weusi, kisha leo tunashindana kwenye uwanja mmoja.
Ukisema mtu mweusi hana akili ya kufikiria kama mtu mweupe, mamilioni ya watu, waliokufa na kuuliwa ambao labda wangekuja kua madaktari, wana sayansi na vingine vingi ambavyo watu ambao maisha yao yamekatwa wanakugeuzia mgongo.
Textile, nguo hizi ndio ilikua viwanda vya kwanza kufanikiwa, na vilifanikiwa vipi? Kwa kuwaweka watu weusi kwenye mashamba yao ili kuwapatia pamba na vitu vingine, mashamba ya kwenye colony zao, mashamba ambayo wamechukua watumwa kuwarudisha kwao, mashamba ambayo damu zimetoka za watu weusi.
Kutoka Wikipedia:
“The Industrial Revolution marks a major turning point in history; almost every aspect of daily life was influenced in some way. In particular, average income and population began to exhibit unprecedented sustained growth”
Facts
Hii video ndefu sana, ila ukiiangalia yote utafaidika sana na historia.
Robin walker ni mwana historia, ambae ana institution inayo fanya uchunguzi wa historia ya afrika, na wanagundua vitu vipya kila siku, historia ya kweli sio ambayo tunaambiwa na wakoloni kila siku.
Ndani yake kwenye dakika ya 21 hivi, Robin walker anasema kwamba
“Kilwa was considered one of the most beautiful and well constructed cities of the world” anasema
Mji wa kilwa ulijengwa karne ya kumi, yani 900 AD na kisha kuongezewa karne ya 15, miaka ya 1400 hivi, kabla ya wakoloni kuja, kabla hawajasema kua wa Afrika wote wanaishi kama wanyama tu hawana maendeleo, na inabidi kutawaliwa, miaka Zaidi ya 400 kabla hawajaanza kuja kuua na kufanya watu wawe watumwa.
Miaka ya 1200 hivi, karne ya 13, east Africa walikua wamejenga vyoo, na majengo ambayo Miaka Zaidi ya 600 kabla wakoloni hawajaja, civilization ilikua inafanya kazi vizuri kabisa, tulikua na majengo ambayo magharibi wanayaota. Mji wa lamu, ambao upo Kenya, unasemekana ulijengwa miaka ya 1370.
Waswahili walikua watu mahiri sana, Swahili settlement zilijenga na ku innovate mambo mengi sana ambayo yanafichwa na historia, historia inayofundishwa ni version ya mkoloni, kwamba civilization afrika ilianza kipindi ambacho walikuja wao, miaka ya 1700-1800 hivi. Ni uongo mtupi. Jana haikua hivyo jana na juzi yetu wameifuta ili kutengeneza leo ambayo tunaamini ka mtu mweupe ana uwezo Zaidi yetu, tupilia mbali mtu yoyote ataewaza hivi, mgeuzie mgongo leo kabla hatujaenda kukutana na mababu zetu waliokua na akili kuliko hawa watu waliokuja kuwauwa na kuwalzimisha kujiunga nao na kuwapa rasilimali kwa kutumia mdomo wa bunduki.
Leo
Leo tunakubaliana kwamba ngozi nyeupe ina uwezo wa kufikiria kuliko watu wenye ngozi nyeusi, kweli akili za utumwa zimefanikiwa kujengwa na wakoloni.
Leo nusu ya cobalt, maliasili ambayo inatumika kutengeneza simu hizi, ambazo dunia nzima tunatumia inatoka congo, inatoka afrika, na wananchi wa congo ni maskini wanaambiwa kwamba hawana uwezo wa kufikiria kama mkoloni, DRC inabidi iwe kama sio nchi tajiri namba moja basi iwe kwenye top 3, maana ndipo wenye upatikanaji mkubwa wa cobalt, copper, diamond, tantalum (inapatikana kwenye simu, computer, dvd player, video games na vingine) na tin, kwanini na vyote hivi Congo sio tajiri, Mifumo ama systems.
Leo tunajaribu na tunakubaliana kwamba tunaweza kua kama Steve Jobs, Mark zuckerberg, Bill Gates ana wengine wambao ni watu wenye ngozi ambazo sio nyeusi, wakati apple inazidi kua tajiri, wakati wakiingi congo wananyonya maliasili ambazo wanaenda kutengenezea Iphones kisha wanarudi kutuuzia hukuhuku afrika, wakati most computers ambazo zinatumia windows zinatumia mali asili za afrika, na badala ya kulipa thamani yake kweli wenyewe wanalipa visenti ili kwenda kuuza bidhaa zao mamilioni. Wamefanikiwa kutengeneza thamani kwa ajili ya kipindi cha ukoloni, na leo vitu vinavyotoka kwa vina thamani kuliko vinavyotoka kwetu.
Leo Hii ukoloni haujaisha, na tusipo amka, kesho haitakua nzuri kabisa.
Uwongo mkubwa wa leo ni kwamba hela ikienda kwa mtu mmoja, hiyi hiyo inaweza kwenda kwa mtu mwingine na yeyote akifanya kazi anaweza kua tajiri kama billgates, thamani haipo hivyo huu ni uongo.
Hivi apple, iphone? jana babu zenu wamebaka, wameua, mmechukua watu weusi kwenda kutengeneza mifumo yenu kurahisisha na kuendeleza uchumi, jana mmefanya watu wawe watumwa, jana mme fanya watu waishi chini ya ukoloni, leo hii mnalipa vi centi ili kupata maliasili, watoto wadogo wanachimba haya madini mnayotumia, na nyie mnatengeneza mabilioni kuuza simu, na kweli dunia nzima tunaangalia apple kama watu wanaotengeneza hela kimaadili?
Na hizi sio siri, ukisearch google ama youtube unaona yanayoendelea. Sio siri, yote yapo wazi.
Hivi battery za simu zote zingetengenezwa Congo, na magari yanayotumia battery yange tengenezwa Congo, alafu nchi ambazo zingenunua hizi simu na magari walipe thamani yenyewe kabisa, congo ingekua maskini, hivi kama kampuni kuchukua cobalt kuweka kwenye battery zake ingebidi ilipe thamani kubwa, la sivyo ijenge viwanda vyake nchini humo ama iwekeze nchini, kuna mtu angepigana unadhani, kuna vita ingetokea?
Hakuna vita Afrika ambayo haijasababishwa na wakoloni kuanzisha, au kusababisha na kuchochewa na mmarekani, and that is fact.
Misaada wanayofanya ni ujinga mtupi.
Watu milioni 13 wanahitaji misaada congo leo, ndio vichwa vya habari vinavyosema leo, lakini hatu address lasirimali wanazochukua, walizochukua, na watazozidi chukua kila siku, aisee mkolini amefanikiwa kusukuma hoja zake kwenye akili za watu.
Eti leo, wanataka okoa wakongo kutoka vitani, vita ambazo wamezitengeneza wenyewe.
Hela zozote wanazotoa wasiziite msaada, nchi yoyote ambayo imeshirika kwenye ukoloni inahitaji kusema kwamba wanalipa walivyoiba, sio msaada.
Ukinivunga miguu leo, alafu kesho unaambia ndugu zangu kwamba eti ohh, namsaidi kwa kumpeleka hospitali, hapana, haunisaidii, unalipa ulichofanya, na nikipona, tutaonana kesho.
Main Thing/kitu muhimu cha kujua na kuelewa kabla ya kwenda kesho.
Na nili comment hili kwenye makala nnayoijibu, everything is gradual, inabidi tuanze A ili kufika B, ndipo tutapoweza fika K, hadi W.
Sio Mtu mmoja ambae anaweza kufikiria kila kitu, mark zuckerberg alitumia PHP kutengeneza facebook kwa idea ambayo aliiba kutoka kwa watu walioitunga, PHP ilibidi itengenezwe kwanza na watu wengine, na lugha ambayo miaka mingi sana imejengwa polepole, je ni kweli wa afrika tulishindwa kutengeneza lugha za programming kabla ya wakoloni?
Hapana, PHP imetengenezwa mwaka 1994, na watu ambao baba zao na bibi zao hawajapitia utumwa na ukoloni.
Hivi watu wote waliouliwa na kuteswa na kubakwa, unadhani hata mmoja wao alikua hana uwezo wa kuja kupata mtoto au mjukuu ambae angekuja kutengeneza lugha ya programming?
unadhani kama mda wote huo watu wangekua hawakimbii na hawaogopi kuuliwa, wanapeleka watoto wao shule, na wanafundishana na kufanya kazi pamoja, na ukiweka rasilimali zote tulizonazo, mkoloni angetufukia? Hapana, na wote wanajua hili ndio maana mifumo bado ipo na inafanya kazi hadi leo, na wamefuta historia kabla ya ukoloni.
Lugha ya kwanza ya kutengenezea program (programing languages) iliyotumika na ilitengenezwa mwaka 1954, unajua nini kilikua kinaendea Tanganyika mwaka huu? Mwalimu Julius Nyerere na Oscar Kambona ndipo walipo igeuza TAA(Tanganyika Afrika Assosication) kua TANU (Tanganyika African National Union), hapa hata uhuru bado.
“Leo hii tunajaribu kukimbia the same race, baada ya historia yote hiyo, tunataka watu wetu washinde OSCARS ama watengeneze kitu cha kushindana na facebook, ama washinde miss world, tunataka watu wetu waweze shindana na mtu mweupe kwenye mifumo ambayo imejengwa kumfaidisha mtu mweupe”.
Swali la kijinga ambalo watu watauliza ni hili hapa
Kama mifumo imejengwa kumfaidisha mtu mweupe kwa nini kuna dangote na matajiri wengine weusi?
Jibu la kwanza -> Ili wachace wawe matajiri, wengi inabidi wawe maskini, na kuna matajiri wachache sana weusi, ambao wanafaidisha mifumo bado, dunia imekubaliana kwamba wachache wengi inaobidi wawe maskini ni watu weusi.
Jibu la pili – Hela za matajiri weusi wote zinaenda wapi? Mtu akinunua Ford, Audi, Porsche, Volkswagen, BMW, Mercedes benz na magari mengine mengi,wanatengeneza hela kutoka kwa watu weusi, wanaende kuwarudishia hela watu ambao babu zao waliuwa watanganyika Zaidi ya laki tatu na kuiba maliasili nyingi sana ili wenyewe waweze kwanza fika kipindi ambacho wantengeneza magari haya.
So ukiota kua tajiri ili ununue Mercedes, ujue watu laki tatu na Zaidi waliouwawa wana kugeuzia mgongo huko walipokua.
Wajerumani walianza kutengeneza automotives magari na vingine, kwenye miaka ya 1860, unafahamu nini kilikua kinaendelea Tanganyika/ east Afrika mwaka 1860? Watu walikua wanagombania na kugawana hii mipaka ya east afrika, wa Portugal waka nyanganywa na Waarabu, Germany na British wanagombania kugawana na kuchora mipaka ili watawale kila mtu na sehemu zake.
Tuzoom kidogo msatari wetu
MATAJIRI WEUSI WACHACHE WAMETENGENZWA ILI KWANZA TUAMINI KWAMBA WOTE TUNA UWEOZO SAWA NA MIFUMO IPO SAWA, PILI ILI WAKUSANYE HELA VIZURI NA KUWARUDISHIA WENYE NGOZI NYEUPE.
ILI KUTENGENEZA HELA INABIDI UTENGENEZE THAMANI, ILA UKIWA MWEUSI THAMANI YAKO HAITHAMINIWI NA WATU WALIOTENGENEZA MIFUMO INAYOELEZEA THAMANI NI NINI.
Aisee, watu wamepotea sana, comment kama hii hapa chini.
Na ukizingatia Tanzania ndipo mifupa ya binadamu wa kale kabisa ilipopatikana, inasikitisha.
Kama mungu unaemtaja hapo na unamuamini kweli yupo, ni kweli wenye upendo na Amani, basi amesha walaani sana wakoloni kwa waliofanya, na yupo upande wetu tuweze fanya kesho ambayo hawakuwai iwaza.
KESHO
Mfumo wa capitalism (ubepari) ndio imetuleta hapa tulipo.
Kesho ya hivi tunaifanyaje? Kesho ambayo afrika ndio bara la kwanza kwa kila sector, kesho ambayo nywele na ngozi za watu weusi za watoto wetu zinapendwa na kukubalika kama zilivyo, kesho ambayo afrika inarudi kua wakwanza kama ilivyotakiwa iwe, Sina majibu yote, nitaandika nyingine kujaribu address kesho lakini kama umeisoma na umeelewa na una cha kuchangia, tafadhali changia, nakubali nikosolewe ila tafadhli weka link kama unasema kitu, usichangie kama hauna facts, hiyo ndio njia nyingine wametushika akili, kukubaliana na vitu bila kuwa na ukweli, bila kua na facts.
Kesho ni kuangalia makosa yote yaliyofanyika. Kujadili na kuweza kukua, bila hivyo sidhani kama tutaweza epuka vikwazo ambavyo hatuvioni vilivyowekwa na wakoloni.
We have to reckon with our history, there is no other way around it.