Ipi flat screen bora kati ya matoleo haya?

Agiza kutokea tunduma utapata kwa bei rahisi izo Brand kubwa mfano inch 43 Samsung utapata kwa 450K.
Mkuu mm naishi mwanza. Iyo biashara ya kupitia tunduma imekaaje. Nieleze kidogo nipate ufahamu, maana sipo vizuri kwenye huu uwanda wa kuagiza vitu kwa cost benefit analysis
 
Asante saaaana.
 
dstv ila hakina hiyo hdmi port
Nadhani nichazamani sana kwani vya sasa vinayo HDMI port.
chukua remote ya tv kuna option ya kuzoom nahisi inaeza kusaidia kutoa partition hiyo
 
Mwisho wa siku bajeti yako ndio itaamua ununue Tv ipi
Nikweli Tv za brand kubwa ni bora zaidi ya akinà TLC na Star X
Nilikua na LG nchi 32 ikafa ghafla na nilikua vibaya kiuchumi
Nikanunua Star X nchi 50 nikaining'iniza ukutani
Mwaka wa 3 huu nafurahia maisha kweli kweli
Dstv hd, Torrent nikishusha movies zangu na series za HD usiku ni burudani, sauti nimeunga kwa sabu ufa

Guyz ni kama mwenye Ranger Rover kumuona mwenye Rav 4 hafaidi maisha
Au mwenye iphone kumuona mtumia Tecno hafurahii smart phone
 
Ushauri wa bure ...
Msipende kununua Tv za kampuni zenye majina makubwa kama SONY, SAMSUNG au LG kwani asilimia kubwa ni copy na sio ORIGINAL .
Ni bora kununua tv ya kichina halisi kutoka kwenye kampuni husika kuliko kununua copy ya Kampuni kubwa . Mfano huwez kukuta copy ya Star-X au arboder au TCL.
Kwa ushauri pia ukitaka tv imara na hutojutia nunua TCL hizi ni tv imara sana na ninayangu inatumika 24 hrs mwaka wa pili sasa haimjui fundi licha ya misukosuko ya short ya umeme lakini bado ipo safi. Picha clear kabisa 1080 au 720 resolution safi kabisa . Nunua TCL mkuu
 
Kiukweli inategemea hizo brand kubwa unanunua sehem gan na umakini wako pia.....me ni mpenzi sana wa sony kuanzia tv had mziki.......nna sony bravia tv ni mwaka wa saba sasa haijawahi kuzingua zaid ya kubadili remote tu madogo wakipasua.......nikitaka kununua huwa naenda kwa agent kabisa wa sony garantee 2years
 
Kadude kako poa hatari na kana mkwara fulani hivi kwenye uwakaji wake proud of blackstone
watu hawaelewi wanakomalia LG na zaga nyingne,kumbe kuna hii kitu ambayo kwanza ni jiwe kama jina lake
 
Nilinunua mwaka 2015 32" nimekuja kuiuza mwaka huu mwanzoni ikiwa haina tatizo lolote.
Nampango nikachukue brand hiyo hiyo. Kwanza napenda muundo wao wa kuweka base (stand) katikati. Sipendi tv zenye miguu huku na huku kama masikio ya popo.
Vipi Blackstone tv inch 24 bei gani mkuu?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…