Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,348
- 26,144
Pamoja na kusemwa,kukosolewa,kukejeliwa,kuombewa dua baya na kutajwatajwa kwa kiburi na kejeli ndani ya Bunge Maalum la Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba amebaki alivyo. Uzalendo wake kwa nchi;utii wake kwa chama tawala-CCM,weledi wake wa kiuongozi na kitaaluma umemuweka Jaji Warioba kuwa mtu wa kipekee.
Jaji Warioba anaijua nchi hii zaidi ya mamilioni ya wananchi wa Tanzania.Anaijua ilipotoka,ilipo na inakokwenda. Jaji Warioba anawajua viongozi wote wakuu wa nchi hii-kuanzia Mwalimu Nyerere hadi Rais Kikwete. Anaujua uimara na udhaifu wa kila mmoja. Kutokana na kuiva kwake kiuongozi,anabaki na mambo yake akilini na moyoni mwake.
Jaji Warioba hana 'bifu' na mtu. Angekuwa hivyo,mara kwa mara angejitokeza kupambana na wanaomsema.Hafanyi hivyo.Kila akiongea,hujielekeza kwenye Rasimu ya Tume yake na kuitetea. Uzalendo wa Jaji Warioba umejidhihiri leo katika Maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Alijitokeza kwa heshima,utii na unyenyekevu mbele ya Rais Kikwete kupokea zawadi yake aliyotunukiwa. Hakujificha;hakusita.
Mungu akupe maisha marefu Jaji Warioba na uione nchi hii ikineemeka!
Jaji Warioba anaijua nchi hii zaidi ya mamilioni ya wananchi wa Tanzania.Anaijua ilipotoka,ilipo na inakokwenda. Jaji Warioba anawajua viongozi wote wakuu wa nchi hii-kuanzia Mwalimu Nyerere hadi Rais Kikwete. Anaujua uimara na udhaifu wa kila mmoja. Kutokana na kuiva kwake kiuongozi,anabaki na mambo yake akilini na moyoni mwake.
Jaji Warioba hana 'bifu' na mtu. Angekuwa hivyo,mara kwa mara angejitokeza kupambana na wanaomsema.Hafanyi hivyo.Kila akiongea,hujielekeza kwenye Rasimu ya Tume yake na kuitetea. Uzalendo wa Jaji Warioba umejidhihiri leo katika Maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Alijitokeza kwa heshima,utii na unyenyekevu mbele ya Rais Kikwete kupokea zawadi yake aliyotunukiwa. Hakujificha;hakusita.
Mungu akupe maisha marefu Jaji Warioba na uione nchi hii ikineemeka!