Inakuaje Kila ukimfadhili mtu mwisho wa siku lazima akulipe baya

pureman2

JF-Expert Member
Aug 21, 2019
1,494
2,538
Inashangaza lakini ndo ukweli wa maisha. "Ujapo wema , maumivu yafuata".

Ndugu Yako anafariki, unaamua kuwachukua wanae uishi nao na kuwasaidia kuendelea na masomo ila mwisho wa siku watoto wataanza kutoa shutuma, baba mdogo /mjomba / shangazi wanatubagua na kutunyanyasa. Mgogoro wa kifamilia hutokea.

Unakutana na watu kwenye maisha wanapitia changamoto za maisha , mambo Yao hayaendi , kila wanaowajua wamewapa mgongo. Unasema isiwe taabu unaamua kuruhusu waishi kwako ili watulize akili na kujitafuta. Baada ya kuzoea wanakupiga tukio , eidha wanabaka wanao, au wanakuibia na kutoroka. Wema wako unageuzwa maumivu.

Wakati mwingine unajitoa sadaka ya kuteketezwa Kwa mpenzi. Unaghalamia pesa, vitu, na muda wako. Unawekeza hisia as if ndo umetumwa na mbingu kuja kumtunza mtoto wa mamamkwe. Umejisahau kidogo unapigwa tukio hadi ukiwaza njaa usikiii na usingizi hauji na afya inazoofu.

Wakuu ebu tieni neno kwenye huu Uzi kuonyesha uzoefu wenu. Biblia yenyewe mahala flani imeandika Kwa sababu ya maovu kuongezeka upendo wa wengi utapoa.
 
Ungetoa tukio kwako kabisa lasivyo hiyo inabaki hearsay stori za wale wachoyo wasio taka kusaidia au wanao saidia kwa kusimanga.
 
Wakati mwingine unajitoa sadaka ya kuteketezwa Kwa mpenzi. Unaghalamia pesa, vitu, na muda wako. Unawekeza hisia as if ndo umetumwa na mbingu kuja kumtunza mtoto wa mamamkwe. Umejisahau kidogo unapigwa tukio hadi ukiwaza njaa usikiii na usingizi hauji na afya inazoofu
Binafamu wengi sio woote utawaonea huruma wakiwa na shida tu wanajiliza.

Lakini wana roho mbaya sana.

Mungu aniepushe Kaka aliyenisomesha nadhani bado nina tight love naye sana.

Nashukuru woote walionisapoti hata kama sijawapa Kitu au Mali lakini nawaheshimu na kuenda nao vizuri
 
Fanya kwa nafasi yako sawa people are dynamic uwezi pata maana halisi ya pipo
 
Inashangaza lakini ndo ukweli wa maisha. "Ujapo wema , maumivu yafuata".

Ndugu Yako anafariki, unaamua kuwachukua wanae uishi nao na kuwasaidia kuendelea na masomo ila mwisho wa siku watoto wataanza kutoa shutuma...
Huu uzi unasikitisha sana.
 
Inashangaza lakini ndo ukweli wa maisha. "Ujapo wema , maumivu yafuata".

Ndugu Yako anafariki, unaamua kuwachukua wanae uishi nao na kuwasaidia kuendelea na masomo ila mwisho wa siku watoto wataanza kutoa shutuma...
Kwa sababu unatoa fashila ukitegemea Jema, Tenda wema nenda zako vinginevyo acha kufadhili.

Utalipwa nini na nani sio kazi yako
 
Mkuu wasikukatishe tamaa..binadamu anatamani usawa ambao hata huwezi kumpa..ngumu ukanihudumia mimi sawa na mwanao..kile unachowiwa wape...kwingine kubali lawama
Lawama zisizo na msingi zinaumiza
 
Ungetoa tukio kwako kabisa lasivyo hiyo inabaki hearsay stori za wale wachoyo wasio taka kusaidia au wanao saidia kwa kusimanga.
Nikiandika itakua marudio , summary ya maumivu nimeiweka kwenye uzi huu
 
Binafamu wengi sio woote utawaonea huruma wakiwa na shida tu wanajiliza.

Lakini wana roho mbaya sana.

Mungu aniepushe Kaka aliyenisomesha nadhani bado nina tight love naye sana.

Nashukuru woote walionisapoti hata kama sijawapa Kitu au Mali lakini nawaheshimu na kuenda nao vizuri
Ni kweli, machozi ya wengi ni unafiki. Afu hili jambo la kumsaidia Kila mwenye shida ni kutaka kupunguzia adhabu watu pengine wanazipitia kutoka na mabalaa yao
 
Inashangaza lakini ndo ukweli wa maisha. "Ujapo wema , maumivu yafuata".

Ndugu Yako anafariki, unaamua kuwachukua wanae uishi nao na kuwasaidia kuendelea na masomo ila mwisho wa siku watoto wataanza kutoa shutuma...
you need to lower your expectation's
 
18a97bab7607ae1e8df9affdd4321a28.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom