Ipo siku Rais Magufuli atatuonesha mafaili anayolala nayo kitandani..

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,434
7,055
files.jpg


Najua mnajua kuhusu suala la mafaili anayolala nayo kitandani. Maana ameshalirudia si chini ya mara moja.

Kwa tafsiri nyepesi kabisa, anachojaribu kuonesha ni kwamba yeye ni mfuatiliaji na sio mtu wa kuamini taarifa za kupewa kwa muhtasari. Anazama mwenyewe.

Tusijeshangaa siku moja, aidha kwa uchovu kwa kutaka tujue uzito wa maneno yake, ataalika waandishi wa habari Ikulu na kuwapeleka mpaka chumbani anapolala kisha aoneshe hayo mafaili.

Ni dhahiri, hicho ni kilio cha kuomba msaada (a cry for help) kutoka kwa kiongozi wetu. Je, anataka tumsaidiaje?

Nadharia nilizonazo;

1. Muda: Mafaili ni mengi maana yake mambo ni mengi ya kufanyia kazi hivyo yanahitaji muda mwingi ili yote yaweze kutekelezwa. So, tumuongeze muda wa kuyafanyia kazi. Miaka 10 inaweza isitoshe.

2. Uaminifu: Ofisi yake haimpi imani ya kutosha kuweza kusaidiana nae kuchakata masuala nyeti ya kitaifa, hivyo anahitaji kueleweka pale anapoamua kufanya maamuzi ya kuwabadilisha badilisha. Zipo tetesi pia kuna watumishi wanatoka kumfanyia figisu.

3. Pride: Huenda kwake ni fahari kuwaambia watz ni namna gani anafanya kazi usiku na mchana kiasi cha kujaza vitendea kazi mpk sehemu anayolala. Lengo ni kupata kukubalika!

Tumsaidieje?
 
Anaongea ukweli ndo maana unaona wengi waliohujumi nchi hii hawampendi maana anahakikisha kila kitu kinachopita kwake anakisoma na kukitolea maamuzi na kama ulimsikia mafaili yenyewe siyo ambayo utaweza kumpa mtu mwingine ayatolee maamuzi zaidi ya yeye tu kwa mujibu wa utaratibu na hapo inaonyesha kuwa Rais wa Tz ana kazi na majukumu mengi ya kufanya kama kweli sheria zinafuatwa.
 
Anaongea ukweli ndo maana unaona wengi waliohujumi nchi hii hawampendi maana anahakikisha kila kitu kinachopita kwake anakisoma na kukitolea maamuzi na kama ulimsikia mafaili yenyewe siyo ambayo utaweza kumpa mtu mwingine ayatolee maamuzi zaidi ya yeye tu kwa mujibu wa utaratibu na hapo inaonyesha kuwa Rais wa Tz ana kazi na majukumu mengi ya kufanya kama kweli sheria zinafuatwa.
Basi apunguziwe majukumu. I mean, delegation of power ifanyike kwa lengo la kumsaidia..
 
Mi naamini Mh uenda anakutana na changamoto nyingi sana hapo, ukiangalia na haya ma miradi mikubwa ambayo mabepari hawataki tuifanye sharti watupe mikopo yao, Angalia ata ulinzi wake sasahivi the way ulivyo mkubwa nafikiri huko kuna zaidi ya majipu sasa wanaoguswa kwenye maslahi yao ni hatari pia.
 
Interest ,

..kuna sababu mbili zinazopelekea hali [mlundikano wa mambo yanayosubiri maamuzi ya Raisi] aliyoizungumzia JPM.

..mosi, Tz ina matatizo mengi mno.

..pili, Katiba ya Tz imempa Raisi madaraka makubwa mno.

..kwa maoni yangu, katiba irekebishwe ili kumpunguzia Raisi wetu mzigo asioustahili wa madaraka na majukumu.

..Sasa ni bahati mbaya kwamba JPM hataki tupate KATIBA BORA, wengine wanaita Katiba mpya.

Cc Nguruvi3 , tindo
 
Interest ,

..kuna sababu mbili zinazopelekea hali [mlundikano wa mambo yanayosubiri maamuzi ya Raisi] aliyoizungumzia JPM.

..mosi, Tz ina matatizo mengi mno.

..pili, Katiba ya Tz imempa Raisi madaraka makubwa mno.

..kwa maoni yangu, katiba irekebishwe ili kumpunguzia Raisi wetu mzigo asioustahili wa madaraka na majukumu.

..Sasa ni bahati mbaya kwamba JPM hataki tupate KATIBA BORA, wengine wanaita Katiba mpya.

Cc Nguruvi3 , tindo
JokaKuu,

Sababu mbili ulizozitoa nakubaliana nazo kwa asilimia zote. Hata maoni yako kuhusu Katiba Bora nayo si mabaya, lakini nina mtazamo tofauti kuhusu hilo..

Naona hitaji hili limekaa kisiasa zaidi ndio maana mvutano mkubwa upo baina ya vyama vya siasa; Tawala/Upinzani..

Upande wa chama tawala wanahofia wakiipitisha katiba inayopigiwa debe, watashindwa uchaguzi na upande pinzani unaamini ikipitishwa watapata dola. Yaani ni game of throne zaidi kuliko kutatua hizi changamoto. Ndio maana Magufuli anaona it's a waste of time and resources..

I may be wrong!
 
JokaKuu,

Sababu mbili ulizozitoa nakubaliana nazo kwa asilimia zote. Hata maoni yako kuhusu Katiba Bora nayo si mabaya, lakini nina mtazamo tofauti kuhusu hilo..

Naona hitaji hili limekaa kisiasa zaidi ndio maana mvutano mkubwa upo baina ya vyama vya siasa; Tawala/Upinzani..

Upande wa chama tawala wanahofia wakiipitisha katiba inayopigiwa debe, watashindwa uchaguzi na upande pinzani unaamini ikipitishwa watapata dola. Yaani ni game of throne zaidi kuliko kutatua hizi changamoto. Ndio maana Magufuli anaona it's a waste of time and resources..

I may be wrong!

..Uko sahihi.

..CCM hawapendi jambo lolote ambalo hawajalianzisha wao.

..sasa hoja ya Katiba bora ni hoja iliyoanzishwa na wapinzani.

..hata harakati za kutetea rasilimali ni suala lililoanzishwa na wapinzani na kinara wake akiwa Tundu Lissu na taasisi ya LEAT.

..Sasa JPM alipoanza kutetea rasilimali ilibidi hatua hizo ziende sambamba na juhudi za kumchafua TL na kuhakikisha anabatizwa utambulisho mpya wa "msaliti" na "adui wa taifa."

..Nikirudi kwenye mada yako, kinachotakiwa ni CCM kuwa na ajenda zao zinazowagusa wananchi ambazo watazipigania ziingie ktk Katiba Mpya.

..Wapinzani nao wawe na hoja zao wazipiganie nazo ziingie kwenye katiba mpya.

..Kila upande utakuwa umepata ushindi fulani. Kilichokwamisha kupatikana katiba bora ni kila upande kutokutaka maridhiano. Vilevile HOTUBA ya JK ilikwenda kuharibu majadiliano ambayo yangepelekea kupatikana katiba bora.
 
..Uko sahihi.

..CCM hawapendi jambo lolote ambalo hawajalianzisha wao.

..sasa hoja ya Katiba bora ni hoja iliyoanzishwa na wapinzani.

..hata harakati za kutetea rasilimali ni suala lililoanzishwa na wapinzani na kinara wake akiwa Tundu Lissu na taasisi ya LEAT.

..Sasa JPM alipoanza kutetea rasilimali ilibidi hatua hizo ziende sambamba na juhudi za kumchafua TL na kuhakikisha anabatizwa utambulisho mpya wa "msaliti" na "adui wa taifa."

..Nikirudi kwenye mada yako, kinachotakiwa ni CCM kuwa na ajenda zao zinazowagusa wananchi ambazo watazipigania ziingie ktk Katiba Mpya.

..Wapinzani nao wawe na hoja zao wazipiganie nazo ziingie kwenye katiba mpya.

..Kila upande utakuwa umepata ushindi fulani. Kilichokwamisha kupatikana katiba bora ni kila upande kutokutaka maridhiano. Vilevile HOTUBA ya JK ilikwenda kuharibu majadiliano ambayo yangepelekea kupatikana katiba bora.
Siongezi neno hapa mkuu. Umesema yote.
 
JokaKuu,

Sababu mbili ulizozitoa nakubaliana nazo kwa asilimia zote. Hata maoni yako kuhusu Katiba Bora nayo si mabaya, lakini nina mtazamo tofauti kuhusu hilo..

Naona hitaji hili limekaa kisiasa zaidi ndio maana mvutano mkubwa upo baina ya vyama vya siasa; Tawala/Upinzani..

Upande wa chama tawala wanahofia wakiipitisha katiba inayopigiwa debe, watashindwa uchaguzi na upande pinzani unaamini ikipitishwa watapata dola. Yaani ni game of throne zaidi kuliko kutatua hizi changamoto. Ndio maana Magufuli anaona it's a waste of time and resources..

I may be wrong!
It is worth having a new constitution kuliko kudhani haifai
 
View attachment 921223

Najua mnajua kuhusu suala la mafaili anayolala nayo kitandani. Maana ameshalirudia si chini ya mara moja.

Kwa tafsiri nyepesi kabisa, anachojaribu kuonesha ni kwamba yeye ni mfuatiliaji na sio mtu wa kuamini taarifa za kupewa kwa muhtasari. Anazama mwenyewe.

Tusijeshangaa siku moja, aidha kwa uchovu kwa kutaka tujue uzito wa maneno yake, ataalika waandishi wa habari Ikulu na kuwapeleka mpaka chumbani anapolala kisha aoneshe hayo mafaili.

Ni dhahiri, hicho ni kilio cha kuomba msaada (a cry for help) kutoka kwa kiongozi wetu. Je, anataka tumsaidiaje?

Nadharia nilizonazo;

1. Muda: Mafaili ni mengi maana yake mambo ni mengi ya kufanyia kazi hivyo yanahitaji muda mwingi ili yote yaweze kutekelezwa. So, tumuongeze muda wa kuyafanyia kazi. Miaka 10 inaweza isitoshe.

2. Uaminifu: Ofisi yake haimpi imani ya kutosha kuweza kusaidiana nae kuchakata masuala nyeti ya kitaifa, hivyo anahitaji kueleweka pale anapoamua kufanya maamuzi ya kuwabadilisha badilisha. Zipo tetesi pia kuna watumishi wanatoka kumfanyia figisu.

3. Pride: Huenda kwake ni fahari kuwaambia watz ni namna gani anafanya kazi usiku na mchana kiasi cha kujaza vitendea kazi mpk sehemu anayolala. Lengo ni kupata kukubalika!

Tumsaidieje?
Namba 3 ndio valid
 
Basi apunguziwe majukumu. I mean, delegation of power ifanyike kwa lengo la kumsaidia..
Wengine wakipewa power wanauza nchi. Wanafikiria kupata hela za kuhonga wakati wa uchaguzi....kama ule mzigo wa Dodoma 2015
 
Anaongea ukweli ndo maana unaona wengi waliohujumi nchi hii hawampendi maana anahakikisha kila kitu kinachopita kwake anakisoma na kukitolea maamuzi na kama ulimsikia mafaili yenyewe siyo ambayo utaweza kumpa mtu mwingine ayatolee maamuzi zaidi ya yeye tu kwa mujibu wa utaratibu na hapo inaonyesha kuwa Rais wa Tz ana kazi na majukumu mengi ya kufanya kama kweli sheria zinafuatwa.
Hahaha wewe muongo, unajibu kana kwamba wewe ni yeye.
Content za hayo mafaili kwako ni za ufisadi tu?! Hakuna mafaili ya vitu vingine, au nyie ndio waimba mapambio wake?!
Mafaili kayasema sana lakini hakusema yanahusu nini, na hiyo ndio theme ya uzi huu, lakini wewe umejibu kwa ujumla as if unayajua hayo mafaili, na unafunga mjadala.
Atuambie content za faili anazo lala nazo sio kila siku kutuambia tu analala na mafaili.
 
Back
Top Bottom