Itifaki Ilivyozingatiwa kwenye Msafara wa TBL

Mafuchila

JF-Expert Member
Apr 29, 2006
751
65
TBL Motorcade.jpg
 
Huo ulikuwa ni msafara wa wa Magali ya TBL ukiwa unatoka katika uwanja wa ndege Mwalimu Nyerere, baada ya kuwasili kwa tuzo yao waliyoipata huko Ujerumani.
 
Huu ni muendelezo wa foleni na msongamano katika jiji letu la Dar.

Nasema hivi, kwani siku za karibuni imekuwa ni kawaida kuruhusu magari kufanya maandamano ilhali barabara zetu zimeshazidiwa. Huu ni upungufu wa fikira.
 
Kuongeza foleni bila sababu za msingi!

Hiyo tuzo ina-compensate vipi "man/hour" zinazopotea barabarani?
 
Huu ni muendelezo wa foleni na msongamano katika jiji letu la Dar.

Nasema hivi, kwani siku za karibuni imekuwa ni kawaida kuruhusu magari kufanya maandamano ilhali barabara zetu zimeshazidiwa. Huu ni upungufu wa fikira.
Hakuna sheria zozote zinazosimamia hali kama hii?
 
......utakuta watu wana sherehe binfasi mathalan harusi, au shughuli ya kidini (something sounds like 'maulid') wanafunga barabara. niliwahi kuuliza wahusika kama wana kibali,wakasema hawana kibali kwa vile wanafunga barabara kwa muda mfupi tu wa masaa kama manne!!! hii naongelea Tanga..ni common sana hii kitu!!!
 
Nami nilistaajabu sana kuona upuuzi huu! Ningependa sana kujua kama TBL waliilipa Serikali kutumia polisi wa Trafiki. All in all ni ujinga uliotukuka
 
Hii nchi ina 'wenyewe'..nyie kaeni tu hapo kazi kutoa mijicho kaa mijusi iliyobanwa na mlango.
 
Back
Top Bottom