Jaji Ramadhani tafadhali bwana! Ama unasema kweli au la...

Hii haina tofauti na maamuzi ya Magu kuukataa sasa mradi wa Bagamoyo wakati alipokuwa waziri hakuupinga na kama aliupinga kwenye baraza la mawaziri lakini hakujiuzulu bali aliunga mkono maamuzi ya wenzake kwahiyo hana tofauti na Jaji huyu mstaafu.
Ni tofauti kabisa kama anga na bahari. Sema tu chuki na hasira yako kwa Magufuli inakufanya utafute kila sababu umchague Rais. Wewe tulia na uzoee. Magufuli ni Rais wetu mpaka 2025!
 
Siyo suala la kutaka ni suala la italiana. Ukiwaondoa na kuwaweka wasiokuwa wanachama wa chama chochote unajuaje unaowaweka hawana mapenzi au ushabiki wa chama chochote?
Kuna mambo usiyoyajua au umeamua kuwa mtetezi wa dhuluma.

Hapo zamani, upendeleo kwa CCM na maagizo ya kuwanyang'anya ushindi vyama vya upinzani, ilifanyika kwa siri lakini kwa awamu hii upendeleo unafanyika kwa uwazi kwa maagizo ya kiongozi wetu, tena kwa vitisho na kwa kukiuka sheria na katiba.

Kuna wakati kiongozi wetu aliwatangazia wateule kwa nafasi ya ukurugenzi wa Halmashauri, akisema, 'safari hii nimewateua wakurugenzi wengi makada wa chama ili wakasimamie ilani ya chama'. Anaongea hayo kwa uwazi huku akijua kabisa kuwa nafasi ya ukurugenzi imeelezwa wazi kwenye miongozo ya Utumishi wa umma, ni nani mwenye sifa ya kuwepo kwenye nafaai hiyo. Yeye anawateua watu toka ofisi za Lumumba, watu ambao hawajawahi kuwa watumishi wa umma, wakati nafasi hiyo kwa kadiri ya mwongozo wa utumishi wa umma inastahili kushikwa na mteule toka kwenye kundi la wafanyakazi wa umma waliofikia ngazi fulani tu.

Pili, usichokijua MMK ni kuwa tatizo kubwa ni kiongozi wetu, mbaye anateua wakurugenzi kwa kuwapa maelekezo kuwa wakapokonye haki za wananchi wakati wa uchaguzi.

Tatizo kubwa lipo kwa anayewateua wakurugenzi. Kwa sasa, mkurugenzi akiamua kutenda haki, na haki hiyo ikampa ushindi mpinzani, mkurugenzi huyo ajue hana kazi. Tuna kiongozi ambaye anafurahia unyang'anyi wa haki za raia japo kwa unafiki anatuhadaa kuwa anapenda haki.

Huku tukipiga hatua taratibu, tuendelee kumwomba Mungu azidi kuwadhalilisha na kuwaonesha kweli yake, wale wapokonya haki na mawakala wao. Taratibu tunapiga hatua, na kuna siku mavazi na picha zao wasiotenda haki, zitawekwa kwenye makumbusho kama kumbukumbu mbaya watu waliojitahidi sana kudhulumu haki za Raia.
 
Mh Jaji yuko sahihi. Unapogundua kosa, haijalishi umelifanya kwa masaa, siku, wiki, miezi au miaka mingapi! Nafasi ya kujisahihisha ikipatikana fanya hivyo. Kwa wkt huo huwezi jua ni mazingira gani yalimkumba akashindwa. Kuna mambo huwezi badilisha kwenye mfumo kama huna '' money power, people's power (influence) au political power ''
 
Puppet on a string...

Kwikwikwikwiii
 
Hii haina tofauti na maamuzi ya Magu kuukataa sasa mradi wa Bagamoyo wakati alipokuwa waziri hakuupinga na kama aliupinga kwenye baraza la mawaziri lakini hakujiuzulu bali aliunga mkono maamuzi ya wenzake kwahiyo hana tofauti na Jaji huyu mstaafu.
Umelenga patamu sana,sijui atakujibu nini hapo!!!!
 
Unajua ndugu hawa wazee wetu umri umekwenda,wanatakiwa kua makini sana katika kauli zao,muda mwingine unakwepa kwanza kuongea ili utafakari.

Wanasahau watanzania ni makini sana kufuatilia nyendo zao
Tujadili hoja yake.
 
Haki au Kweli haina rangi, taifa, kabila, jamii, jinsia, chama cha siasa au kundi lolote lenye mshikamano fulani.
 
Nisomapo mabandiko marefu hivi, ambayo mwanzo wake tu yananionyesha kuyapinga huwa napata taabu sana kutuliza akili yangu isiyumbe na kuwa na uvumilivu wa kusoma hadi mwisho wa maandiko.

Kwa bahati nzuri nimevuta subira kweli mpaka nilipofikia sehemu niliyokubaliana na mleta mada; hasa kwenye 'mapendekezo' ya kuweka utaratibu mzuri wa kuhakikisha wasimamizi wanatenda haki kila mara wanaposimamia uchaguzi. Na kwamba adhabu kali itolewe kwa yeyote anayebainika kupindisha matakwa ya wapiga kura.

Sasa huo utani? wa kuwaamuru watu unaowateua! Huo uwe utani!

Hapa ndipo dharau ya watu tuliowaheshimu sana kwa misimamo ilipoanzia, haijulikani ni kitu gani kilichoingia ndani ya ubongo wao na kuukoroga kama uji.

Unapokuwa shabiki au mwanachama wa chama, halafu uwe refa wa kusimamia haki kati ya mwanachama mwenzako na mpinzani, hili halileti maana yoyote, hasa katika mazingira haya tuliyonayo sasa.

Tunazungumzia chama kilichopo kwenye madaraka, na mara baada ya uchaguzi huo, hata hao mashabiki na wanachama waliosimamia uchaguzi wanategemea teuzi za juu zaidi ili waendelee kuneemeka! Kwa nini hili watu (hasa hao walioko CCM na wanaofaidika na chama kama hicho wanaung'ang'ania... sababu ni hiyo hiyo moja, kwa sababu wanafaidika na mpango huo.

Sasa tunaona baadhi ya watu, hata kama hawashabikii chama, lakini wanashabikia mtu, hadi kumwona matamshi yake ya utata kuwa ni utani?

Nadhani mwisho nimalizie tu kwa kusema hili moja. Kama huko CCM kweli bado kuna watu wanaoamini kwa dhati ya mioyo yao kwamba kuna chama kinachosimamia hatma ya taifa hili; hao watu ni wa kuwahesabu, na huenda hata vidole vya mikono miwili huvimalizi. CCM ni ya wapigaji; ni ya maslahi. Hata hao akina Augustino ni maslahi zaidi ndiyo waliyoyaweka mbele.
Kwa hiyo kama hawakutokea kupinga anayoyahoji mwandishi, asijifanye hilo halijui.

Kati ya hao wachache waliobaki huko ni akina Mzee Sinde Warioba, ambaye naye imemlazimu sasa anyamaze na kubaki kuwa mtazamaji na kuogopa kutia mchanga kwenye kitumbua cha kijana. Hayo ndio maadili yaliyobaki huko CCM.

Na Tanzania ya watu zaidi ya milioni hamsini, Tume iliyo huru kweli itashindwa kabisa kuwapata watu wachache tu wa kusimamia uchaguzi mpaka ilazimu wawe makada wa chama waliojitambulisha?
 
Kuna siku huyu pamoja na majaji wastaafu wenzake walialikwa ikulu kuongea na Mh Rais.
JPM aliwapa nafasi ya kumshauri kuhusu jambo lolote.
Mbona hakusema lolote kuhusu wakurugenzi kusimamia Uchaguzi Mkuu na chaguzi nyingine?
 
Inabidi nami nikubaliane na dhana hii. Katika mkondo ule ule uliompata Dr Mhogo, huyu naye alichukua kitu; akauza utu wake.

Inashangaza sana, hasa katika yale aliyokuwa akiyaelezea kuhusu Mwalimu Nyerere na misimamo aliyokuwa nayo, ya kutetea alicho kiamini bila ya kuteteleka. Hasa inapohusu haki za wanyonge na watu wanaoonewa.
 
Siyo suala la kutaka ni suala la italiana. Ukiwaondoa na kuwaweka wasiokuwa wanachama wa chama chochote unajuaje unaowaweka hawana mapenzi au ushabiki wa chama chochote?
Wataangaliwa historia yao. Mfano sio wanachama wa chama chochote for the past five years. Hii isimamiwe na sheria na mtu anaapa, kinyume chake anaadhibiwa vikali. Tuko mil 50+, kupata watu 200 wasimamizi wa uchaguzi ambao ushahidi unaonyesha sio wanachama yawezekana.
 
MUNGU WA MBINGUNI ANAYAONA HAYA
 
...... matatizo yenyewe ndiyo hayo; sizitaki mbichi hizi
 
Hahahaa. What a weak argument. Kwenye utawala wowote wa kiimla usitegeee wanaomtumikia mtawala watafanya maamuzi au kutenda kwa utashi wao. Mtu anateuliwa kwa kuambiwa na mtawala wake kwamba asipofanya X basi Y itamtokea, halafu unaleta hoja mufilisi kwamba maadili binafsi ya watumishi wa umma ndo kigezo kinachoamua kama watafanya ufisadi wa kisiasa au hawatafanya. Unaishi kwenye pango gani Mzee ambapo hata mambo rahisi yanayoendelea ulimwenguni huwezi kuyaelewa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…