Is there any correlation between colonels and coups in west African nations?

Is there any correlation between colonels and coups in west African nations?

donlucchese

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2011
Posts
17,257
Reaction score
22,130
Salam wakuu

Straight to the point... Tumeshuhudia nchi nyingi sana za Africa magharibi uongozi wa juu (Rais) akipinduliwa na Jeshi kuingia madarakani. Miezi michache iliyopita luteni kanali mamady doumbouya alishika chat baada ya kuipindua serikali ya Guinea nakushika madaraka ya uRais, hatujapoa naona luteni kanali Paul Henry Damiba wa Burkina Faso ametwaa madaraka ya uRais.

Swali langu wakuu, Kuna mahusiano gani ya hiki cheo Cha luteni kanali na coup d'etat? Je, kwanini wasiwe mabrigedia, majenerali au wakuu wa majeshi kabisa lakini ni maluteni kanali? Naomba kuwasilisha
 
Salam wakuu
Straight to the point... Tumeshuhudia nchi nyingi sana za Africa magharibi uongozi wa juu (Rais) akipinduliwa na Jeshi kuingia madarakani. Miezi michache iliyopita luteni kanali mamady doumbouya alishika chat baada ya kuipindua serikali ya Guinea nakushika madaraka ya uRais, hatujapoa naona luteni kanali Paul Henry Damiba wa Burkina Faso ametwaa madaraka ya uRais.
Swali langu wakuu, Kuna mahusiano gani ya hiki cheo Cha luteni kanali na coup d'etat? Je, kwanini wasiwe mabrigedia, majenerali au wakuu wa majeshi kabisa lakini ni maluteni kanali? Naomba kuwasilisha
Hiyo ni regression si correlation basi
 
Labda kwa sababu colonel anakuwa inbtween. Bado anaonekana sehemu ya Wanajeshi wa ngazi ya chini wakati huohuo anaelekea kuwa kwenye tabaka la wakubwa jeshini. Colonel Muamar Gadafi case
Kanali jeshini sio ngazi ya Chini jeshini... Kanali ni miongoni mwa maafisa wangazi ya juu jeshini.... Kikosi anachoweza handle brigedia jeshini pia Kanali huweza ki handle... Kanali ni senior officer
 
Salam wakuu

Straight to the point... Tumeshuhudia nchi nyingi sana za Africa magharibi uongozi wa juu (Rais) akipinduliwa na Jeshi kuingia madarakani. Miezi michache iliyopita luteni kanali mamady doumbouya alishika chat baada ya kuipindua serikali ya Guinea nakushika madaraka ya uRais, hatujapoa naona luteni kanali Paul Henry Damiba wa Burkina Faso ametwaa madaraka ya uRais.

Swali langu wakuu, Kuna mahusiano gani ya hiki cheo Cha luteni kanali na coup d'etat? Je, kwanini wasiwe mabrigedia, majenerali au wakuu wa majeshi kabisa lakini ni maluteni kanali? Naomba kuwasilisha
Kanali ni kiongozi wa kikosi maalum ndani ya jeshi (regiment) iwe cha makomandoo au kazi zingine maalum.

Ndo maana wana uwezo wa kuamua kuchukua nchi kutokana na ujuzi na elimu ilotukuka kuhusu masuala ya kijeshi.

Kanali Doumbouya ana CV ya kijeshi iloshiba na kati ya kozi alozifanya ipo kozi maalum ya kijeshi amefanya nchini Israeli kwenye chuo kiitwacho International Security Academy.

Kanali Paul Henry Damiba nae pia ni msomi ( ana masters degree ya criminology) na "in fact" yeye na Alpha Konde (rais wa Guinea alepinduliwa na Doumbouya) walisoma pamoja kwenye chuo cha kijeshi cha Ecole kilichopo Paris nchini Ufaransa.

Ndo maana Doumbouya amemweka mahali salama bwana Alpha Konde kwani anafahamu umahiri wake kijeshi.

Ila Damiba ni Luteni kanali ambacho ni cheo cha chini ya kanali na alikuwa miongoni mwa walinzi wa rais Blaise Compaore.

Damiba nae ni mwanajeshi wa ngazi ya juu kabisa kijeshi na ana mafunzo ya kijeshi kutoka Marekani na ameongoza operesheni nyingi dhidi ya ugaidi na ameandika kitabu (kitafute usome) chaitwa "West Africa Armies and Terrorism: Uncertain Responses?"

Hivyo tukirudi kwenye suali lako kwamba kuna correlation? jibu ni kweli, kwani bila hawa viongozi wa vikosi maalum jeshini uwezekano wa kufanya mapinduzi kitaalam huwa ni mdogo sana.

Kwahiyo kunakuwepo na kikosi maalum au Unit kiwe cha makomandoo au wale wa ulinzi wa raisi (regiment of presidential security) ndo mipango huwa nadhifu.
 
Labda kwa sababu colonel anakuwa inbtween. Bado anaonekana sehemu ya Wanajeshi wa ngazi ya chini wakati huohuo anaelekea kuwa kwenye tabaka la wakubwa jeshini. Colonel Muamar Gadafi case
Luten Kanali Makamba, Simba Kalia, Kinana, na wale maluten walitaka kumpindua Mchopa
 
"Damiba...ameandika kitabu (kitafute usome) chaitwa "West Africa Armies and Terrorism: Uncertain Responses?""

Ninadhani alikisoma kitabu chake na akaona tatizo huko Burkinabe
Acha mzaha bana 🙂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom