- Toa onyo
- Toa muda
- Ongeza muda kidogo
- Adui acheke
- Halafu piga
Venezuela chini ya Nicolás Maduro walipewa nafasi. Trump akasema: ondoka kwa amani. Akaongeza muda. Maduro akacheka, akadhani ni maneno tu. Lakini muda ulipoisha Maduro akafanyiwa surprise, alibebwa juu juu mpaka Washington DC mchezo ukaisha.
Mwaka jana Trump alimwambia wazi Ayatollah: “Acheni kurutubisha nuclear.”. Alitoa nafasi. Akaongeza muda, Diplomasia kwanza kama mfanyabiashara anayetaka deal. Ayatollah akadhani huo ni udhaifu, alimcheka. Ndani ya saa chache baada ya muda kuisha B-2 bombers zikaingia. zilipiga kiwanda cha Fordow kwa precision, Kwanza Ayatollah alikana kuficha aibu Lakini satelaiti hazidanganyi. Baadaye ukweli ukatoka: miundombinu iliharibiwa vibaya na waziri alikiri pigo lilikuwa zito. Trump alimwambia wazi Ayatollah wanajua alipo na kawazuia Israel wasimuue ila akirudia Tena hawezi kumsaidia (
Vita ya sasa ilianza hivyo hivyo, Trump alimwambia Ayatollah msirejee kwenye urutubishwaji wa nuclear , Iran wakampuuza, Trump akatoa nafasi, akaongeza muda, Ayatollah akamcheka kumchukulia ni maneno matupu, kilichofuata Ayatollah kaweka rekodi ya kuwa kiongozi mkubwa kubamizwa ndani ya sekunde 40 tu pamoja na viongozi wengi wakubwa, rudia tena kusoma ni SEKUNDE 40 !
Siku chache zilizopita Trump alitoa onyo Iran Fungueni njia ya mafuta lasivyo nitapiga viwanda vyenu vya nishati na umeme, alitoa muda wa masaa 48, Kisha kama kawaida yake ameongeza muda siku 5., Iran wanafanya kosa lile lile wanamchukulia poa ni maneno tu hawezi chochote,