Nikweli hasa wakazi wa Maeneo karibu ya Msitu wa Ngezi,ila serikali ilipiga marufu baada ya popo kuanza kuadimia,maana pia ni vivutio vya utalii katika msitu ule.Ila ni wale popo wakubwa,wanamafuta balaa.
Sasa kwa sasa ukikamatwa umemkamata popo ujue jela,watu wa maliasili wanakukamata.
Sasa hivi tunakula Panya buku,huku ni mlo wa kawaida sana tu,ndio maana nasema haya makabila ya huku na bara yanashabihiana sana.
Huku panya buku dili,na akionekana mtaani basi atakimbizwa mbio mbaya hadi apatikane,kisha watu wanamchoma wanamla,maana ni mzuri zaidi akichomwa.