It is Now OR---

Kalamu

Platinum Member
Joined
Nov 26, 2006
Posts
19,508
Reaction score
26,132
.... Kamwe siwezi kusema 'Never' kwa Tanzania yetu hii; lakini tukiikosa fursa hii ya Oktoba 29... 'It is going to be very messy in future kuwaondoa madarakani waovu hawa.

Wanatuonyesha vigali vya polisi kwa hofu kubwa sana, na kujitangaza mara mbilimbli kuwa maAmiri Jeshi Wakuu; yote haya ni kwa hofu ya kujuwa waTanzania wakiamua kweli wakati huu ndio mwisho wao..

Oktoba 29, ni siku ya kipekee sana kwa nchi yetu.

Kinacho ombwa kwa kila mTanzania, ni kujitokeza tu kuandamana. Hutakiwi kufanya kitu kingine chochote

Kuwepo kwako katika maandamano hayo popote pale utakapokuwa ndiyo kinga sahihi ya kuepusha maisha ya waTanzania wenzako.

Polisi watano hadi kumi hawawezi kuwakabili waTanzania elfu ishirini sehemu yoyote hapa nchini.

Unachotakiwa ni kuwepo, huhitaji kukimbizana na mtu yeyote siku hiyo. Polisi akithubutu atakimbia mwenyewe.

Wewe njoo tu tushirikiane kuandamana ili tuwaondoe watu waovu hawa wanaolididimiza taifa letu.

Tusipo fanya hivi wakati huu, maana yake ni kwamba tumekubali maumivu makali ndani ya utawala huu.

Ni kwamba tumekubali kufanywa watwana ndani ya nchi yetu; ni kwamba tumekubali kunadi raslimali za nchi yetu tulizo jaliwa na Mwenyezi Mungu ili zitusaidie kuinua hali ya maisha ndani ya nchi yetu Tutakuwa tumekubali kupoteza utu wetu, HAKI zetu katika mambo yote yanayo tuhusu kama waTanzania....


Tusiiachie hii nafasi adhmu ipite hivi hivi..

Tukamwambie Samia Suluhu Hassan na Genge lake, IMETOSHA.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Swali kubwa ni nani atakuwa wa kwanza kuwagomea polisi..atakayekuwa wa kwanza kupigwa kirungu...na wa kwanza kuuawa...

Ingawa yanaitwa "maandamano" yaandaliwa kama mapambano na polisi...hapa ndipo palipo pagumu.

Ila kweli kama siyo sasa..basi mabadiliko yatahairishwa tena.
 
Hamna kitu kama hicho
 
Reactions: Tui
Ingawa yanaitwa "maandamano" yaandaliwa kama mapambano na polisi...hapa ndipo palipo pagumu.
Unajuwa kwa nini? Polisi ndio wanafanya kila kitu kionekane kuwa ni mapambano; sasa waTanzania wafanyeje?
Wewe huoni tayari akina Muliro wanavyo pambana kila mahali?
Watu kwenda tu mahakamani kusikiliza kesi wanavunjwa miguu; hayo tayari siyo mapambano?
Swali kubwa ni nani atakuwa wa kwanza kuwagomea polisi..atakayekuwa wa kwanza kupigwa kirungu...na wa kwanza kuuawa...
Kwa nini hili liwe swali kubwa; na kwa nini liwahusu waandamanaji zaidi ya 20,000 dhidi ya polisi watatno. Hao polisi hilo swali wao haliwahusu?

Na cha muhimu zaidi, unasahau kuwa hao polisi ni waTanzania , wanazo akili timamu; na wao hawapiganii maslahi anayopigania Samia Suluhu Hassan na Genge lake.

Hili lisiwe swali la kuwatia uoga waTanzania kama afanyavyo Mulilro na huyo Kamanda wake Mkuu. Sitegemei wewe kuwa sehemu ya hao watu waovu.
 
Hii kitu tunatoka, vijana wamefikia breaking point, wamechoka sana kuibiwa.
Kwa kuwa maandamano ni ya nchi nzima na kila sehemu hadi vijijini, mitaani waTanzania wote washiriki.
Kama ilivyo vita, vijana wanakwenda mstari wa mbele; lakini hata waTanzania wengine wanachangia juhudi hizo kwa njia mbalimbali; kama ilivyokuwa wakati wa vita ya Nduli Idd Amin.
 

Kwani wewe utakuwa umejificha wapi?

Hebu jitolee basi uwe kama Dr King kwenye maandamano yake mengi wakati wa civil rights movements

 
Je maandamano yanaelekea wapi?
Je maandamano yana malengo gani?
Au ni maandamano ya kutoa ccm mdarakani?

Kama yanaiga mfumo wa kuelekea ikulu kama Sri Lanka, Bangladesh na Nepal inabidi watu waende ikulu dar hata kwa fisi au kwa ungo.

Au maandamano yaanzie stendi ya kivukoni, stendi ya mwendokasi kivukoni, au stendi ya feri kwenye pantoni upande wa posta.
Au watanzania woooote na watu wote waende kama wanaenda kwenye ibada kwenye misikiti na makanisa yaliyo karibu na ikulu
Kwa misikiti waende kuswali misikiti ya posta, upanga, kariakoo, magomeni

Msikiti wa kisutu, kitumbini, kariakoo kwa mtoro, ksij, msikiti wa maamur upanga.

Makanisa
Watanzania woooote waende kusali misa za St Joseph cathedral ya posta na Azania Front ya posta.
Pakiwa na nyomi kwenye misa ya St Joseph cathedral na Azania Front ya posta pamoja nyomi kwenye stendi ya kivukoni kuingia ikulu ya Dar ni fasta tu.

Pia kuna ccc upanga na kkkt kariakoo
Mitaa ya posta iwe na nyomi, upanga na kariakoo pawe na nyomi kubwa lote linaelekea ikulu

Inabidi pawe na watu laki mbili hadi 1m karibu na ikulu baada ya hapo safari ya kuelekea ikulu inaanza. Labda iwe hivyo.


NB: ikulu zipo nyingi sana, Kuna Dar, Dodoma, Zanzibar, Kila mkoa una ikulu ndogo
 
Polisi ndio wanaharibu, wangeacha watu waandamane huku wakiwapa ulinzi matishio yote haya yasingekuwepo.

Ila walipoanza vitisho ndio watu nao wamereact.
 
Do the Maasai way, 3 days done
 
Kwani wewe utakuwa umejificha wapi?

Hebu jitolee basi uwe kama Dr King kwenye maandamano yake mengi wakati wa civil rights movements

View attachment 3492983
Ukimsoma huyu Mwenyekijiji; mstari wake huo wa kwanza lengo lake ni kutia watu hofu, uoga.
Sasa nashindwa kujuwa watu wa aina ya huyu wanafaidika vipi na utawala huu.

Inasikitisha zaidi, ukirudi nyuma kabisa kuangalia mtu kama huyu alivyo kuwa kutokana na maandishi yake ya wakati huo!
 
Kwa namna CCM inavyoendesha nchi, muda wowote mambo yanaweza kulipuka. Sasa hivi serikali kwa kutumia vyombo vya dola imeamua ku-operate kama kikundi cha wahuni na kila siku ndivyo wanavyozidi kuharibu. Tarehe 29 inaweza kabisa kupita salama, lakini tayari tumeshafikia kwenye point of no return. Ufisadi na mauaji yote ambayo yameshafanyika mpaka sasa HAYATARUHUSU kabisa CCM kubadilika tena na kuwa kama zamani. Hata katiba wanayosema ''watatoa'' itakuwa mbovu kuliko hii ya sasa ili iwalinde.
 
Inatakiwa tujue tukitoka kuandamana direction na destination ni wapi?!

vituo vya kupigia kura?
vituo vya polisi au wapi?
hapo ndo me sijaelewa
tukisema tutoke kila mtu kwake lazima kuwe na sehem ya kukutana la sio itakuwa ni uzurulaji Tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…