kenny mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 17, 2021
- 322
- 902
Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran irudi haraka kwenye meza ya mazungumzo na kusaini makubaliano ya kusitisha mpango wa nyuklia kabla haijapoteza kila kitu. Rais Trump ameandika hayo kupitia ukurasa wake wa Truth social Taarifa hiyo nmekuekea hapo chini kwenye comments
Trump amesema anafahamu mipango yote ya kimkakati ya mashambulizi ya Israel na inayofuata ni mikubwa na ya kikatili zaidi hivyo Iran isithubutu kuingia kwenye mtego wa kujaribu kupigana na Israel kwakua itapoteza kila kitu ikiwemo utawala wa Ayatollah
Rais Trump amesema Israel ina uwezo mkubwa kimedani na silaha za hatari ikiwemo za ubora wa juu mno zinazozalishwa Marekani na mbaya zaidi inajua kuzitumia kwa usahihi mkubwa
Trump anasema aliipa Iran siku 60 kusaini makubaliano ila ikazembea nafasi hiyo hatimaye usiku wa kuamkia leo ambapo ilikuwa ni siku ya 61 Israel ikachukua hatua kali. Trump anasema aliionya Iran kwamba inaweza kukumbana na hatua ambazo haijawahi kushuhudia, kuambiwa au kusikia ila ikawa haiamini ikadhani ni vitisho vitupu tu
Rais Trump amesema jambo lenye tija kwa sasa kwa Iran ni kuchangamkia fursa ya mazungumzo kukwepa mkono zaidi wa Israel, fursa ambayo ameiita kama nafasi ya pili "Second Chance" na kuitaka Iran kuitumia haraka kabla mambo hayajaharibika kabisa
Wakati huo huo rais wa Iran Masoud Pezeshkian amelaani mashambulizi ya Israel na kuapa kwamba lazima Iran ilipize kisasi chenye uzito unaostahili
Je Iran itajibu ili kupata awamu ya pili ya mashambulizi ya Israel?.
Trump amesema anafahamu mipango yote ya kimkakati ya mashambulizi ya Israel na inayofuata ni mikubwa na ya kikatili zaidi hivyo Iran isithubutu kuingia kwenye mtego wa kujaribu kupigana na Israel kwakua itapoteza kila kitu ikiwemo utawala wa Ayatollah
Rais Trump amesema Israel ina uwezo mkubwa kimedani na silaha za hatari ikiwemo za ubora wa juu mno zinazozalishwa Marekani na mbaya zaidi inajua kuzitumia kwa usahihi mkubwa
Trump anasema aliipa Iran siku 60 kusaini makubaliano ila ikazembea nafasi hiyo hatimaye usiku wa kuamkia leo ambapo ilikuwa ni siku ya 61 Israel ikachukua hatua kali. Trump anasema aliionya Iran kwamba inaweza kukumbana na hatua ambazo haijawahi kushuhudia, kuambiwa au kusikia ila ikawa haiamini ikadhani ni vitisho vitupu tu
Rais Trump amesema jambo lenye tija kwa sasa kwa Iran ni kuchangamkia fursa ya mazungumzo kukwepa mkono zaidi wa Israel, fursa ambayo ameiita kama nafasi ya pili "Second Chance" na kuitaka Iran kuitumia haraka kabla mambo hayajaharibika kabisa
Wakati huo huo rais wa Iran Masoud Pezeshkian amelaani mashambulizi ya Israel na kuapa kwamba lazima Iran ilipize kisasi chenye uzito unaostahili
Je Iran itajibu ili kupata awamu ya pili ya mashambulizi ya Israel?.