juvenile davis
JF-Expert Member
- Apr 13, 2015
- 4,752
- 4,449
Katika maisha ya ujana tunakutana na mambo mengi sana, mengine ya kutisha na mengine ya kawaida. Binafsi katika ujana wangu nimepitia mambo mengi mazito, nimeumizwa sana katika mapenzi na nimeumiza sana wanawake.
Kati ya kitu siwezi kusahau katika maisha yangu na namuomba Mungu anisamehe na najutia sana ni mambo mawili;
Jambo la kwanza: Nilikuwa na mwanamke ambaye alinipenda na nilidumu naye miaka minne katika mahusiano huku akinisubiri kwamba ntamuoa, lakini kiukweli moyoni mwangu sikuwa na hata wazo la kumuoa zaidi ya kumnyandua tu. Hadi pale ambapo alinishtukia kwamba mimi siyo muoaji na hadi sasa huyo binti ameolewa na kwa ndoa kabisa.
Alikuwa ni mwanamke mwema sana kiukweli, namkumbuka sana katika maisha yangu. Kinachoniuma zaidi na namuomba Mungu wa mbinguni anisamehe sana ile dhambi ni kwamba huyo dada ameshatoa mimba zangu tatu. Hakuna kitu najutia kama kumlazimisha atoe mimba zangu mara tatu.
Najua wengi mtasema kwanini alikubali kutoa, sababu ni kwamba alikuwa ananiogopa sana akihisi akikataa nitamuacha na kwa kuwa alinipenda na kuniamini basi hakutaka kuniudhi, kifupi alikuwa ananisikiliza sana. Nakukumbuka sana ewe dada na Mungu akupe maisha marefu na naomba unisamehe sana.
Jambo la pili: Ni kwamba nimewahi kutoka kimapenzi na shemeji yangu (rafiki wa mpenzi wangu). Kwa kweli inaniumiza sana juu ya unafiki wangu niliokuwa naufanya. Ewe kijana jitahidi sana kuwa kijana mwema kwa jamii na kwa Mungu ili usije ukajutia sana hapo baadae kwa makosa unayoyafanya leo. Mungu atusaidie sana.
Je, wewe ni lipi linakufanya huwa unaniumia sana ulilowai kumfanyia mpenzi wako?
Kati ya kitu siwezi kusahau katika maisha yangu na namuomba Mungu anisamehe na najutia sana ni mambo mawili;
Jambo la kwanza: Nilikuwa na mwanamke ambaye alinipenda na nilidumu naye miaka minne katika mahusiano huku akinisubiri kwamba ntamuoa, lakini kiukweli moyoni mwangu sikuwa na hata wazo la kumuoa zaidi ya kumnyandua tu. Hadi pale ambapo alinishtukia kwamba mimi siyo muoaji na hadi sasa huyo binti ameolewa na kwa ndoa kabisa.
Alikuwa ni mwanamke mwema sana kiukweli, namkumbuka sana katika maisha yangu. Kinachoniuma zaidi na namuomba Mungu wa mbinguni anisamehe sana ile dhambi ni kwamba huyo dada ameshatoa mimba zangu tatu. Hakuna kitu najutia kama kumlazimisha atoe mimba zangu mara tatu.
Najua wengi mtasema kwanini alikubali kutoa, sababu ni kwamba alikuwa ananiogopa sana akihisi akikataa nitamuacha na kwa kuwa alinipenda na kuniamini basi hakutaka kuniudhi, kifupi alikuwa ananisikiliza sana. Nakukumbuka sana ewe dada na Mungu akupe maisha marefu na naomba unisamehe sana.
Jambo la pili: Ni kwamba nimewahi kutoka kimapenzi na shemeji yangu (rafiki wa mpenzi wangu). Kwa kweli inaniumiza sana juu ya unafiki wangu niliokuwa naufanya. Ewe kijana jitahidi sana kuwa kijana mwema kwa jamii na kwa Mungu ili usije ukajutia sana hapo baadae kwa makosa unayoyafanya leo. Mungu atusaidie sana.
Je, wewe ni lipi linakufanya huwa unaniumia sana ulilowai kumfanyia mpenzi wako?