Inawezekana mkuu wa kaya anashaurika

Inawezekana mkuu wa kaya anashaurika

Joined
Apr 6, 2015
Posts
36
Reaction score
15
Nimewahi kusikia kutoka kwa watu wangu wa karibu, ndugu na jamaaa waliowahi kufanya kazi ama wanaofanya kazi kwa wahindi hadi hivi sasa kuwa, kama mfanyakazi ukionekana una mawazo chanya, mwenye akili nyingi, mjanja na mvumbuzi wa mambo kiasi ambacho unaweza kumshauri bosi nini mfanye kwa ajili ya maendeleo ya kampuni basi unaweza kuishia kufukuzwa kazi kwani jamaa hao (yani wahindi) huwa wanahisi kuwa kwa akili nyingi ulizonazo huenda ukawa unawapiga kiaina bila wao kujua. Kwahiyo ili kuendelea kufanya kazi kwenye taasisi zao ni bora kujifanya mjinga tu au zoba ili kulinda ajira yako.

Sasa kwenye kaya yetu, watu wengi wanasema mkuu wetu hashauriki hata kidogo. Wazo likanijia, huenda anashaurika na washauri wapo wengi wenye akili nyingi tu na mawazo ambayo yataisongesha mbele kaya yetu sema wanaogopa kutoa huo ushauri na kuamua kukaa kimya ili waendelee kupata chochote kitu kwa ajili ya mkono kwenda kinywani maana utumbuaji umekuwa wa hali ya juu. Hii inapelekea mkuu kuwa 'One man army' na kufanya maamuzi mengi makubwa kama ambavyo akili yake inamtuma bila kuhojiwa ama kushauriwa na yoyote yule.

Karibuni wadau tujadili.
 
Hata mwalimu aliwahofu wenye akili nyingi, wengi walipangiwa kazi baada ya f4, wabovu ndo walipewa ufadhili wa elimu ya juu ndo maana maprof wengi vilaiza wasio na tija
 
nikweli aiseee bora kulinda mlo tuu siku ziende
 
Ukisoma filosofia ya ualimu kuna kitu kinaitwa haiba au kwa kiingereza personality
-kuna watu wenye haiba ya kudhani kuwa wao ndio wanajua wao ndio wako sahihi kuliko wengine -superiority complex
-kuna watu wana haiba ya kudhani kuwa wao hawawezi wala hawajui , hili ni kundi la watu waliojijaza defencensive mechanism. ni watu wanaodhani kuwa matatizo yao yamesababishwa na wengine. ..hawa ni inferiority complex
-kuna watu wana haiba ya maridhiano, na kufanya kazi kama timu.. kushare maarifa hawa wanaamini katika umoja na mgawanyo wa madaraka. .Nyerere alikuwa mmojawapo
-kuna watu wana haiba ya kusikiliza wengine zaidi kukubali ushauri wao kwakuwa tu ni watu wake...watu wabaya huwapotosha sana watu wenye haiba hii....Kikwete alikuwa na hili tatizo
Magufuli ni mtendaji anayeamini katika ubora na viwango, muumini wa kufanya kama ilivyo ama inavyotakiwa...kwa hali nchi ilipokuwa imefika, palihitajika mtu wa haiba na kaliba yake LAKINI ilipaswa ama la ilitakiwa aundiwe baraza au kamati yenye nguvu kisheria kumsaidia katika mipango maamuzi na utendaji, ili pamoja na kuwa na nia njema kabisa ya yale ayafanyayo lakini mwisho wa siku asiache majeraha ya uonevu ukatili mgawanyiko kwa wananchi wa kawaida na hata kwenye maisha ya kisiasa na hata wale wasiokubaliana naye
Ni vigumu mno na ni kitu kisichowezekana kabisa upendwe na wote au uchukiwe na wote
 
Wanaweza kuwa na uwezo mdogo pia maana hili tumeliona hata kutoka kwa mawakili wa Jamuhr.

Unachosema pia kinaweza kuwa kweli ukijaribu kuangalia teuz za ma DC na wakurugenz. Uwezo wao mdogo sana
 
Back
Top Bottom