Mwakamajoka
Senior Member
- Nov 21, 2017
- 170
- 149
Tehran(Irani) wamesema malalamiko ya Tel Aviv(Israeli) kuhusu Unmanned Aerial Vehicle(UAV)/Drone ya Irani kuangushwa na ndege ya Taifa la Israeli ni jambo ambalo ni upuuzi(illogical). Kamanda wa Irani emeonya kwamba watairuhusu/kuifungulia JEHANAMU kwenye ngome ya Kizayuni na kuharibu vituo vyote vya kijeshi vya Marekani vilivyopo nchini Israeli.
"Tuhuma kuhusu ndege/Drone ya Irani na kuhusika kwa Irani kuitungua ndege vita ya Kizayuni ni upuuzi", Bahran Qassemi(Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje wa Irani).
Bahran Qassemi amesema maofisa wa Irani nchini Siria wanafanya kazi za kishauri na wanafanya shughuli zao kwa ombi la serikali halali ya Siria na ya kisheria.
"Vitendo korofi vingine vikifanywa na Tel Aviv(Israeli) vitasababisha serious response. Na hiyo ndiyo itakayo kuwa sababu ya Irani kutengeza JEHANAMU ndani ya Taifa hilo la Kizayuni(Israeli)", Brigadier General Hosseini Salami(Mkuu msaidizi wa Iran's Elite Revolutionary Guards Corps).
Qassemi akaendelea kutema cheche kwa kusema Siria ni Taifa, na Serikali yake na Majeshi yake yanahaki ya kuiilinda mipaka ya nchi na kupambana na aina yoyote ya vitendo tukutu/korofi vya kigeni. Mapema siku ya Jumamosi Jeshi la Ulinzi la Israeli(IDF) limesema limeidhibiti UAV/Drone ya Irani ambayo iliruka mpaka wa Siria na kuingia Israeli. Kwa kujibu mapigo Israeli ilifanya mashambulizi ya anga kwenye maeneo yenye shughuli za Irani nchini Siria.
Jeshi la Israeli badae likasema kwamba ndege vita moja F-16 ilianguka kutokana na mashambulizi makubwa yaliofanywa na Siria. Marubani walifanikiwa kutoka ndani ya ndege na wapo salama. Kwa kujibu mashambulizi ya Siria, Israeli Defense Force (IDF) ikafanaya mashambulizi ya kutosha kwenye maeneo 12 yenye shughuli za Irani nchini Siria, Damascus hawajasita kusema vitendo vya Israeli ni UKOROFI.
Kugusia Sera za Marekani nchini Irani na vikwazo walivyowekewa Jamhuri ya Kiislamu(Irani), Salami amesema Irani inaweza kuharibu vituo vyote vya kijeshi vya Marekani vilivyopo nchini Israeli kwa kufanya mashambulizi kutoka nchini Irani.
Wasiwasi umepamba moto kati ya Israeli na Irani kutokana na tukio la Jumamosi. Jeshi la Israeli limemuonya Siria na Irani kwa kuruga uhuru wake kama Taifa kwa kusema kwamba nchi zote (Irani na Siria ) watalipa ghalama kubwa wakikiuka onyo hili. Israeli Defense Force (IDF) likaweka mkazo kwa kusema Tehran na Damascus wanacheza na MOTO.
We could ‘destroy all US bases in region & create hell for Zionist regime’ – Iranian commander