djesco
Senior Member
- Jun 26, 2013
- 166
- 52
Naomba niingie moja kwa moja kwenye mada KAMA IFUATAVYO:
Nimeoa na nina mke na mtoto mmoja, niko na mke wangu kwa miaka 6 sasa.Ni mtu ambaye tumetoka kijiji kimoja na shule tulisoma shule moja, maisha yetu ni ya kawaida tu ila tunapendana sana na kukwaruzana kupo kibinaadam,katika suala zima la chakula cha usiku nikimshika lazima maji ayaite mma,binafsi nililkuwa namuamini sana huyu mwananamke na kama ingetokea mtu akauliza ni nani anaamini kwamba mke wake hana mchepuko!?
Mie ningekuwa wa kwanza kunyoosha mkono, ila kumbe nilkuwa najidanganya.Mwaka 2013 alijiunga na mtandao wa kijamii wa facebook na kabla ya kujiunga aliniruhusu nami nikamkubalia mwaka huu mwezi wa pili nikamnunulia simu aina ya TECNO H6 ili mradi mama mtoto nae aende na wakati, aisee kumbe kumruhusu ajiunge na facebook na kumnunulia smartphone ili ajiunge whatsapp na mengineyo.
Lilikuwa ni kosa kubwa sana mara mambo yakaanza kubadilika mdogomdogo,kupewa unyumba ikawa mpaka mieleka na kuchana chupi vinginevyo sipati kitu,mara nikimuita kumuuliza kitu hata kama yuko sentimita moja kutoka mahali nilipo basi mpaka nirudie mara 3 ndo ataitika,simu kaweka pattern hata mpelelezi wa FBI hawezi kuzitoa ila alichokuwa hajui ni kwamba ile e-mail ya playstore nilimfungulia mimi na password nilimuwekea mie so e-mail naijua na password naijua ,majibu ya ovyo na mengine mengi ya kukera.
Ila yote nikawa namwambia mama mtoto umebadilika ila anayekuzuzua nitamjua akanibishia kuwa hana mchepuko mie nikamjibu sawa ila ipo siku nitajua na hatakuwa na la kuniambia akawa anabisha.Ilikuwa ni tarehe 06/076/2015 nikiwa likizo ambapo mke wangu aliamka asubuhi akawa analalamika anajihisi homa nikamshauri aende kazini akaombe ruhusa halafu arudi nyumbani na kwenda hospitalini ili ajue shida ni nini.
Akafuata ushauri wangu na kweli saa 5 asubuhi akawa amerudi nyumbani akiwa na dawa kibao alizopewa huko hospitalini.Siku ya 07/07/2015 jioni nikachukua simu yake nikawa nimeenda nayo kiwanjani ili nikague baadhi ya sms zake za whatsapp,fcebook,na zile za kawaida.
Kwa vile aliweka pattern mie nikaingiza mara 5 simu ikaomba e-mail na password nikaingiza ikakubali nikatoa option ya pattern ikawa free nikawa nafuatilia message za whatsapp mara ikaingia message imeandikwa,"hujambo kipenzi changu?" kuangalia jina limeandikwa "wanyumbani" nikai-trace ile namba kwenye M-Pesa maana ilikuwa ni namba ya Voda ikawa imeleta jina la huyo wa nyumbani,ni mtu ambaye namfahamu kabisa,niliumia sana,nikaendelea ku-chat kwa kujifanya mie ndo mhusika jamaa akafunguka weee then nikaamua kuachana nae.
Nikapiga screen shots yale mazungumzo na zile message nikazifuta ikabaki ile ya hujambo kipenzi,nikarudi nyumbani nikamkuta mama mtoto amelala homa imemkaba kweli jioni hiyo nikamwamsha nikampa simu afu nikamuuliza kwani wanyumbani ni nani!? Maana kakutumia meseji kwenye whatsapp hebu isome akaisoma afu akaniambia ni mtu fulani hakunificha nikazidi kumchimba akasema hajui ni kwanini jamaa aliamua kumtumia hiyo meseji.
Nikajifanya mjinga nikalala ila simu sikumpa asubuhi ya siku iliyofuata nikamchukua mtoto alikuwa anaumwa mapunye nikampeleka hospitalini,nikiwa huko nikaamua kuingia kwenye account yake ya facebook aisee nilitamani kulia sema nikajikaza kiume,nikarudi nikamwambia sasa mama mtoto jana ulikataa na leo unalo la kuniambia!? Akawa hana la kusema! Homa ikapanda mara mbili.
Nikamsubiri akapona nikaanza sasa kumuuliza vizuri aniambie ni kwanini aliamua kunisaliti!? Akasema ni shetani na hata yeye hajui,nikamuuliza tena je,alikuwa tayari kugeuzwa chombo cha starehe!? Akabaki mdomo wazi la kuniambia hana,nikamuuliza tena alikuwa na malengo gani na jamaa!? Hakuwa na jibu.
NAOMBA NISIWACHOSHE:
Mwisho wa siku nikaona ngoja nishirikishe mama yangu mie tukayaongea yakaisha na kasema harudii na amekoma na ananishukuru kwa jinsi nilivomuokoa kutoka mdomoni mwa mamba,hiyo ikaisha.
Juzi nikiwa ofisi moja hivi kukutana na mkubwa mmoja wa ofisi hiyo akawa anaongea dakika moja mara kanyeyuka kwenda nje kujibu simu na katika kufuatilia maongezi alikuwa analalamika kuwa mke wake ka-cheat na mwanaume mwingine,wiki mbili nyuma kuna dogo nusra apigwe hapa kitaa kisa aatoka na mke wa jamaa mwingine,na katika kufuatilia zaidi nimegundua michepuko imekuwa fasheni.
Sasa swali ni je,KWANINI KUCHEPUKA KUMEZIDI SANA SIKU HIZI!? KWANINI UMDANGANYE MKEO/MMEO KWA KU-CHEAT NJE!? KWA MDADA JE,UMEKUBALI KUGEUZWA TAMBALA LA DEKI KWA KUKUWA NA MCHEPUKO!?
Naomba tujadili hili na nini kifanyike
Asanteni
Nimeoa na nina mke na mtoto mmoja, niko na mke wangu kwa miaka 6 sasa.Ni mtu ambaye tumetoka kijiji kimoja na shule tulisoma shule moja, maisha yetu ni ya kawaida tu ila tunapendana sana na kukwaruzana kupo kibinaadam,katika suala zima la chakula cha usiku nikimshika lazima maji ayaite mma,binafsi nililkuwa namuamini sana huyu mwananamke na kama ingetokea mtu akauliza ni nani anaamini kwamba mke wake hana mchepuko!?
Mie ningekuwa wa kwanza kunyoosha mkono, ila kumbe nilkuwa najidanganya.Mwaka 2013 alijiunga na mtandao wa kijamii wa facebook na kabla ya kujiunga aliniruhusu nami nikamkubalia mwaka huu mwezi wa pili nikamnunulia simu aina ya TECNO H6 ili mradi mama mtoto nae aende na wakati, aisee kumbe kumruhusu ajiunge na facebook na kumnunulia smartphone ili ajiunge whatsapp na mengineyo.
Lilikuwa ni kosa kubwa sana mara mambo yakaanza kubadilika mdogomdogo,kupewa unyumba ikawa mpaka mieleka na kuchana chupi vinginevyo sipati kitu,mara nikimuita kumuuliza kitu hata kama yuko sentimita moja kutoka mahali nilipo basi mpaka nirudie mara 3 ndo ataitika,simu kaweka pattern hata mpelelezi wa FBI hawezi kuzitoa ila alichokuwa hajui ni kwamba ile e-mail ya playstore nilimfungulia mimi na password nilimuwekea mie so e-mail naijua na password naijua ,majibu ya ovyo na mengine mengi ya kukera.
Ila yote nikawa namwambia mama mtoto umebadilika ila anayekuzuzua nitamjua akanibishia kuwa hana mchepuko mie nikamjibu sawa ila ipo siku nitajua na hatakuwa na la kuniambia akawa anabisha.Ilikuwa ni tarehe 06/076/2015 nikiwa likizo ambapo mke wangu aliamka asubuhi akawa analalamika anajihisi homa nikamshauri aende kazini akaombe ruhusa halafu arudi nyumbani na kwenda hospitalini ili ajue shida ni nini.
Akafuata ushauri wangu na kweli saa 5 asubuhi akawa amerudi nyumbani akiwa na dawa kibao alizopewa huko hospitalini.Siku ya 07/07/2015 jioni nikachukua simu yake nikawa nimeenda nayo kiwanjani ili nikague baadhi ya sms zake za whatsapp,fcebook,na zile za kawaida.
Kwa vile aliweka pattern mie nikaingiza mara 5 simu ikaomba e-mail na password nikaingiza ikakubali nikatoa option ya pattern ikawa free nikawa nafuatilia message za whatsapp mara ikaingia message imeandikwa,"hujambo kipenzi changu?" kuangalia jina limeandikwa "wanyumbani" nikai-trace ile namba kwenye M-Pesa maana ilikuwa ni namba ya Voda ikawa imeleta jina la huyo wa nyumbani,ni mtu ambaye namfahamu kabisa,niliumia sana,nikaendelea ku-chat kwa kujifanya mie ndo mhusika jamaa akafunguka weee then nikaamua kuachana nae.
Nikapiga screen shots yale mazungumzo na zile message nikazifuta ikabaki ile ya hujambo kipenzi,nikarudi nyumbani nikamkuta mama mtoto amelala homa imemkaba kweli jioni hiyo nikamwamsha nikampa simu afu nikamuuliza kwani wanyumbani ni nani!? Maana kakutumia meseji kwenye whatsapp hebu isome akaisoma afu akaniambia ni mtu fulani hakunificha nikazidi kumchimba akasema hajui ni kwanini jamaa aliamua kumtumia hiyo meseji.
Nikajifanya mjinga nikalala ila simu sikumpa asubuhi ya siku iliyofuata nikamchukua mtoto alikuwa anaumwa mapunye nikampeleka hospitalini,nikiwa huko nikaamua kuingia kwenye account yake ya facebook aisee nilitamani kulia sema nikajikaza kiume,nikarudi nikamwambia sasa mama mtoto jana ulikataa na leo unalo la kuniambia!? Akawa hana la kusema! Homa ikapanda mara mbili.
Nikamsubiri akapona nikaanza sasa kumuuliza vizuri aniambie ni kwanini aliamua kunisaliti!? Akasema ni shetani na hata yeye hajui,nikamuuliza tena je,alikuwa tayari kugeuzwa chombo cha starehe!? Akabaki mdomo wazi la kuniambia hana,nikamuuliza tena alikuwa na malengo gani na jamaa!? Hakuwa na jibu.
NAOMBA NISIWACHOSHE:
Mwisho wa siku nikaona ngoja nishirikishe mama yangu mie tukayaongea yakaisha na kasema harudii na amekoma na ananishukuru kwa jinsi nilivomuokoa kutoka mdomoni mwa mamba,hiyo ikaisha.
Juzi nikiwa ofisi moja hivi kukutana na mkubwa mmoja wa ofisi hiyo akawa anaongea dakika moja mara kanyeyuka kwenda nje kujibu simu na katika kufuatilia maongezi alikuwa analalamika kuwa mke wake ka-cheat na mwanaume mwingine,wiki mbili nyuma kuna dogo nusra apigwe hapa kitaa kisa aatoka na mke wa jamaa mwingine,na katika kufuatilia zaidi nimegundua michepuko imekuwa fasheni.
Sasa swali ni je,KWANINI KUCHEPUKA KUMEZIDI SANA SIKU HIZI!? KWANINI UMDANGANYE MKEO/MMEO KWA KU-CHEAT NJE!? KWA MDADA JE,UMEKUBALI KUGEUZWA TAMBALA LA DEKI KWA KUKUWA NA MCHEPUKO!?
Naomba tujadili hili na nini kifanyike
Asanteni