Mi nadhani sababu kubwa ni kukosekana kwa mawasiliano thabiti kwenye ndoa. Sawa mke/mmeo anaweza akawa hana kauli nzuri, hajitunzi, hakufurahishi kitandani etc. Swali ni kwamba je, mshawahi kukaa kulizungumzia hilo swala linalowakwaza? Na kutafuta solution kwa pamoja? Wengi wetu tukiona kasoro km hyo badala ya kuzungumza na mwenzi wako wewe unakimbilia mchepuko. Na hapo unakuwa unaongeza tatzo juu ya tatzo sababu kuna mambo ya maradhi nk.
Jambo la pili ni ukosefu wa ukweli na uwazi kwenye ndoa. Mnapokuwa kwenye ndoa nyinyi si wawili tena bali ni mwili mmoja..kwhy hakuna haja ya kuweka siri kwa mwenzi wako au kudanganyadanganya au kufanya maigizo. Haya maswala ya kuweka password kwny cmu yako ili iwejee?? Ni nn unachoficha mkeo/mmeo asikijue? nk nk. Hata km mkeo hapiki chakula vizuri mwambie kwa hekima na kama wewe unajua basi muelekeze kwa upendo, kuliko kuacha kula chakula chake bila kumwambia sababu ni nn.
Na jambo la mwisho ni kujiheshimu ww kwanza na kuwa na hofu ya Mungu. Km unajua thamani yako basi hutofanya kitendo cha kumuumiza mwenzi wako. Maana wewe kama mwanamke km unajua thamani ya mwili wako hutoweza kuruhusu mtu yoyote akutumie tu!
Na ukiwa na hofu ya Mungu utaheshimu kiapo mlichokula mbele ya madhabahu takatifu / mbele ya sheikh.