Imeniuma sanaa!

Umenena vema, inakukwaza wewe, haiwakwazi wao.

Unaweza kuwa unakwazika na mtu kubeba mimba kabla ya ndoa. Lakini uarabuni wanakwazika na binti tu kupoteza ubikra wake. Jipime hapo.

Na njia anayopitia kila mmoja hadi kufikia ndoa ni tofauti na mwenzake, but mwisho wa siku ni kujaribu 'to be a better person' kila siku.

Ukiona askari mwenzako kaanguka, humkanyagi kichwa, mshike mkono, kama huwezi mwombee tu inatosha.

am sorry to say this but hii tabia ya wasichana kukimbilia kubeba mimba sikuhizi kabla ya ndoa inanikwaza sana
 
Pole sana hiyo changamoto ktk mahusiano nakushauri usitoe hiyo mimba lea huyo mtoto ;wewe sio wakwanza kupitia hali hiyo vumilia utavuka tu ktk pito hilo na huyo mtoto atakuwa baraka kwako na wengine tuliza moyo wanaume wengine ndivyo walivyo pole sana
 
kwa vile ww Mungu kakuepusha usifikir ndio ulikuwa makin sana ila hukubahatika kukutana na wakwale. Na acha hyo kauli ungekuwa single ningekutafuta kwa gharama yoyote ili nikuthibitishie kuwa huna ujanja ila hukubahatika kukutana nao

Una uhakika na unachokisema?
 
Usiitoe hiyo mimba mwenzio yalinikuta kama yako mwanzo niliwaza sana but now am happy to be a mother nilianza kuuza barafu na ice cream zikanibeba mpaka sasa na duka kubwa mwanangu namlea anamiaka 3 sasa baba mtu anahahaha hana hata mtoto hdi leo
 

Usithubutu kutoa mimba aisee, heri dhambi moja kuliko mbili, Muwe na reservation ya mapenzi, kufikiri kuwa mtu anakupenda kama unavyompenda wewe ni kujidanganya.
 
na ww bhana!! mbona ukampekea siku mbaya.
 
Usithubutu kutoa mimba aisee, heri dhambi moja kuliko mbili, Muwe na reservation ya mapenzi, kufikiri kuwa mtu anakupenda kama unavyompenda wewe ni kujidanganya.

Baba V@ ntakuja pm. cc watu8@ kaka yangu
 
Last edited by a moderator:
Bana watu tuache uzembe na visingizio.


Kosa na kwanza kwenda peku na mtu asiyejua msimamo wake juu yake
Kosa la pili, kupanda bangi na kutegemea uote mchicha

Sasa suala la mimba kuingia, afu mtu anataka tushauri kutoa hapana, hapa inahusisha maisha ya mtu mwingine.

Na hadi kufika chuo kikuu walau ana miaka 18+, na uzoefu alioupata huko duniani unamtosha kabisa kulea. Na akitaka asijipasue kichwa ashirikishe nduguze, mimba sio laana na si ugonjwa. Vipi angekuwa na ngwengwe?

kumbuka tunatofautina, pia hatujui mazingira aliyonayo huyu dada!
 
Kulea tu wala usijali...nafahamu haya mambo vizuri..mie ningekuwa wewe ningeamka na akili za saa nane usiku..mimba sitoi na mwanaume namuacha.. Kisha namwambia kabisa mimba nimetoa na ndo mwisho wetu..(kama hamuonani onani)...kisha nazaa nalea ...
Kufanya hivyo ili kuepuka usumbufu...maanina manake kuna mijianaume mingine kulea mimba haitaki mtoto akikua ndo anaanza nina mwanangu mahali fulani....aisee jikaze tu maisha wala siyo magumu kama ulivyojijengea akilini...
 
Nimekupenda buree..
Usiitoe hiyo mimba mwenzio yalinikuta kama yako mwanzo niliwaza sana but now am happy to be a mother nilianza kuuza barafu na ice cream zikanibeba mpaka sasa na duka kubwa mwanangu namlea anamiaka 3 sasa baba mtu anahahaha hana hata mtoto hdi leo
 
 
Huyo mwanamme, kama ningekuwa mie, ningetimka asilani. Kama mwanamme anakubali kushiriki mapenzi bila kondomu, na hata kama alivaa kondomu ikapasuka, basi ajue anawajibika moja kwa moja. Asiyetaka mimba hafanyi mapenzi.

Na hii dhana ya kuwa mwanamke ndio ajikinge tu na mimba is for weak men, wanamme wa kweli wanawajibika na wao kuwakinga wenza wao wasipate ujauzito, inapotokea hutafuta suluhisho la pamoja. Hakuna mtoto abayezaliwa na jinsia moja, kwa hiyo hakuna jinsi ambavyo jinsia moja ione haiwajibiki au imechezewa trick, lame excuse.

Mwanamme anayeshindwa kuchukua wajibu wa mimba aliyoshiriki kuipata alizaliwa kimakosa, hiyo sperm ilipotea kabisa, bora ingeenda zalisha mhogo watu tukala kripsi tu, tena na pilipili ya unga.

 
usitoe mimba, hakuna litakaalo kushinda.....maisha yanaendelea..muombe Mungu akupe wepesi ktk hilo..pole mwaya ila liwe fundisho usimuamini mwanaume kiasi hicho
 
Men!!!!
Ni vizuri umejua aina ya mtu uliyekuwa nae na kumuamini ni mtu wa namna gani hasa,pole kwa sababu ungetamani kuyajua haya mapema.
Usithubutu kutoa hiyo mimba,lea mamy na uje ulee mwanao kwa mapenzi yote.
Wapo watoto wengi wanalelewa na mzazi mmoja kwa sababu zozote zile na wanakua tu,hata wako atakua.
Go and talk to your mama,hata akichukia mwanzoni hawezi kuchukia milele.
Good luck.
 

asantee.....
 
Kwa nini kajiharibia maisha? Kivipi?

Kuna watu wanaolewa, wanazaa watoto hata watano, wnaachana vile vile, nao wamejiharibia maisha?

Bora huyu bado mdogo, ana muda wa kurekebisha makosa, mtoto sio 'salala'. Kuna wanawake wangapi wamesoma huku wameshazaa, tena wengine sekondari kabisaa. Hakuna jambo lisilo na suluhu, na maisha ni changamoto tu, Kikubwa ni kukubali kurekebbishika. Sio tena kesho arudi na mimba ya mwingine wakati kichanga hata bado hakijatambaa.

 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…