unaweza kudadavua zaidi hii post mkuu?
Hebu ngoja tuwekane sawa hapa
Haya makadirio huwa yanapotosha sana kwasababu vigezo
wanavyotumia ni kama alexa ranking na (yahoo/google)
backlink.
Tatizo la alexa ni kuwa siyo wote wanaotumia hiyo addon
kwenye browser zao kwahiyo data zao siyo sahihi.
-
Nilazima udownload alexa addon kwenye browser ili waweze
kukusanya data
Tatizo lingine ni kwamba mapato ya website yanategemea na
aina ya traffic. Unaweza kuwa na traffic kubwa sana (according
to alexa) kama ya twitter lakini ukashindwa kui-monetize.
Mfano mzuri ni
facebook ambayo ina
traffic kubwa sana lakini
mapato yake ni chini ya $1 billion kwa mwaka wakati huo huo
mapato ya
google ni $23 Billion kwa mwaka.
Hii ni kwasababu watu wanapotumia google huwa wanatafuta
information kwa hiyo wanakuwa katika mood ya ku-click aidha
ads au SERP (search engine result pages). Wakati wale wa
facebook wanakuwa katika mood ya kuangalia nani kafanyanini.
Hivyo sirahisi kwa wao ku-click facebook ads ndiyo maana
mapato yake hayaendani na traffic yake.
Wanasema makadirio ya mapato ya
Google ni $3,400,153.46
kwa siku, Hii siyo sahihi kwasabau Google wanatengeneza zaidi
ya $60 million kwa siku.
Mfano mwingine ni hii website ya magicofmakingup.com,ambayo
ni namba moja clickbank kwenye mambo ya
self help. Huyu
jamaa anauza kijitabu chake pale clickbank na anatengeneza
zaidi ya $2,000 kwa siku lakini hawa jamaa wa sitetrail.com
wanasema hii website inatengeneza $144 tuu kwa siku, gimme
a break.
- Kwahiyo hizi estimation zinapotosha.
Zamani jamiiforums walikuwa wanaweka adsense ads lakini
wakazitoa kwasababu zilikuwa hazilipi (according to invisible).
Mimi kwakuwa kwenye hii industry kwa muda mrefu nakubaliana
kabisa na invisible kwasababu google ads zinawekwa kutokana
na content. Lakini CTR ya ads inategemeana na relevance ya
contents ana ads.
Google huwa wana-parse content ili waweze kuamua ni ads
gani zitafaa kwenye hiyo page.
Sasa google bots wakiona content za jamiiforum zenye maneno
kama "Dr Slaa wa Tanzania", "mkuu wa mkoa wa kilimanjaro",
"maandamano ya Arusha" system yao kwa kutukia technologia
kama probabilistic latent semantic indexing wanaweka ads za
Tanzania safari, cheap flight to Tanzania ambazo siyo relevant
na contect.Hii ni kwasabu wanao advitise maneno kama Tanzania
au Arusha hulenga watalii wa magharibi wanao kuja kutalii
mbuga za wanyama Tanzania .
Sasa tatizo linakuja kuwa watumiaji wa jamiiforum wengi
hawahitaji kujua what is the cheapest Tanzania safari. kwahiyo
hawawezi ku-click, matokeo yake impression inakuwa kubwa
lakini clicks chache (Low CTR).