Imekaaje hii, hotelini mzungu kampa paka samaki mkubwa

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Wazungu wana mambo ya ajabu sana, wacha nikupe mkasa nilioshuhudia leo

Mida ya lunch leo kuna rafiki yangu kazini katutoa lunch rafiki zake twende hotelini kupiga msosi.

wakati tunapiga msosi maeneo ya wazi nyuma ya hoteli, tukawa tunamshangaa mzungu flani yupo na paka wa pale hotelini wanacheza, mzungu alikuwa anampapasa manyoya huyo paka, tulishangaa maana paka yule alikuwa wahapo hotelini hata sijui kama anasafishwaga

Sasa kumbe mda huo nadhani alikuwa kaweka order ya samaki wa kukaanga\

tukamona waiter anamplelekea samaki mbili kubwa kiasi, tukataniana mzungu ana njaa kali.

LA HAULA!!! Samaki moja aliwekwa chini kwenye kimfunikocha ndoo paka akaanza kufaidi samaki kimasihara.

Haikutosha hivyo lakini paka anapoendelea kupata hio lishe adim, mzungu alikuwa bado anamkuna kuna kichwani guju paka akiendelea kumfanyia samaki umafia

Kwa hali hii hawa wenzetu unaweza kumtoa out na kugharamia msosi wa gharama ukaishia kumuhudumia paka

Nadhani ni muda sasa sheria ziweke wazi kuna binadamu kupata mlo mmoja tu ni kazi, yafaa angenunulia hata watu wenye shida huyo samaki kuliko kumpa paka
 
Mimi mwenyewe huwa namkaangia hadi mayai plus kumnunulia samaki watu wakija wanashangaa utazini paka hastahili kula vitu vizuri afu wanaume wanaopenda wanyama huwa wana mapenzi ya dhati kwa wake zao au wapenzi
 
Back
Top Bottom