James Mwakibinga amuomba radhi Emanuel Nchimbi kwa kumchafua, ametubu hatarudia

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
Heshima kwenu wakuu,

Tarehe 16 Mwezi wa nane 2016 kuna mwanaccm aitwaye Mwakibinga, alitoa taarifa ya kumchafua Emanuel Chimbi. Taarifa yenyewe ni hii=>UVCCM wapinga wenzao kutumbuliwa na Kamati Kuu ya UVCCM, Wamvaa Mh Nchimbi

Baadae Emanuel Nchimbi akamtaka Mwakibinga alotoa hiyo taarifa amuombe radhi na kumlipa kiasi cha Bil 2 kama gharama za kumchafua.=>Dr. Emmanuel Nchimbi: Ninamtaka Mwakibinga aniombe radhi na kunilipa bilioni 2 kwa kuniita mwizi

Sasa leo naona jamaa katekeleza Matakwa ya Nchimbi. Jameni Vijana, acheni kukurupuka.

CC: Lizaboni , Tulime , Elli
 
Hawa ndiyo wanaoichafua CCM yetu. CCM inaonekana kichaka cha waropokaji na wepesi katika kujenga hoja. Ni aibu kwa Mwakibinga pamoja na wengine wenye hulka kama yake. LAKINI, ni uungwana kuomba msamaha. Ana bahati, angefanywa mbaya Mahakamani.

Mzee Tupatupa
 
Wanaandika kwa kuropoka ili kutafuta vyeo. Lizaboni ndipo anapowaacha kwa mbali
 
Nchimbi usikubali mpelekeshe akulipe afilisike! Kesho tujifunze kuacha kuropoka, kuacha kuambiwa nini cha kusema. uache kuambiwa namna ya kufikiri na chama!
Najua ameandika hapa ili kukwepa rungu la kisheria. Ila ukweli utajulikana soon
 
Wanaandika kwa kuropoka ili kutafuta vyeo. Lizaboni ndipo anapowaacha kwa mbali
Wewe ni mmoja kati ya mwanalumba aliyeshadadia ile taarifa ya mwakibinga anayoikana leo.

Kwa tamko hili mme-surrender kwa Nchimbi kwa kuwa hamna namna nyingine tena.
 
Nyinyi vijana wote wakurupukaji na waropokaji kama mmemeza moto mdomoni mwisho wenu mwaka huu baada ya uchaguzi wa ndani, nawashauri mjipange kwenda kufanya shughuli zingine za kuwaingizia kipato, uganga njaa wenu na vibaraka wenu wote mwisho July......
 
Kama ni Nchimbi yule nayemjua kashateuliwa hana time naye coz kashateuliwa kuwa balozi nchi FULANI hivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…