Jamani mwenzenu DSTV imenishinda

Jamani mwenzenu DSTV imenishinda

Mantombazane

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2014
Posts
579
Reaction score
367
Mimi ni mpenzi mkubwa wa mpira wa miguu hasa ligi mbali mbali duniani.

Nilikuwa nalipia DSTV Premium 139,000 wakapandisha mpaka 199,000, na sasa hivi wamenitumia ujumbe kuwa kuanzia kesho yaani Octoba 1, itakuwa 219,000. Nimekata tamaa kabisa kwani hiyo bei ni kubwa sana.

Nimeiangalia hiyo bei nikaona mpangaji wangu analipa 30,000 kwa mwezi, hivyo kwa bei hiyo atalipa kodi ya miezi 6 yaani 180,000 na atabaki na chenji ya umeme 39,000.

Uchunguzi wangu umegundua kuwa wengi wameacha kulipia kifurushi cha juu na kile cha kati kwasababu hata ukitoza kwa watazamaji wengine hutapata hiyo hela ya kulipia.

Wenyewe wanajitahidi kupiga simu kukumbushia malipo lakini ukweli wengi wetu tutakwama, labda wafikirie upya bei zao. Sasa hapa Azam ndio wangechangamka mapema ili tuachane na hawa Multichoice.
 
Leo cku ya 3 mfululizo napigiwa sim na wafanyakaz tofauti kwa nn sijalipia na kila anayepiga namchana clear kua gharama zimepanda sana!!
 
Mimi nishakitupilia mbali kingamuzi chaoo long time agooo.garama zao it's to muchhhh
 
huu ni unyonyaji wa wazi kabisa.... mi wananijazia tu ma-email yao yakijinga wakati niliisha acha kutumia liking'amuzi lao
 
Vizuri ni gharama jamani

Hawana uzuri unaopita TV nyingine zinazochaji gharama ndogo kuliko yao mara kumi. Kinachowapa jeuri DSTV ni fedha za serikali, mashirika ya umma na ya kumataifa yaliyopo Tanzania. Kuna idara na mashirika mengi sana yanayowalipiwa wafanyakazi wao hivyo kwa vile hizi fedha hazina uchungu kwa wanaolipa ndio maana wanapandisha kila wakijisikia. Kwa kifupi fedha ya umma ndio inawapa jeuri.
 
Dstv...basi nisicomment chochote ile sheria ya mitandao isije kunikaba koo. Mwezi wa kumi naihama.
 
Siku Azam akipata haki ya kuonyesha EPL, DSTv waanze kuaga Tanzania.
 
Kuwa matawi si mchezo , ndio maana makaka poa wanaongezeka huko bongo kutaka ku maintain trend.
 
Mimi ni mpenzi mkubwa wa mpira wa miguu hasa ligi mbali mbali duniani.

Nilikuwa nalipia Dstv Premium 139,000 wakapandisha mpaka 199,000 na sasa hivi wamenitumia ujumbe kuwa kuanzia kesho yaani Octoba 1 itakuwa 219,000 Nimekata tamaa kabisa kwani hiyo bei ni kubwa sana.

Nimeiangalia hiyo bei nikaona mpangaji wangu analipa 30,000 kwa mwezi hivyo kwa bei hiyo atalipa kodi ya miezi 6 yaani 180,000 na atabaki na chenji ya umeme 39,000.

Uchunguzi wangu umegundua kuwa wengi wameacha kulipia kifurushi cha juu na kile cha kati kwasababu hata ukitoza kwa watazamaji wengine hutapata hiyo hela ya kulipia.

Wenyewe wanajitahidi kupiga simu kukumbushia malipo lakini ukweli wengi wetu tutakwama labda wafikirie upya bei zao. Sasa hapa Azam ndio wangechangamka mapema ili tuachane na hawa Multichoice

Uko Lumumba au Mabadiliko?
 
Kile cha pass wamekifikisha sh ngapi maana tulizoea tsh 22,000/= ila itabidi tusepe maana hawasikii
 
shkamoo str 4922, shkamoo Champion TV, Shkamoo PTV , Shkamoo POWER VU , Shkamoo anko QSAT Q28 , Shkamoo BISS KEYS , Shkamoo FTA, Shkamoo Dish Ft 6,Shkamoo Mchina...


Mtoa Mada unahitaji Mabadiliko!
 
Hahahahhhhaàaa kumbe tuko wengii ee. Yaan Nilipiga mahesabu kodi ya nyumba ninayolipa inazidiwa na king'amuzi. Nikasema yatosha. Kwa kuwa mi mpenzi wa La Liga nimenunua Azam. Naangalia La liga kiroho safi. EPL naenda Bar nanunua soda yangu 1000. Naangalia game. Mwaka huu watafika 300,000.
 
Leo cku ya 3 mfululizo napigiwa sim na wafanyakaz tofauti kwa nn sijalipia na kila anayepiga namchana clear kua gharama zimepanda sana!!
hao ndyo wakongwe wa digital acha wapandishe....
 
Eboooh! Hivi bado mnalipia dstv?mie dish lao nilimuuzia mama ntilie anakaaNgia samaki!
 
Back
Top Bottom