Interview never ends (Interview Haiishi)

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Huu ni ukweli ambo wengi bado hawajaujua, katika uhalisia wa mambo interview haiishi, huwa inaendelea hadi unapostaafu.


Interview ziko za namna kuu mbili ambazo walimu hawakuwahi kutufundisha.


Ipo direct interview na indirect interview.


Direct interview ni ile ambayo huwa in written or oral, ambayo muhusika husailiwa mbele ya panel ya watu kadhaa kabla ya kuchaguliwa kuwa mmoja kati ya wafanyakazi katika taasisi husika.


Indirect interview ni ile inayofanya bila kuwa na panel, huanza mara baada ya mkataba wa kazi kuanza.


Ubaya ni kwamba vijana wengi huwa wanadhani interview huisha mara baada ya wao kuitwa kazini baada ya kufaulu interview yao ya kwanza ambayo ni direct interview.


Mikataba mingi ya siku hizi ni ya muda maalumu ‘fixed term contracts’ kuanzia mwaka mmoja na kuendelea. Katika muda wa mkataba ndio muda ambao indirect interview inachukua nafasi yake.


Katika kipindi hiki ndipo muajiri hukuangalia vizuri kama kweli unafaa kuongezewa mkataba au la. Na kama mfanyakazi ataonekana kufeli indirect interview, basi wakuu wa taasisi huamua kumtoa hata kabla ya mkataba kuisha. Kama anavumilika huwa wanamuacha hadi muda wa mkataba kuisha kasha hawampi mkataba mwingine tena.


Hapa ndio kwenye kazi, kuna watu wamefanya kazi mashirika mengi tofauti tofauti na kupata experience tofauti tofauti, lakini hawajiulizi kwa nini taasisi walizofanya nazo kazi haziwaiti, au kuwaomba waongeze mkataba. Ukweli ni kwamba wamefeli indirect interview.


Zamani, interview kwa wafanyakazi wa serikali iliisha kwenye direct interview, ila kwa sasa kuna indirect interview hata huko na ndio sababu kwa wale wanaofeli hutumbuliwa.


WITO: Kwa wote mlioajiriwa, msidhani kuwa interview imeisha, endeleni kuwa na juhudi kama ulivyokuwa na ari na juhudi katika direct interview.

****** *******

Kwa makala zaidi tembelea African Awareness and Reality: INTERVIEW NEVER ENDS (Interview Haiishi)


Muandishi wa Makala haya ni mshauri wa masuala ya mahusiano na vijana.

Anapatikana kwa namba 0718651585 (Whatsapp)

Anakaribisha majadiliano.
 
Huu ni ukweli ambo wengi bado hawajaujua, katika uhalisia wa mambo interview haiishi, huwa inaendelea hadi unapostaafu.

Interview ziko za namna kuu mbili ambazo walimu hawakuwahi kutufundisha.

Ipo direct interview na indirect interview.

Direct interview ni ile ambayo huwa in written or oral, ambayo muhusika husailiwa mbele ya panel ya watu kadhaa kabla ya kuchaguliwa kuwa mmoja kati ya wafanyakazi katika taasisi husika.

Indirect interview ni ile inayofanya bila kuwa na panel, huanza mara baada ya mkataba wa kazi kuanza.

Ubaya ni kwamba vijana wengi huwa wanadhani interview huisha mara baada ya wao kuitwa kazini baada ya kufaulu interview yao ya kwanza ambayo ni direct interview.

Mikataba mingi ya siku hizi ni ya muda maalumu ‘fixed term contracts’ kuanzia mwaka mmoja na kuendelea. Katika muda wa mkataba ndio muda ambao indirect interview inachukua nafasi yake.

Katika kipindi hiki ndipo muajiri hukuangalia vizuri kama kweli unafaa kuongezewa mkataba au la. Na kama mfanyakazi ataonekana kufeli indirect interview, basi wakuu wa taasisi huamua kumtoa hata kabla ya mkataba kuisha. Kama anavumilika huwa wanamuacha hadi muda wa mkataba kuisha kasha hawampi mkataba mwingine tena.

Hapa ndio kwenye kazi, kuna watu wamefanya kazi mashirika mengi tofauti tofauti na kupata experience tofauti tofauti, lakini hawajiulizi kwa nini taasisi walizofanya nazo kazi haziwaiti, au kuwaomba waongeze mkataba. Ukweli ni kwamba wamefeli indirect interview.

Zamani, interview kwa wafanyakazi wa serikali iliisha kwenye direct interview, ila kwa sasa kuna indirect interview hata huko na ndio sababu kwa wale wanaofeli hutumbuliwa.

WITO: Kwa wote mlioajiriwa, msidhani kuwa interview imeisha, endeleni kuwa na juhudi kama ulivyokuwa na ari na juhudi katika direct interview.


Muandishi wa Makala haya ni mshauri wa masuala ya mahusiano na vijana.

Anapatikana kwa namba 0718651585 (Whatsapp)

Anakaribisha majadiliano.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom