Jaji Bomani awachafua wazanzibari

Wewe unasema wapiga kura walizidi huko Pemba.
Sasa nikuulize swali moja tu jepesi, hivi si kila kituo kulikuwa na mawakala wa vyama vyote?
Sasa kama mawakala hao, pamoja na wa vyama vya CCM na CUF waliweka saini ya fomu za matokeo, ikiwa na maana walikuwa wamejiridhisha kuwa uchaguzi haukuwa na kasoro zozote.
Sasa huyo Jecha kukurupuka na kutangaza kuyafuta matokeo hayo tena bila kushirikisha makamishna wenzake wa ZEC, hivi huo bado
haujawa ushahidi wa kutosha wa mazingira kuwa Jecha 'aliamriwa' na CCM kutoa tamko hilo baada ya kugundua ya kuwa mgombea wao Dr Shein amebwagwa na Maalim Seif?
Kwa hali inayoendelea nchini mwetu ya CCM kutaka kung'ang'ania madarakani hata kwenye yale maeneo wanayojua dhahiri wameshindwa, kutakuja kuiletea maafa nchi hii.
Mfano halisi ni uchaguzi huo wa Zanzibar na hivi sasa umehamia kwenye uchaguzi wa mameya huku Bara.
Tumeshuhudia huko Tanga jana namna uchaguzi wa meya wa huko, namna msimamizi wa uchaguzi alivyoamua kumtangaza mgombea wa CCM ambaye alishindwa kuwa ndiye mshindi na mgombea wa CUF ambaye ndiye aliyeshinda akatangazwa kushindwa!
Hata hivyo kama lilivyotokea kwa Jecha baada ya kuyafuta matokeo ya Zanzibar 'akapelekwa' mafichoni, vivyo hivyo kwa msimamizi wa uchaguzi wa jijini Tanga, naye amesepa kwenda mafichoni mara tu baada ya kutangaza kuwa mgombea wa CCM kuwa ndiye aliyeshinda uchaguzi.
Hivi kama kweli msimamizi huyo angekuwa ametangaza kitu ambacho yeye aliamini ndicho sahihi, ni kitu gani kilichomtoa nduki baada ya kuyatangaza matokeo hayo??!!!!
 
Kama kweli jaji ameongea haya basi akapimwe akili!!!
Huyo Bomani ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa serikali, kwa kuyatamka hayo ameishusha taaluma yake ya uanasheria kwa kiwango cha hali ya juu sana.
Ninaamini kuwa huyo mzee ameamua kuiweka 'rehani' pale Lumumba hiyo taaluma yake ya uanasheria.
 

Toa ushahidi
 

Ahsante sana

Nakumbuka kauli ya Rais wananchi warudi nyumbani baada ya kupiga kura, hakuna kulindwa kura, kila chama kina wakala wa kulinda kura,na kila kituo kuna list ya wapiga kura, jee walikuwa wapi hao mawakala?
 
Pokea like zangu 100 kwa mpigo.
Huo ni ukweli mtupu wa asilimia 100 uliompa Mheshimiwa Rais wetu Magufuli ili autafakari na kuuchukulia hatua.
Kwa hiyo kazi imebaki kwake aidha kusuka au kunyoa.
 
Mayor....uchaguzi wake Tanga.Mayor.......uchaguzi wake kinondoni.......na Mayor uchaguzi wake Ilala.Tuiombee Burundi amani.
 
Jaji Bomani hawezi kupendekeza liundwe jopo hapohapo akisema uchaguzi urudiwe, angeacha jopo liamue.
 
Ngigana Watanzania wa Zanzibari Uchaguzi umeishapita, Tafadhari kuondoa hii kadhia Matokeo yatangazwe, mshindi kwa asilimia sitini anajulikana!!
MaCCM kubali kushindwa Uchaguzi wa Zanzibari, mpeni Maalimu Seif na CUF nchi!!!
Fanyeni maridhiano wakiwa na Serikali yao, mnataka tulipuliwe mabomu??
 
Last edited by a moderator:
Inasikitisha sana kama nchi kuwa na watu kama bomani.Unategemea kuwa watakuwa wakombozi kwa weledi walio nao lakini wanageuka vibaraka wachumia tumbo.
 
Duuuh huyu bomani hora angekaa kimya tu kuliko kujidhalilisha huku

Tatizo la watu wa kina Bomani ni kutanguliza UKEREKETWA NA UKADA na si TAALUMA NA UKWELI, huu ni ugonjwa kwa wataalamu wetu na hata washauri wa viongozi wetu wakubwa. Kwa hali hii watu wasimshangae jaji Bomani bali ekemewe .
 
Tatizo la watu wa kina Bomani ni kutanguliza UKEREKETWA NA UKADA na si TAALUMA NA UKWELI, huu ni ugonjwa kwa wataalamu wetu na hata washauri wa viongozi wetu wakubwa. Kwa hali hii watu wasimshangae jaji Bomani bali ekemewe .

Tusisahau kwamba kutenganisha majukumu masuala yauchaguzi na muungano ni kuwatukana na kuwadhihaki waasisi wa muungano walio uunganisha kwa ishara ya mchanga. Hakika km matokeo ya uchaguzi Zanzibar ni batili basi na huku bara tunaongozwa na serikali batili.
 
Tuendako ni hatari sana na kama swala la Zanzibar litachukuliwa kizarau....wataanza kujitoa muhanga tena zaidi bara
 
Alichokifanya Maalim ni sawa na mwanafunzi wa kidato cha nne alieliona jina lake kwenye karatasi ya waliofaulu kwenye ukuta wa shule na kusema kuwa amefaulu ila anasubiria kutangazwa kwenye redioni tu.
 
Uchaguzi mkuu Zanzibar, Chaguzi za mameya Tanga, Ilala, Kinondoni-zinaonyesha dhahiri ni chama gani kinachovuruga chaguzi na amani Tanzania halafu vyombo vya dola vinaclaim kuwa na inteligensia.
 
Mkuu umenena haswa mimi kwa uono wangu tokea hapo zamani nilikuwa siamini kama tuna wasomi nchini ila kuna watu wenye njaa na kutaka kula yao isiwekewe kizuwio. Watu kama Shivji,Mwakyembe na wasomi wengine kwanini wanaweka maslahi ya chama kwanza kuliko nchi. Pia ukitaka kujua kama sisi Watanzania tuna matatizo ya akili angalia leo tuna Prof Ibrahim Lipumba ni Proffessor wa uchumi kwanini tusimtumie kuukuza uchumi?? lakini utaambiwa sio ccm. Ndio maana au mtu kasomea Medical lakini unamkuta yupo Bot na aliesomea Politics ndio utasikia waziri wa afya mmhh kweli sie masokwe.:crazy:
 
karibuni tutamuona jaji warioba kwenye itv atakuja kusema haya haya aliyosema jaji bomani kwa style tafauti kidogo lakini ujumbe utakuwa ule ule ni msimamo wa ccm,
ccm wanawabana hawa wazee kwenye koo kwa kamba ya pension na matibabu wanawaburuza kila wanapowahitaji kuwatumia
kwa wazee wenye kehma na busara kama hawa wanapokuja kukinzana na taaluma zao na ufahamu wa hali halisi ni aibu sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…