Internet ya tiGO Kimeo

Uncle Rukus

JF-Expert Member
Jun 16, 2010
2,415
398
Mimi ni mtumiaji mzuri wa huduma za tigo hasa huduma ya internet , nimekuwa mtumiaji wa package ya standard month tsh 40,000/- (kabla hawajabadilsha bei )kwa takribani miezi 8 hivi hadi walipo badilisha mashart na kutoa 4gb only, nikahamia max month kutokana na matumizi yangu kuwa juu nikaona hii ndio package inayonifaa kwa matumizi yangu.


Nimetumia package hii ya max month tsh 100,000 (15 gb )kwa miezi 4 hivi, toka wiki iliyopita speed yake imekuwa ndogo sana na uwezi kufanya chochote cha maana na hata kwa siku ukiacha computer on uku ukidownload uwezi maliza kudownload file la 700mb , ukiangalia gharama ya hii package na huduma tunayopewa haviendani kabisa huu ni wizi kabisa sijui TCRA wanafanya kitu gani wakati wananchi tunaibiwa mchana kweupe na haya majambazi ya huduma za mitandao.

Ukiwasiliana na huduma kwa wateja kitengo cha data hawana majibu ya kueleweka na hawana msaada wowote zaidi ya kukuambia "chomoa modem na uchomeke tena"

Je kuna wadau wengine mmekutana ka na tatizo ili ya kushuka kwa speed ya mtandao wa tigo?
 
Ndio maana nimekuwa nikisema, kwa matumizi makubwa ya internet hapa bongo, bado tuna safari ndefu.
Hakuna mtandao nafuu na wenye uhakika. Mkuu, kwa kuwa tayari wameishakata hela yako, no way out.
 
Tigo ndio mobile internet provider ambaye anatoa huduma zake kwa gharama nafuu zaidi kuliko hao wengine, ila kwa style hii bora niachane nao tu kwa sasa hadi watakapo jirekebisha
 
mitandao yote huwa kuna muda ipo fresh sikuzingine hovyo kbsa, ila unlimited ya voda bomba30 sio mbaya sana..
 
Mimi ni mtumiaji mzuri wa huduma za tigo hasa huduma ya internet , nimekuwa mtumiaji wa package ya standard month tsh 40,000/- (kabla hawajabadilsha bei )kwa takribani miezi 8 hivi hadi walipo badilisha mashart na kutoa 4gb only, nikahamia max month kutokana na matumizi yangu kuwa juu nikaona hii ndio package inayonifaa kwa matumizi yangu.


Nimetumia package hii ya max month tsh 100,000 (15 gb )kwa miezi 4 hivi, toka wiki iliyopita speed yake imekuwa ndogo sana na uwezi kufanya chochote cha maana na hata kwa siku ukiacha computer on uku ukidownload uwezi maliza kudownload file la 700mb , ukiangalia gharama ya hii package na huduma tunayopewa haviendani kabisa huu ni wizi kabisa sijui TCRA wanafanya kitu gani wakati wananchi tunaibiwa mchana kweupe na haya majambazi ya huduma za mitandao.

Ukiwasiliana na huduma kwa wateja kitengo cha data hawana majibu ya kueleweka na hawana msaada wowote zaidi ya kukuambia "chomoa modem na uchomeke tena"

Je kuna wadau wengine mmekutana ka na tatizo ili ya kushuka kwa speed ya mtandao wa tigo?

Ni kweli mkuu unachosema, speed yao imepungua tofauti na ilivyokuwa awali. Tatizo la nchi yetu hakuna utawala wa sheria, hii ni dhuluma tena iliyowazi kabisa. Yaani bado safari ni ndefu, huduma ya internet kwa karne hii sio anasa bali ni hitaji muhimu kwa kila mwananchi. Kwakweli kuna haja ya kupambana na huu ujambazi wa mawasiliano kwa kila njia ikiwa ni pamoja na kutoa malalamiko yetu kwa wahusika hata kama watayapuuzia lakini ujumbe uwafikie waelewe kwamba we know our rights.
 
Yaani hata mimi mbona najuta speed kimeo download speed inafika 5kbps ndo imejitahidi yaani bongo mbona shida kibao
 
Back
Top Bottom