Ni tofauti kabisa kama anga na bahari. Sema tu chuki na hasira yako kwa Magufuli inakufanya utafute kila sababu umchague Rais. Wewe tulia na uzoee. Magufuli ni Rais wetu mpaka 2025!Hii haina tofauti na maamuzi ya Magu kuukataa sasa mradi wa Bagamoyo wakati alipokuwa waziri hakuupinga na kama aliupinga kwenye baraza la mawaziri lakini hakujiuzulu bali aliunga mkono maamuzi ya wenzake kwahiyo hana tofauti na Jaji huyu mstaafu.
Kuna mambo usiyoyajua au umeamua kuwa mtetezi wa dhuluma.Siyo suala la kutaka ni suala la italiana. Ukiwaondoa na kuwaweka wasiokuwa wanachama wa chama chochote unajuaje unaowaweka hawana mapenzi au ushabiki wa chama chochote?
Tofauti yao inamsaidia nini bibi yangu aliyeko kijijini?Kuna tofauti kubwa sana kati ya Mzee Mwanakijiji before 2015 VS Mzee Mwanakijiji after November 2015.
Hawa ni watu wawili tofauti kiakili na pengine kimwili.
Ukijadili mada yeyote toka jina hilo basi sema RIP kwa huyo before 2015
Baadhi ya binadamu wenzetu wameanza kurejea kwenye usokwemtu
Puppet on a string...
Na. M. M. Mwanakijiji
Wakati mwingine unaweza kujisikia kizunguzungu ukiwasikiliza viongozi wetu ambao sasa wanaonekana “wanajua”. Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani amenukuliwa na gazeti moja akionesha kuunga mkono uamuzi wa Mahakama Kuu kutangaza kuwa mfumo unaowaweka viongozi au wanachama wa chama tawala kama wasimamizi wa uchaguzi ni kinyume na Katiba. Amedai kuwa tangu 1995 (akiwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi) walitoa mapendekezo ya kuondoa utaratibu huo. Lakini kwa miaka ishirini hilo halijatokea hadi hivi sasa.
Jambo ambalo linanitibua mimi zaidi ni kuwa Jaji huyu huyu ambaye anadai kuwa wana viongozi na mashabiki wa vyama vya siasa wasijiwekwe kusimamia uchaguzi alijitokeza 2015 akiwa amevaa magwanda ya CCM akitaka kugombea Urais chini ya mfumo ule ule ambao anadai wao hawakuupenda! Mfumo ambao anataka tuamini kuwa aliona hautakuwa wa haki (fair) kwa vyama vingine?
Sasa Jaji Ramadhani tafadhali bwana; hivi kama kweli ulijua kuwa mfumo huu ni mbaya kilichokufanya usimame na kutaka kugombea Urais kwa tiketi ya CCM ilikuwa ni nini? Unataka tuamini kuwa mapenzi yako kwa CCM yalikuja baada ya kuwa umeondoka Ujaji Mkuu? Je, haiwezekani kuwa kumbe mwenzetu tangu miaka “ile ya nineteen kweusi” ulikuwa ni mwanachama na shabiki wa CCM? Kwamba ulipokuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ulikuwa tayari na “mahaba” na chama tawala?
Kama hili ni kweli basi kuna mambo mawili; kwamba, unaamini kuwa kwa wewe kuwa na mapenzi au uanachama wa Chama cha Mapinduzi hakukufanya uvunje uadilifu wako wa kusimamia taratibu au sheria bila kujali mgombea anatoka chama gani. Kwamba, kama Augustino Mrema angeshinda mwaka 1995 wewe na wenzako mlikuwa tayari kumtangaza mshindi hata kama CCM ingeondoka madarakani? Je hili ni kweli?
Kama hili ni kweli unataka tuamini kuwa mwanachama wa chama cha siasa akisimamia na kuzingatia viapo vyake, maadili ya kazi, sheria na haki anaweza kusimamia uchaguzi bila kupendelea chama chake. Kwamba, ndio maana wapo wabunge wa vyama vya upinzani ambao wameshinda na kurudia kushinda kwenye majimbo yao licha ya wasimamizi wa majimbo hayo kuwa ama ni wanachama wa chama tawala au mashabiki wa chama hicho.
Jambo la pili ni kuwa kama hilo la kwanza si kweli basi ni wazi kuwa hukuwa mwadilifu na kuwa ulikuwa unafanya kazi kwa upendeleo ukiongozwa na mahaba kwa chama chako. Kwamba, kwa vile tunajua sasa kuwa wewe ulikuwa ni mwana CCM ulikuwa unafanya kazi kwa kificho kumbe moyoni ulikuwa na chama unachokipendelea kishinde.
Kama hili la pili ni kweli basi hoja yako ya kuwaondoa mashabiki na wanachama (walijionesha wazi) wa CCM kwenye kusimamia uchaguzi ni jambo la msingi, la lazima na ambalo haliepukiki. Hii ina maana kuwa siyo wana CCM tu bali Watanzania wote wanapaswa kushuku kila wakati na mara zote unapofanyika uchaguzi pale ambapo wasimamizi wa uchaguzi bado ni wana CCM. Kwamba, WAtanznaia na hasa wapinzani wasidhanie hata kwa mbali kuwa wakurugenzi hawa wa uchaguzi wanaweza kutenda haki.
Nikiangalia yote mawili naamini tatizo letu kubwa haliko kwenye uanachama wa wakurugenzi wa uchaguzi au watendaji wengine. Hii ni kwa sababu huwezi kuondoa mapenzi ya mtu kwa chama Fulani hata kama mtu huyo hatovaa gwanda hilo wakati akiwa kazini. Tatizo letu ni kutokuwa na mfumo ambao uko wazi, unaoneshimika na kila mtu na ambao kila mtu anaweza kuuamini kumtendea haki. Inapotokea kwamba wapinzani wanalazimika “kulinda kura” kwa kuhofia kuibiwa ni wazi kuwa mfumo hauko sawa na hauaminiki.
Badala ya kuhangaika na “uanachama” wa Wakurugenzi wa Uchaguzi naomba kupendekeza kwa heshima na taadhima tuangalia uadilifu wa watendaji – ikiwemo kuweka adhabu kubwa kwa mkurugenzi ambaye anaonekana kuharibu uchaguzi kwa sababu za kisiasa. Ni lazima tuangalie mfumo wa uchaguzi kuhakikisha kuwa wapinzani wanapata haki ile ile wanayopewa CCM. Haiwezekani wapinzani wanalazimika kutumia nguvu kubwa kweli hata kurudisha fomu za kugombea wakati CCM inaonekana wana mlango wao mwingine maalum.
Nitatoa mfano, Rais Magufuli alipozungumza (labda kwa utani au akimaanisha) kuwa yeye anateua wakurugenzi wa halmashauri halafu ati waje kumtangaza mgombea wa upinzani kashinda. Tulitarajia Tume ya Uchaguzi ingesimama na kutetea nafasi yake na kuwataka watendaji wake kutekekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na siyo matakwa ya siasa. Kama Rais Magufuli atawafukuza kazi wakurugenzi wa halmashauri kwa sababu wamemtangaza mpinzani hii ni haki na wajibu wake.
Ndio maana niliposoma habari ya kauli yako hii nimebakia kusema “Jaji Ramadhani, tafadhali bwana!”
Niandikie:mwanakijiji@jamiiforums.com
Umelenga patamu sana,sijui atakujibu nini hapo!!!!Hii haina tofauti na maamuzi ya Magu kuukataa sasa mradi wa Bagamoyo wakati alipokuwa waziri hakuupinga na kama aliupinga kwenye baraza la mawaziri lakini hakujiuzulu bali aliunga mkono maamuzi ya wenzake kwahiyo hana tofauti na Jaji huyu mstaafu.
Tujadili hoja yake.Unajua ndugu hawa wazee wetu umri umekwenda,wanatakiwa kua makini sana katika kauli zao,muda mwingine unakwepa kwanza kuongea ili utafakari.
Wanasahau watanzania ni makini sana kufuatilia nyendo zao
Kuna siku huyu pamoja na majaji wastaafu wenzake walialikwa ikulu kuongea na Mh Rais.
Na. M. M. Mwanakijiji
Wakati mwingine unaweza kujisikia kizunguzungu ukiwasikiliza viongozi wetu ambao sasa wanaonekana “wanajua”. Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani amenukuliwa na gazeti moja akionesha kuunga mkono uamuzi wa Mahakama Kuu kutangaza kuwa mfumo unaowaweka viongozi au wanachama wa chama tawala kama wasimamizi wa uchaguzi ni kinyume na Katiba. Amedai kuwa tangu 1995 (akiwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi) walitoa mapendekezo ya kuondoa utaratibu huo. Lakini kwa miaka ishirini hilo halijatokea hadi hivi sasa.
Jambo ambalo linanitibua mimi zaidi ni kuwa Jaji huyu huyu ambaye anadai kuwa wana viongozi na mashabiki wa vyama vya siasa wasijiwekwe kusimamia uchaguzi alijitokeza 2015 akiwa amevaa magwanda ya CCM akitaka kugombea Urais chini ya mfumo ule ule ambao anadai wao hawakuupenda! Mfumo ambao anataka tuamini kuwa aliona hautakuwa wa haki (fair) kwa vyama vingine?
Sasa Jaji Ramadhani tafadhali bwana; hivi kama kweli ulijua kuwa mfumo huu ni mbaya kilichokufanya usimame na kutaka kugombea Urais kwa tiketi ya CCM ilikuwa ni nini? Unataka tuamini kuwa mapenzi yako kwa CCM yalikuja baada ya kuwa umeondoka Ujaji Mkuu? Je, haiwezekani kuwa kumbe mwenzetu tangu miaka “ile ya nineteen kweusi” ulikuwa ni mwanachama na shabiki wa CCM? Kwamba ulipokuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ulikuwa tayari na “mahaba” na chama tawala?
Kama hili ni kweli basi kuna mambo mawili; kwamba, unaamini kuwa kwa wewe kuwa na mapenzi au uanachama wa Chama cha Mapinduzi hakukufanya uvunje uadilifu wako wa kusimamia taratibu au sheria bila kujali mgombea anatoka chama gani. Kwamba, kama Augustino Mrema angeshinda mwaka 1995 wewe na wenzako mlikuwa tayari kumtangaza mshindi hata kama CCM ingeondoka madarakani? Je hili ni kweli?
Kama hili ni kweli unataka tuamini kuwa mwanachama wa chama cha siasa akisimamia na kuzingatia viapo vyake, maadili ya kazi, sheria na haki anaweza kusimamia uchaguzi bila kupendelea chama chake. Kwamba, ndio maana wapo wabunge wa vyama vya upinzani ambao wameshinda na kurudia kushinda kwenye majimbo yao licha ya wasimamizi wa majimbo hayo kuwa ama ni wanachama wa chama tawala au mashabiki wa chama hicho.
Jambo la pili ni kuwa kama hilo la kwanza si kweli basi ni wazi kuwa hukuwa mwadilifu na kuwa ulikuwa unafanya kazi kwa upendeleo ukiongozwa na mahaba kwa chama chako. Kwamba, kwa vile tunajua sasa kuwa wewe ulikuwa ni mwana CCM ulikuwa unafanya kazi kwa kificho kumbe moyoni ulikuwa na chama unachokipendelea kishinde.
Kama hili la pili ni kweli basi hoja yako ya kuwaondoa mashabiki na wanachama (walijionesha wazi) wa CCM kwenye kusimamia uchaguzi ni jambo la msingi, la lazima na ambalo haliepukiki. Hii ina maana kuwa siyo wana CCM tu bali Watanzania wote wanapaswa kushuku kila wakati na mara zote unapofanyika uchaguzi pale ambapo wasimamizi wa uchaguzi bado ni wana CCM. Kwamba, WAtanznaia na hasa wapinzani wasidhanie hata kwa mbali kuwa wakurugenzi hawa wa uchaguzi wanaweza kutenda haki.
Nikiangalia yote mawili naamini tatizo letu kubwa haliko kwenye uanachama wa wakurugenzi wa uchaguzi au watendaji wengine. Hii ni kwa sababu huwezi kuondoa mapenzi ya mtu kwa chama Fulani hata kama mtu huyo hatovaa gwanda hilo wakati akiwa kazini. Tatizo letu ni kutokuwa na mfumo ambao uko wazi, unaoneshimika na kila mtu na ambao kila mtu anaweza kuuamini kumtendea haki. Inapotokea kwamba wapinzani wanalazimika “kulinda kura” kwa kuhofia kuibiwa ni wazi kuwa mfumo hauko sawa na hauaminiki.
Badala ya kuhangaika na “uanachama” wa Wakurugenzi wa Uchaguzi naomba kupendekeza kwa heshima na taadhima tuangalia uadilifu wa watendaji – ikiwemo kuweka adhabu kubwa kwa mkurugenzi ambaye anaonekana kuharibu uchaguzi kwa sababu za kisiasa. Ni lazima tuangalie mfumo wa uchaguzi kuhakikisha kuwa wapinzani wanapata haki ile ile wanayopewa CCM. Haiwezekani wapinzani wanalazimika kutumia nguvu kubwa kweli hata kurudisha fomu za kugombea wakati CCM inaonekana wana mlango wao mwingine maalum.
Nitatoa mfano, Rais Magufuli alipozungumza (labda kwa utani au akimaanisha) kuwa yeye anateua wakurugenzi wa halmashauri halafu ati waje kumtangaza mgombea wa upinzani kashinda. Tulitarajia Tume ya Uchaguzi ingesimama na kutetea nafasi yake na kuwataka watendaji wake kutekekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na siyo matakwa ya siasa. Kama Rais Magufuli atawafukuza kazi wakurugenzi wa halmashauri kwa sababu wamemtangaza mpinzani hii ni haki na wajibu wake.
Ndio maana niliposoma habari ya kauli yako hii nimebakia kusema “Jaji Ramadhani, tafadhali bwana!”
Niandikie:mwanakijiji@jamiiforums.com
Inabidi nami nikubaliane na dhana hii. Katika mkondo ule ule uliompata Dr Mhogo, huyu naye alichukua kitu; akauza utu wake.Kishatafuna pesa za watu huyo kwa hiyo lazima zimtokee tundu lolote lile. Ndiyo sababu anakuja hapa kuandika upuuzi wake ili kumfurahisha master wake. Ukiwa na tamaa ya pesa za haraka haraka matokeo yake ndiyo kama haya. Unapoteza reputation na credibility.
Wataangaliwa historia yao. Mfano sio wanachama wa chama chochote for the past five years. Hii isimamiwe na sheria na mtu anaapa, kinyume chake anaadhibiwa vikali. Tuko mil 50+, kupata watu 200 wasimamizi wa uchaguzi ambao ushahidi unaonyesha sio wanachama yawezekana.Siyo suala la kutaka ni suala la italiana. Ukiwaondoa na kuwaweka wasiokuwa wanachama wa chama chochote unajuaje unaowaweka hawana mapenzi au ushabiki wa chama chochote?
MUNGU WA MBINGUNI ANAYAONA HAYATatizo kubwa lipo kwa anayewateua wakurugenzi. Kwa sasa, mkurugenzi akiamua kutenda haki, na haki hiyo ikampa ushindi mpinzani, mkurugenzi huyo ajue hana kazi. Tuna kiongozi ambaye anafurahia unyang'anyi wa haki za raia japo kwa unafiki anatuhadaa kuwa anapenda haki.
...... matatizo yenyewe ndiyo hayo; sizitaki mbichi hiziJambo ambalo linanitibua mimi zaidi ni kuwa Jaji huyu huyu ambaye anadai kuwa wana viongozi na mashabiki wa vyama vya siasa wasijiwekwe kusimamia uchaguzi alijitokeza 2015 akiwa amevaa magwanda ya CCM akitaka kugombea Urais chini ya mfumo ule ule ambao anadai wao hawakuupenda! Mfumo ambao anataka tuamini kuwa aliona hautakuwa wa haki (fair) kwa vyama vingine?
Sasa Jaji Ramadhani tafadhali bwana; hivi kama kweli ulijua kuwa mfumo huu ni mbaya kilichokufanya usimame na kutaka kugombea Urais kwa tiketi ya CCM ilikuwa ni nini? Unataka tuamini kuwa mapenzi yako kwa CCM yalikuja baada ya kuwa umeondoka Ujaji Mkuu? Je, haiwezekani kuwa kumbe mwenzetu tangu miaka “ile ya nineteen kweusi” ulikuwa ni mwanachama na shabiki wa CCM? Kwamba ulipokuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ulikuwa tayari na “mahaba” na chama tawala?
Kama hili ni kweli basi kuna mambo mawili; kwamba, unaamini kuwa kwa wewe kuwa na mapenzi au uanachama wa Chama cha Mapinduzi hakukufanya uvunje uadilifu wako wa kusimamia taratibu au sheria bila kujali mgombea anatoka chama gani. Kwamba, kama Augustino Mrema angeshinda mwaka 1995 wewe na wenzako mlikuwa tayari kumtangaza mshindi hata kama CCM ingeondoka madarakani? Je hili ni kweli?
Ukabila na udini vinamsumbua sanaPuppet under the instructions of the puppet master.