Ingekuwa wewe Ungefanyaje?

Ingekuwa wewe Ungefanyaje?

Smart Finance

Member
Joined
Apr 10, 2025
Posts
35
Reaction score
112
Mfano umetuma kimakosa shilingi 500,000 kwenye akaunti isiyo sahihi, ukampigia simu uliyemtumia Ili akurejeshee mpokeaji simu akasema atakata 100,000 na akurudishie 400,000

Kwa huzuni kubwa ukakubaliana naye atume hiyo hiyo maana huna namna nyengine. Una shida zako unahitaji kufanya muamala huo haraka iwezekanavyo.

Lakini kwa bahati mbaya na yeye akakosea na kukutumia 4,000,000 badala ya 400,000 kama alivyosema.

UTAFANYAJE?
 
Mrushie pesa yake kamili auone ubinadamu wako.. Utakuwa umefanya jumbo jema sana
 
Kuoneshaa kuwa uko smart zaidi yake unamrudishia tu 3,500,000

Au kama we ni tapeli kama yeye basi na wewe unakata 100,000 kama yeye unamrusishia nyingine
 
Mfano umetuma kimakosa shilingi 500,000 kwenye akaunti isiyo sahihi, ukampigia simu uliyemtumia Ili akurejeshee mpokeaji simu akasema atakata 100,000 na akurudishie 400,000

Kwa huzuni kubwa ukakubaliana naye atume hiyo hiyo maana huna namna nyengine. Una shida zako unahitaji kufanya muamala huo haraka iwezekanavyo.

Lakini kwa bahati mbaya na yeye akakosea na kukutumia 4,000,000 badala ya 400,000 kama alivyosema.

UTAFANYAJE?


Follow the Smart Finance - SW channel on WhatsApp: Smart Finance - SW | WhatsApp Channel
Ubaya ubwela!Ningemrudishia m3
 
Unakata 1m, unarudisha 3m.
Ubaya ubwelaa, km mbwai na iwe mbwai.
😂😂😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom