goodhearted
JF-Expert Member
- Feb 15, 2015
- 1,021
- 1,268
Hizi mada za ualimu zimenigusa sana. ok mimi pia ni mwalimu katika halmashauli fulani. Mambo yanayonipata inafikia hatua natamani niachane tu na hii kazi
Ni hivi, baada ya kumaliza kujaza mikataba nilipostiwa kuanza kazi katika shule flani ya kata. Tulichokikuta huko sijawahi kukiona katika shule yoyote.
Aisee kwanza shule ilikuwa na walimu 7 tu ila maajabu mkuu wa shule ndo kila kitu, yeye ndo mtaaluma, mwl wa chakula na mengineyo mengi. Hakuna cha school balaza wala nini. Kwenye vikao yeye ndo msemaji mkuu na hakuna kupingwa.
Tumefight sana kuadjust lakini mwisho wa siku aligawa madaraka japo kwa shida sana lakini anapokupatia unakuwa huna full mandate na kitengo chako utafuatilia mpaka uone kero. Mfano mwl wa taaluma hana uwezo hata wa kwenda kuchapa mitihani yeye kazi yake ni kuandaa ratiba tu.
Mbaya zaidi amekaa muda mrefu kwa hiyo amewaaminisha wanafunzi na wazazi kuwa shule ni yake na hakuna mtu wa kumhamisha hivyo wanafunzi wanamheshimu yeye pekee, wanadharau walimu wengine utafikiri wanafunzi wenzao tu na ukiwaadhibu kama yeye hayupo basi akirudi watakusemea kwake na asivyo na busara utaitwa mbele yake kuhojiwa.
Hayo ni machache tu lakini kisa kikubwa kilicho nifanya niandike uzi huu ni hiki,,
Baada ya msuguano wa hayo yote walimu wote tulikubaliana kumwomba afisa elimu kuwa atuhamishie huyu mkuu ikiwezekana watuletee mwingine
Kwa shinikizo kubwa afisa elimu alituma "tume yake" kuja kuchunguza tulichokuwa tukipinga. Ilivyo ondoka tuliambiwa tutapewa feedback.
Cha ajabu ni kuwa siku ya kufunga mimi sikuwepo nilikuwa na matatizo hivyo nilikuwa na ruhusa. Habari waliyopewa ni kuwa mimi nimehamishwa kituo cha kazi na wengine watafuata. Na sitalipwa usumbufu wa aina yoyote ile kwa kuwa ni matatizo tumejitafutia sisi. Kwa hiyo gharama ya kusafirisha mizigo yangu itakuwa juu yangu, Mbaya zaidi aliwazuia walimu wezangu wasinipe taarifa hizi, japo kuna huyo mmoja kanipenyezia.
Yeye kama mkuu hajaniambia chochote hivyo ni kama chini ya kapeti.
Samahani kwa uzi mrefu wakuu, ila hapo nimejitahidi kufupisha na naombeni mchango wenu ,hivi ni kweli unaweza kuhamishwa kwa jeuri namna hiyo alafu ujigharamikie kwa uhamisho ambao hujauomba?? Kweli jamani??
Kama ni kweli nafikiria kuchukua maamuzi magumu...najua kitaa maisha ni magumu sana lakini.... HUU NI ZAIDI YA UONEVU
MAWAZO YENU TAFADHALI.
Ni hivi, baada ya kumaliza kujaza mikataba nilipostiwa kuanza kazi katika shule flani ya kata. Tulichokikuta huko sijawahi kukiona katika shule yoyote.
Aisee kwanza shule ilikuwa na walimu 7 tu ila maajabu mkuu wa shule ndo kila kitu, yeye ndo mtaaluma, mwl wa chakula na mengineyo mengi. Hakuna cha school balaza wala nini. Kwenye vikao yeye ndo msemaji mkuu na hakuna kupingwa.
Tumefight sana kuadjust lakini mwisho wa siku aligawa madaraka japo kwa shida sana lakini anapokupatia unakuwa huna full mandate na kitengo chako utafuatilia mpaka uone kero. Mfano mwl wa taaluma hana uwezo hata wa kwenda kuchapa mitihani yeye kazi yake ni kuandaa ratiba tu.
Mbaya zaidi amekaa muda mrefu kwa hiyo amewaaminisha wanafunzi na wazazi kuwa shule ni yake na hakuna mtu wa kumhamisha hivyo wanafunzi wanamheshimu yeye pekee, wanadharau walimu wengine utafikiri wanafunzi wenzao tu na ukiwaadhibu kama yeye hayupo basi akirudi watakusemea kwake na asivyo na busara utaitwa mbele yake kuhojiwa.
Hayo ni machache tu lakini kisa kikubwa kilicho nifanya niandike uzi huu ni hiki,,
Baada ya msuguano wa hayo yote walimu wote tulikubaliana kumwomba afisa elimu kuwa atuhamishie huyu mkuu ikiwezekana watuletee mwingine
Kwa shinikizo kubwa afisa elimu alituma "tume yake" kuja kuchunguza tulichokuwa tukipinga. Ilivyo ondoka tuliambiwa tutapewa feedback.
Cha ajabu ni kuwa siku ya kufunga mimi sikuwepo nilikuwa na matatizo hivyo nilikuwa na ruhusa. Habari waliyopewa ni kuwa mimi nimehamishwa kituo cha kazi na wengine watafuata. Na sitalipwa usumbufu wa aina yoyote ile kwa kuwa ni matatizo tumejitafutia sisi. Kwa hiyo gharama ya kusafirisha mizigo yangu itakuwa juu yangu, Mbaya zaidi aliwazuia walimu wezangu wasinipe taarifa hizi, japo kuna huyo mmoja kanipenyezia.
Yeye kama mkuu hajaniambia chochote hivyo ni kama chini ya kapeti.
Samahani kwa uzi mrefu wakuu, ila hapo nimejitahidi kufupisha na naombeni mchango wenu ,hivi ni kweli unaweza kuhamishwa kwa jeuri namna hiyo alafu ujigharamikie kwa uhamisho ambao hujauomba?? Kweli jamani??
Kama ni kweli nafikiria kuchukua maamuzi magumu...najua kitaa maisha ni magumu sana lakini.... HUU NI ZAIDI YA UONEVU
MAWAZO YENU TAFADHALI.