Jaji Lubuva ajibu mapigo ya UKAWA kuhusu BVR

Jaji Lubuva ajibu mapigo ya UKAWA kuhusu BVR

Mkuu ulipotea sana , hebu nijalie matokeo ya marudio ya uchaguzi wa Serikali za mitaa huko Sumbawanga.

mkuu acha uchokozi,...timu nzima ya LB bk7 haikuonekana jana, sasa unataka wakimbie tena?

BTW: nasikia magamba wameyapinga matokeo hayo.
 
Chini ya miezi miwili kuandikisha watu zaidi ya milioni ishirini Tanzania nzima, uhakiki taarifa na kisha utegeneze daftari lenye kukubalika na kutoa vitambulisho. Vitambulisho vya taifa tuna zaidi ya miaka miwili hata robo tu ya kazi haijafanyika.
 
Ninachukia sana jinsi watanzania wanavyotumia huu msamiati wa CHANGAMOTO ie. challanges

Utamsikia Mwalimu, wanafunzi wake hawajui kusoma wala kuandikia akisema kwamba Shule yangu ina changamoto ya wanafunzi kutojua kusoma na kuandika!

Shule haina madawati. Mwalimu mkuu utamsikia anasema kwamba Shule yangu ina changamoto ya kutokuwa na madawati!

Mtanzania hana fedha mfukoni. Utamsikia anasema nina changamoto ya kutokuwa na fedha naomba unikopeshe.

Mtanzania amefiwa na baba/mama yake, Utasikia anasema nina changamoto ya kufiwa na baba/mama yangu!

Sasa sikia huyu ni Judge, NEC haina vifaa vya kutosha vya kuandikisha wapiga kura. Vifaa vilivyopo kwasasa ni 250 badala ya 5,000 vinavyotakiwa kuandikisha Watanzania wote wenye sifa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.

Yeye tatizo hilo la ukosefu wa vifaa vya kukidhi mahitaji anaita chagamoto!

Kukosa vifaa vya kutosha inakuwa CHANGAMOTO kweli?!

Msamiati wa matatizo umegeuzwa kuwa changamoto!
Haaaahaaahaaaaaaaaaa! Umenikuna! Basi tu nina changamoto sio demu vinginevyo ningehakikisha 'nakupa'
 
Tatizo ni hawa wote wanaoitwa watendaji wa serikali ni ccm tupu, tumeona juzi aliyekuwa polisi akishika mikoa mbalimbali kama rpc leo anagombea ubunge kupitia ccm na wengine wanateuliwa kushika nyadhifa za juu ndani ya chama.
Tusishangae hata mzee lubuva anakitumikia chama cha mapinduzi katika kuhakikisha hujuma inafanikiwa
 
Mashine ya BVR haisomi vidole vilivyogangamala jaji anasema ni idadi ndogo sana. Jaji mzima ansema pale Makambako ni idadi ndogo lakini jaji mzima anashindwa kuelewa pale ni mjini. Ndio maana anaona watu ni wengi na wenye vidole sugu wachache. Jaji anashindwa kuunganisha doti kwamba nchi hii ni kubwa sana na asilimia 80 wapo vijijini wanalima na kagonga mawe. Hao idadi kubwa wana vidole sugu je jaji mzima amejiandaaje na tatizo hilo. Jaji mzima anaanza kupiga porojo kama mswahili na kujiruhusu kujiondoa ufahamu kama wale waliomtuma ili akamilishe kura ya maoni 30.4.15. Jaji mzima haoni hiyo ni ndoto ya mchana lakini anaendelea kupiga domo kama wanywa kahawa wa Saigon Club ya pale Kariakoo. Jaji mzima anaulizwa kama kura ya maoni ipo Aprili 30, jaji mzima anajiumauma tu eti anaangalia hali halafu atawataarifu wananchi. Jaji mzima anashindwa kuelewa na kuwa muwazi kwamba hilo jambo haliwezekani na kama wanaotaka kura ya maoni 30 April wanaendelea na wanang'ang'ania tu, si awasukumie shipa lao ili alinde heshima yake. Namhurumia sana jaji mstaafu kwa maswaibu yanayompata. Hivi hajajifunza tu wakina jaji Kisanga, Nyalali, Warioba yaliyowapata baada ya kufanya kazi zilizotukuka lakini wakasimangwa sana na watu wenye akili nyepesi lakini madaraka na mamlaka zimewalemea kama Machiavelli alivyowa-describe ma-absolute monarchies wa renaissance kule ulaya. Kwanza ni walevi wa madaraka "power corrupts absolutely" na kwamba ili waingie madarakani hao mambwana wanasem "the means justify the end" Kwa Tz jaji Luvuba ndio means yenyewe kama hajielewi na kujitambua basi ana matatizo ya ugonjwa mbaya sana wa "retirement stress." Ukweli utajidhihirisha muda si mrefu na jaji mzima atachuma aibu yake.
 
Back
Top Bottom