Jamani nini chanzo cha michepuko?

Jamani nini chanzo cha michepuko?

1.Sometimes wanawake tunasababisha cos kujisahau na kujiona wewe ndo wewe 2.nyingne wanaume wanakuwa busy kutafta pesa wakidhan pesa pekee ndo mwanamke anataka anarudi kachoka mbayaaa kumbe some we need their time though little their attention. And etc
3.Kutojua kujicontrol cos kutaman hakuishi hata kama umeoa/umeolewa ila ni kujicontrol tu na kumheshim mwenzio ulomchagua kati ya wengi maishani.ni hayo tu
 
Shetani hataki kuwa pekee yake hivyo sasa anashambulia kila idara ndoa,familia,pesa,kazi,taifa,biashata.Ni wakati wa toba na maombi.
 
Wanawake wengine tamaa ya vitu na mahitaji ambayo hawayapati kwa mume wa ndoa.

Mume hamlidhishi kitandani.

Kaolewa kama fashion

Kakuchoka.

Anajaribu kuona wanaume wengine wakoje kunako sita.

Your not enough for her. Hata kama anaomba poo, lakini haridhiki hauna amsha amsha kitandani.
Upo. So kuna factor nyingi sana mkuu. Zingine jazieni.
 
Pole sana mkuu ulipitia pagumu sana lakini nakupongeza kwa kuvuka salama ni wachache sana wenye busara na hekima kama wewe,na uyo mwanamke naamini kajifunza sana.
 
Unajuaje kama ina fika mwisho wa kina..!? Uliingiza rula kupima akasema hapo mwisho haya oanisha na yako au ww ukisikia ukunga unajua yes nmegusa utumbo!? Mkuu hawa viumbe ni wajanja sana hvo usijipe asilimia zote labda upewe na watu kama wawili( mkeo na mchepuko/x)
 
Mi nadhani sababu kubwa ni kukosekana kwa mawasiliano thabiti kwenye ndoa. Sawa mke/mmeo anaweza akawa hana kauli nzuri, hajitunzi, hakufurahishi kitandani etc. Swali ni kwamba je, mshawahi kukaa kulizungumzia hilo swala linalowakwaza? Na kutafuta solution kwa pamoja? Wengi wetu tukiona kasoro km hyo badala ya kuzungumza na mwenzi wako wewe unakimbilia mchepuko. Na hapo unakuwa unaongeza tatzo juu ya tatzo sababu kuna mambo ya maradhi nk.

Jambo la pili ni ukosefu wa ukweli na uwazi kwenye ndoa. Mnapokuwa kwenye ndoa nyinyi si wawili tena bali ni mwili mmoja..kwhy hakuna haja ya kuweka siri kwa mwenzi wako au kudanganyadanganya au kufanya maigizo. Haya maswala ya kuweka password kwny cmu yako ili iwejee?? Ni nn unachoficha mkeo/mmeo asikijue? nk nk. Hata km mkeo hapiki chakula vizuri mwambie kwa hekima na kama wewe unajua basi muelekeze kwa upendo, kuliko kuacha kula chakula chake bila kumwambia sababu ni nn.


Na jambo la mwisho ni kujiheshimu ww kwanza na kuwa na hofu ya Mungu. Km unajua thamani yako basi hutofanya kitendo cha kumuumiza mwenzi wako. Maana wewe kama mwanamke km unajua thamani ya mwili wako hutoweza kuruhusu mtu yoyote akutumie tu!

Na ukiwa na hofu ya Mungu utaheshimu kiapo mlichokula mbele ya madhabahu takatifu / mbele ya sheikh.
 
Back
Top Bottom