Jamani bei hizi za mafuta

kimbendengu

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2013
Posts
7,759
Reaction score
14,474
Rais wa Tanzania ,Waziri wa chakula,hizi bei za bidhaa hizi mnaziona ?Bei ya ngano mumeiona?Bei za nondo mumeziona ? Je kama mlipigiwa kura na watanzania mnaona haya maisha kwa raia wenu ni sawa ?Mnampango gani nahali ya mfumuko wa bei za bidhaa ambazo huku mtaani ni balaaaaaa.
 
Wap ulipigaa kuraa hawamu hii ya ctaa mkuu wngu,
 
Hawawezi kuongea kitu wao ndio wamiliki wa sheli
Wao ndio wamiliki wa baadhi ya viwanda
Wao ndio wamiliki wa baadhi mazao yanayolimwa kama kina msukuma hapo wanafurahi wanapiga hela maana kipindi kile walikuwa wanabanwa
Kkoo pale maduka yao yamejaa we unadhani wataongea nn.

Yaani hapo mwanasiasa anatakiwa akae mbali na biashara ila akiwa muhusika mkuu haya ndo madhara yake.
 
Sheli=Total=Puma,
Nilitaka kumaanisha kuanzia sasa unapaswa kujua neno sheli unalitumia visivyo,kiswahili fasaha ni kituo cha mafuta,sheli ni kampuni kubwa ya mafuta kama vile unavyoona Total ama puma.
Kwa faida ya wote mnaotumia hili hili jina vibaya,
Thnx
 
Lugha hukua kwa sasa pamoja na watu kuelezwa kuwa sheli ni kampuni la mafuta bado watu wameendelea kulitumia. Itabidi lifanywe kuwa jina rasmi.
 
Lugha hukua kwa sasa pamoja na watu kuelezwa kuwa sheli ni kampuni la mafuta bado watu wameendelea kulitumia. Itabidi lifanywe kuwa jina rasmi.
Kila mtu ukisema sheli anakuelewa una maana gani, nyongeza mkuu.
 
Namkumbuka Hashim Rungwe. Sahv tungekuwa foleni ya ubwabwa tu bila kuumia na bei ya mafuta ya kupikia😃
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…