Jamii tuzungumze kuhusu baadhi ya wababa na matunzo kwa watoto

Jamii tuzungumze kuhusu baadhi ya wababa na matunzo kwa watoto

Dkt. Gwajima D

Minister
Joined
Nov 28, 2015
Posts
1,706
Reaction score
8,657
1759493445739.jpeg

Wasalaam.

Jamii tuzungumze tubadilishane mawazo kidogo.

Malalamiko mengi kuhusu watoto kutelekezwa, kwenye upande wa mtelekezaji, mara zote anakuwa baba watoto😭, kwa nini lakini? Napokea mengi mengi, inasikitisha, tuzungumze kidogo.

Ndugu BAADHI YA WABABA; tunzeni watoto wenu tafadhali. Unakuta wababa wengine mmejaaliwa afya njema kabisa, kazi ya heshima ofisi ya umma au binafsi tena na cheo juu, wengine na biashara za kipato kabisa, bado kweli mnashindwa kuwa kielelezo cha baba mwema, kutwa mashtaka ya huyu hatunzi watoto wake, kawatelekeza, mama nahangaika peke yangu, watoto wanalia na kujuta. Kweli?

Unasikiliza, unamwangaliaa, unamtafakari unasema Eeh Mungu, mfunulie huyu ajue majukumu yake kuhusu baraka ulizompa.

BAADHI YA WABABA; Hivi kweli tuanze kuwatuma maafisa ustawi wa jamii huko ofisini kwenu na mwisho mabossi wenu wajue halafu mje mtulaumu? Wengine mnapelekwa mahakamani na hukumu ikitoka hamtekelezi hadi mivutano.

BAADHI YA WABABA; Mjitafakari, haipendezi hata kidogo, mmebarikiwa, msituongezee kazi za kuwataka mtimize majukumu yenu kwa njia ambazo zinaweza kumfanya Mwenyezi Mungu aondoe baraka zake.

Nasema BAADHI YA WABABA maana, ni nadra sana kusikia kesi za WAMAMA kutelekeza watoto.

Pongezi ziwafikie Wababa wote wanaoshirikiana vema na wamama au wazazi wenzao wa kike kutimiza wajibu wao.

Hivi hawa baadhi ya wababa wana shida gani hadi mioyo yao inakuwa migumu hivi na kuathiri watoto wasio na hatia halafu, wanaharibu utambulisho wa mwanaume kuwa, ni mbeba maono ya taasisi ya familia? Haya maono gani sasa haya? Wanafeli wapi?

Tubadilishane mawazo maana najua humu JF wababa na wamama wote ni wema kabisa 🌹na maoni yao yatakuwa mema kabisa....
 
Usijizime data mheshimiwa. Usijisahaulishe vimbwanga vyenu nyie wanawake kwa waume zenu kiasi cha kuzikimbia hata hizo familia na watoto
Sasa watoto wanahusikaje? Kiongozi huonesha njia kwa wanyonge. Kwa hiyo hapo baba anakuwa amejizima data za uongozi au? Ili nijue sasa kumbe uongozi kwenye familia ni mtihani hata kwa baadhi ya wababa ...
 
Sasa watoto wanahusikaje? Kiongozi huonesha njia kwa wanyonge. Kwa hiyo hapo baba anakuwa amejizima data za uongozi au?
Mambo haya umeyasema hutokea sana ndoa zinapoyumba na kuvunjika. Hivi unafaham rate ya ndoa kuvunjika na unawajua ni akina nani wanaongoza ku file kesi za divorce kati ya mume na mke?

Mnawa push wakina baba nje ya maisha ya watoto wao tena kwa kashfa nyingi mnooo halaf kwa kigezo cha gender mahakama zinawapa upendeleo mkubwa sana na kuwakandamiza akina baba, halaf mwisho wa siku mkipata mnachotafuta (kuvunja ndoa) mnarudi bado kuwa harras wanaume kuwa hawatunzi watoto!! Mna akili nyie kweli?
Screenshot_20250610_085134_Lite.jpg
 
Muwe mnawapima na DNA hao watoto, na mtoe majibu sahihi si hadi watu wakapime Kenya.

Kuna watu katika magomvi wanaambiwa watoto si wao na vitimbi vya wanawake ni vingi mno. Halafu yakifika kwenu mnawapendelea wanawake na kuwakandamiza wanaume.

Japo ni kweli kuna mataahira machache yanatelekeza watoto na wake zao bila sababu zenye mashiko
 
Kuna wanawake ni waongo waongo sana nyakati nyingine. Kuwa makini na ndimi zao kabla ya kumshushia rungu Baba.
Mimi siegemei upande kwa sababu tu wamelalamika, tunafikia hadi kuwaita wote na kuwasikiliza, ila mwisho wa siku hakuna matokeo. Tunachukua watoto kwenye makao ya watoto. Sasa kama mama watoto mkorofi, wewe baba si uchukue wanao? Au lipia huduma zao? Hapo vipi
 
Wanawake hutumia mtoto kama fimbo ya kumnyanyasa mwanaume ikiwemo kuacha kabisa kumtii na kuanza kumuomba vitu kwa amri hivyo kupelekea mwanaume kuwa na msongo wa mawazo na kususa.
Okay, umeona sasa kuwa, maamuzi ya nioe au nianze mahusiano, yanahitaji uchague sawa sawa na upime na ujue kuwa, nini utafanya ikiwa safari itaharabika njiani. Kuna washauri wa mipango humu leo walikuwa wanasema kupanga kupanga, sasa je, hii kupanga haiwezi kuanzia ngazi ya mtu na familia? Tuzungumze tafadhali
 
Mh. ukimaliza hili uzungumze kuhusu wamama kuwabambikia wababa watoto wasio wao. Pawepo na upimaji wa vinasaba pindi mtoto anapozaliwa kumjua Baba mzazi halisi wa mtoto. Ni ngumu mno kwa mwanaume kutelekeza damu yake.
 
Muwe mnawapima na DNA hao watoto, na mtoe majibu sahihi si hadi watu wakapime Kenya.

Kuna watu katika magomvi wanaambiwa watoto si wao na vitimbi vya wanawake ni vingi mno. Halafu yakifika kwenu mnawapendelea wanawake na kuwakandamiza wanaume.

Japo ni kweli kuna mataahira machache yanatelekeza watoto na wake zao bila sababu zenye mashiko
Sasa hapa jasiri mwongoza njia si ndiyo inatakiwa aje mapema ustawi wa jamii aseme, jamani kabla sijatelekeza hawa watoto hebu nisikilizeni mnishauri. Inakuwaje mnashindwana, hakuna hatua zaidi, unatelekeza watoto, wanaingia mtaani, wanafanyiwa ukatili mtaani au hata majumbani na wewe upo, mioyo hii ni kama huu wangu au wa yule au ikoje?
 
Back
Top Bottom