GE2025 Itutu: Tunaiomba Serikali itoke hadharani ikemee utekaji

GE2025 Itutu: Tunaiomba Serikali itoke hadharani ikemee utekaji

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mgombea Ubunge Jimbo la Ilemela kupitia Chama cha Alliance For Democratic Change (ADC), Shabani Itutu ameitaka Serikali itoke hadharani kukemea matukio ya utekaji yanayoendelea kuripotiwa nchini

Akizungumza na wananchi kwa nyakati tofauti kwenye ziara ya kampeni ya mtaa kwa mtaa katika kata ya Kahama, Busweru, Kangahe, Kirumba na Kitangiri, Shabani Itutu amedai kitendo cha Serikali kuendelea kukaa kimya kinaweza kupelekea kushamili kwa matukio hayo na kuonekana ya kawaida katika jamii hali itakayokuwa inahatarisha usalama na amani nchini

"Toka utekaji utokee sijaiona Serikali ikitoka hadharani kukemea utekaji, tunaiomba Serikali itoke hadharani ikemee utekaji, watoto wa wenzao wa maskini wanatekwa huku wakiacha masikitiko kwa familia zao wakati walikuwa wakitegemewa," amesema Itutu

Ameongeza kuwa "Utekaji umetawala hii nchi lazima tuukemee kwa pamoja tusipokemea utekaji utakuja kuvunja amani ya nchi, watu wataona utekaji ni jambo la kawaida, utekaji unaumiza sana chukulia ametekwa baba, dada, kaka, shangazi yako halafu watu wanadunda hawachukui hatua yoyote,"

Hata hivyo Itutu amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi kuchagua viongozi watakao waletea maendeleo huku akiwataka wananchi kuwapuuza wale wote wanaokusudia kufanya maandamano


 
Mgombea Ubunge Jimbo la Ilemela kupitia Chama cha Alliance For Democratic Change (ADC), Shabani Itutu ameitaka Serikali itoke hadharani kukemea matukio ya utekaji yanayoendelea kuripotiwa nchini

Akizungumza na wananchi kwa nyakati tofauti kwenye ziara ya kampeni ya mtaa kwa mtaa katika kata ya Kahama, Busweru, Kangahe, Kirumba na Kitangiri, Shabani Itutu amedai kitendo cha Serikali kuendelea kukaa kimya kinaweza kupelekea kushamili kwa matukio hayo na kuonekana ya kawaida katika jamii hali itakayokuwa inahatarisha usalama na amani nchini

"Toka utekaji utokee sijaiona Serikali ikitoka hadharani kukemea utekaji, tunaiomba Serikali itoke hadharani ikemee utekaji, watoto wa wenzao wa maskini wanatekwa huku wakiacha masikitiko kwa familia zao wakati walikuwa wakitegemewa," amesema Itutu

Ameongeza kuwa "Utekaji umetawala hii nchi lazima tuukemee kwa pamoja tusipokemea utekaji utakuja kuvunja amani ya nchi, watu wataona utekaji ni jambo la kawaida, utekaji unaumiza sana chukulia ametekwa baba, dada, kaka, shangazi yako halafu watu wanadunda hawachukui hatua yoyote,"

Hata hivyo Itutu amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi kuchagua viongozi watakao waletea maendeleo huku akiwataka wananchi kuwapuuza wale wote wanaokusudia kufanya maandamano


Wanawezaje kukemea jambo wanalolifanya wao wenyewe?
 
Back
Top Bottom