Mimi ni kijana ambae kwa sasa nina miaka 31, nimekuwa na mpenzi wangu ambae tumekuwa na uhusiano kwa takriban miaka 5. Kwa kuwa nilimtangulia chuo mwaka mmoja tulipanga mpaka apate kazi ndio tufanye taratibu za kuoana. Baada ya kumaliza masomo yake nilijitahid kuhakikisha kwamba anapata kazi katika mkoa ambao mimi nafanya kazi. Bahati nzuri alipata katika shirika moja katika wilaya nyingine ila ndani ya mkoa ule. Kutoka ninapofanyia kazi mimi mpaka kwake ni mwendo wa masaa matatu. Baada ya kufanya kazi kwa mwaka mmoja tukiwa tunatembeleana kila wkend na kila mtu anapopata mda mimi nilipata nafasi ya kwenda kusoma Shahada ya pili. Nilipofika chuoni Dar es salama nilianza kuiona tofauti za mawasiliano,mawasiliano hafifu na msg au Majibu ya mkato. Nilijitahid sana kujikaza kama mwanaume lakini hali iliendelea kuwa tete. Alichokuja kuniambia ni kwamba mimi na yeye basi, iliniuma kwa sababu tayari nilishaanza taratibu za kwenda kujitambulisha Kwao mwezi wa 4 '2013. Suala hilo limenifanya niwaogope wasichana kiasi kwamba kila ninaemuona naona ni wale wale. Najitahid kumuomba mungu lakini mpaka sasa kama binadamu hali hii ya hodí hainiishi na kwa sasa ni dhahiri nahitaji mke.