Habari wana MMU wote . Nadhani ni wazima na kama kuna mtu ni mdhaifu basi tunamwomba Mungu amrejeshee afya kama zamani.
Tatizo langu wana MMU wenzangu ambalo limekuwa likinisumbua sana kupenda kuangalia makalio ya wadada . Yaani nikipishana tu mdada yeyote aliyefungasha siwezi kuvumilia lazima nigeuze shingo nyuma nimwangalie. Wakati mwingine huwa najitahidi kujikaza nisigeuke nyuma lakini mwisho naishia kugeuza shingo na kuangalia ili nijiridhishe nafsi yangu.
Hii tabia ilishawahi kuniaibisha mbele za watu kwani kuna siku moja nilipishana na dada mmoja aliyejaaliwa nikajikuta nimegeuza shingo kwa mda mrefu kuangalia kazi ya uumbaji , huku naendelea na safari yangu lakini shingo nimeigeuza nyuma ndipo nilipokutana na adha ya kutumbukia kwenye dimbwi la maji huku watu wote waliokuwa jirani wakinicheka .
Sasa hii tabia inanifanya niwe mtumwa . Na ninavyojiona nahitaji kabisa msaada wa ushauri wenu .
Tatizo langu wana MMU wenzangu ambalo limekuwa likinisumbua sana kupenda kuangalia makalio ya wadada . Yaani nikipishana tu mdada yeyote aliyefungasha siwezi kuvumilia lazima nigeuze shingo nyuma nimwangalie. Wakati mwingine huwa najitahidi kujikaza nisigeuke nyuma lakini mwisho naishia kugeuza shingo na kuangalia ili nijiridhishe nafsi yangu.
Hii tabia ilishawahi kuniaibisha mbele za watu kwani kuna siku moja nilipishana na dada mmoja aliyejaaliwa nikajikuta nimegeuza shingo kwa mda mrefu kuangalia kazi ya uumbaji , huku naendelea na safari yangu lakini shingo nimeigeuza nyuma ndipo nilipokutana na adha ya kutumbukia kwenye dimbwi la maji huku watu wote waliokuwa jirani wakinicheka .
Sasa hii tabia inanifanya niwe mtumwa . Na ninavyojiona nahitaji kabisa msaada wa ushauri wenu .