Kwa wale tunaofahamu Historia ya vyombo vya habari Tanzania kwa hakika mtu hawezi kubisha kuwa IPPMedia ni moja kati ya vyombo vya habari vya mwanzo na vilivyokuwa makini Tanzania kwa kuanzisha tovuti. Kwa wale walio mbali na Tanzania ambao hupenda kufahamu kimejiri nini Tanzania, hakika watakubali kuwa Tovuti ni moja wapo ya njia nyepesi kabisa katika kupata habari za Tanzania kwa ujumla ukiacha SIMU na SMS kwa ndugu na jamaa waliopo Tanzania.
Hivi karibuni kumetokea tabia ambayo ama kwa makusudi au kwa kutokuwa na uwezo kwa IPP kuwanyima watanzania habari katika mtandao wao. Naam! Ninasema hivyo kwa sababu kuu moja, hii tovuti ni active na inakuwa updated kila siku na ina matangazo ya biashara mengi, Ila tovuti hii imekuwa ikichapisha vichwa vya habari tu, yaani ukitaka kufungua kusoma zaidi link au habari haipo. Inawezekana IPPMedia wanafanya hivi ili kuwafanya watu wanunue magazeti yao lakini wanatakiwa kujua kuwa uwezo wao wa kusambaza hayo magazeti ni Kwa Tanzania tu tena baadhi ya sehemu. Watu waliopo nje ya Tanzania hawawezi kuyapata hayo magazeti.
Ushauri:
1. Kwa nini wasiitoe tu hiyo Tovuti yao badala ya kuwaibia wafadhili wanaolipia matangazo yao kwenye Tovuti hiyo kwa kuchapisha vichwa vya habari na kuwafanya wasomaji wengi kutoingia kabisa kwenye Tovuti hiyo!
2. Kama ni mbinu ya biashara, kuwafanya watu wanunue magazeti yao basi wasambaze dunia nzima hayo magazeti na sisi tulio nje tupate kuyasoma, vinginevyo waweke habari katika mtandao wao kwani ni lengo la kufungua mtandao huo.
3. Kama wakiona haiwezekani basi wafiche kurasa zao kwa watembeleaji wa Tanzania kitu ambacho kinawezekana na watembeleaji wa nje wawe na access ya habari.
Nionavyo mimi kwa mtindo huu wa IPP kweli inaonesha kuwa sasa magazeti haya yanakoenda si kuzuri.
Hivi karibuni kumetokea tabia ambayo ama kwa makusudi au kwa kutokuwa na uwezo kwa IPP kuwanyima watanzania habari katika mtandao wao. Naam! Ninasema hivyo kwa sababu kuu moja, hii tovuti ni active na inakuwa updated kila siku na ina matangazo ya biashara mengi, Ila tovuti hii imekuwa ikichapisha vichwa vya habari tu, yaani ukitaka kufungua kusoma zaidi link au habari haipo. Inawezekana IPPMedia wanafanya hivi ili kuwafanya watu wanunue magazeti yao lakini wanatakiwa kujua kuwa uwezo wao wa kusambaza hayo magazeti ni Kwa Tanzania tu tena baadhi ya sehemu. Watu waliopo nje ya Tanzania hawawezi kuyapata hayo magazeti.
Ushauri:
1. Kwa nini wasiitoe tu hiyo Tovuti yao badala ya kuwaibia wafadhili wanaolipia matangazo yao kwenye Tovuti hiyo kwa kuchapisha vichwa vya habari na kuwafanya wasomaji wengi kutoingia kabisa kwenye Tovuti hiyo!
2. Kama ni mbinu ya biashara, kuwafanya watu wanunue magazeti yao basi wasambaze dunia nzima hayo magazeti na sisi tulio nje tupate kuyasoma, vinginevyo waweke habari katika mtandao wao kwani ni lengo la kufungua mtandao huo.
3. Kama wakiona haiwezekani basi wafiche kurasa zao kwa watembeleaji wa Tanzania kitu ambacho kinawezekana na watembeleaji wa nje wawe na access ya habari.
Nionavyo mimi kwa mtindo huu wa IPP kweli inaonesha kuwa sasa magazeti haya yanakoenda si kuzuri.