Jamani mimi ni mpweke sana

Jamani mimi ni mpweke sana

INSPECTOR JOE

Member
Joined
Apr 14, 2014
Posts
26
Reaction score
12
Wapendwa mimi sina hata wa kunifariji,yote hii kisa nimeachika.Nilikuwa na mpenzi wangu tuliokuwa tunapenda sana ila aliamua kuniacha bila kuniambia sababu, sasa mimi nimebaki mpweke.

Please naombeni ushauri wenu
 
Njoo hapa Que Pasa.......Karen..... mara moja.......panahappen mbaya kabisa.......tudiscuss hii issue yako........
 
...bwana mdogo unaonekana upo desperate sana...kila uzi unaoanzisha ni ishu za upweke
 
Duniani hakuna upweke sisi wenyewe ndio tunajijengea mazingira ya upweke kwa kujenga ukuta wa chuki baina yetu na wale wanaotamani kuzifaidi busara zetu....fungua milango ya upendo na uuvunje mlango wa visasi na watu wema ,wenye upendo wa dhati kwenye maisha yako watakuja wenyewe....na watakufanya uyafurahie maisha...huku kila siku wakikupa sababu ya kutabasamu......
 
Ukubwani ndo unazidi hasa ukiwa huonekani

Unajua huyu sio mpweke bali anapitia kile kipindi kigumu cha kupigwa kibuti, na kwa tafsiri ya wengi huo ndio upweke! Kumkosa mwandani mtima wa roho ambaye mnaweza kukaa pekeyenu mkanong'onezana ya moyoni, yale yalifichika kwenye uvungu wa mioyo
Lakini kuna upweke wa mawazo, upweke wa uchumi upweke wa kazi,upweke wa imani yani huna kitu unachojinasibu nacho
 
Unajua huyu sio mpweke bali anapitia kile kipindi kigumu cha kupigwa kibuti, na kwa tafsiri ya wengi huo ndio upweke! Kumkosa mwandani mtima wa roho ambaye mnaweza kukaa pekeyenu mkanong'onezana ya moyoni, yale yalifichika kwenye uvungu wa mioyo
Lakini kuna upweke wa mawazo, upweke wa uchumi upweke wa kazi,upweke wa imani yani huna kitu unachojinasibu nacho
hapo nimekusoma
 
Pole sana kuna mdau hapo juu kaeleza vizuri tu upweke wa ainagani pengine unao, ni dhahiri mtu anapokua mpweke amekosa tu mtu wakumpenda wa jamii ya kike au ya kiume hivyo wewe jipe moyo tu kwani ni hsli iliopo na inapita,usiumie sana japo unamia lakini jua ni leo na kesho tu utarudi katika hali ya kawaida. Pole lakini.
 
Wapendwa mimi sina hata wa kunifariji,yote hii kisa nimeachika.Nilikuwa na mpenzi wangu tuliokuwa tunapenda sana ila aliamua kuniacha bila kuniambia sababu, sasa mimi nimebaki mpweke.

Please naombeni ushauri wenu

nipe no yako ya simu nikuondoe upweke kwa kuchat kwa sms
 
kuwa single boy kama mimi demu hakuchanganyi kichwa akileta upuuzi unabadilisha faili...
hutakuwa mpweke kaka....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom