Pinokyo Jujuman
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 552
- 104
Maelezo yako hayana mafao kwa sababu unajaribu kuwagawa viongozi wa ngazi za juu wa ccm katika makundi mawili yaani waliosafi na mafisadi. Lakini ki ukweli ni kwamba hakuna aliye safi wote wako kundi moja, hapa unajaribu tu kumtetea mmoja wao dhidi ya mwingine, kwa kutoa mfano, jiulize lowasa fisadi na jk je? kuna ufisadi wa aina nyingi kama wa raslimali, utumiaji mbaya wa madaraka, kuigawa jamii kiitikadi nk nk. Ukiunganisha aina zote za ufisadi jk ni mfisadi hatari kuliko el
source ya habari yangu ni mtu aliyekaribu sana na lowassa.
Lowassa amejiwekea option tatu, moja kubaki ccm kama hawatamwekea vikwazo vya kugombea urais, pili amuunge mkono mtu wake ndani ya ccm na ikitokea mtu wake amekosa ataenda chadema. Mazungumzo ya awali yalishafanyika na chadema kwamba itakuwa rahisi sana kumsafisha. Hoja kubwa ni kwamba tatizo la ufisadi si la mtu binafsi bali la mfumo uliojengwa na ccm, kwamba unaweza ukawa na wana ccm wabovu wakaja chadema wakawa wasafi kwani mfumo utakaojengwa na chadema hauruhusu ufisadi. Na nadhani hiyo ndio hoja si kwamba wana chadema ni malaika, hata kidogo. Watakachofanya ni kujenga mfumo mpya na taasisis huru zenye nguvu kupambana na rushwa. Akiwa ndani ya chadema lowassa hatakuwa kiongozi bali mtu wa kawaida ila anahitaji zaidi ulinzi azibughudhiwe maana anahofia wakiingia kina sitta watamsumbua sana.
Sasa mkakati mkubwa wa lowassa kwa sasa ni kuisaidia chadema indirectly ili izidi kuimarika na kuwa tisho la kweli kwa cm. Lengo ni nini? Inasemekana lengo ni kuwa ccm ikiwa imewekwa kitanzini hawatamudu kuruhusu mgawanyiko ndani ya chama hasa kuwaondoa wale wanaoonekana kama mafisadi. Itabidi waruhusu tu yule atakayeshinda kura za maoni ipite bila mizengwe ili chama kibaki kimoja. Lakini swali ni je, kama lowassa akipata tiketi ya ccm atawarudisha vipi wale ambao tayari wameshahamia chadema na kuijenga vilivyo? Wengine watasema kirahisi kuwa ni uzushi ila kama upo karibu na viongozi wakuu wa chadema au marafiki wa lowassa watakuambia kwa sasa lowassa yupo karibu sana na chadema na kuna agenda nzito ndani yake. Siku njema
Lowasa akija CDM basi huo ndio utakuwa mwanzo mpya wa wananchi kuondoa imani na chama chochote cha siasa kwani lowasa ni fisadi sugu sasa how comes na yy aje tuungane? Ktk hili viongozi wa juu wa CDM wanatakiwa kujihadhari sana kwani CDM hatuna tena haja ya ushawishi wowote kutoka nje kwani tunajitosheleza kila idara so haitakuwa vyema tena hao mafisadi kuja ku-teplace tena nafasi huku CDM.
Imekaa kiudaku zaidi!
Source?
lowassa ni ccm for life yule....he bleeds CCM...haendi popote...atakufa nayo!!
source ya habari yangu ni mtu aliyekaribu sana na lowassa.
Lowassa amejiwekea option tatu, moja kubaki ccm kama hawatamwekea vikwazo vya kugombea urais, pili amuunge mkono mtu wake ndani ya ccm na ikitokea mtu wake amekosa ataenda chadema. Mazungumzo ya awali yalishafanyika na chadema kwamba itakuwa rahisi sana kumsafisha. Hoja kubwa ni kwamba tatizo la ufisadi si la mtu binafsi bali la mfumo uliojengwa na ccm, kwamba unaweza ukawa na wana ccm wabovu wakaja chadema wakawa wasafi kwani mfumo utakaojengwa na chadema hauruhusu ufisadi. Na nadhani hiyo ndio hoja si kwamba wana chadema ni malaika, hata kidogo. Watakachofanya ni kujenga mfumo mpya na taasisis huru zenye nguvu kupambana na rushwa. Akiwa ndani ya chadema lowassa hatakuwa kiongozi bali mtu wa kawaida ila anahitaji zaidi ulinzi azibughudhiwe maana anahofia wakiingia kina sitta watamsumbua sana.
Sasa mkakati mkubwa wa lowassa kwa sasa ni kuisaidia chadema indirectly ili izidi kuimarika na kuwa tisho la kweli kwa cm. Lengo ni nini? Inasemekana lengo ni kuwa ccm ikiwa imewekwa kitanzini hawatamudu kuruhusu mgawanyiko ndani ya chama hasa kuwaondoa wale wanaoonekana kama mafisadi. Itabidi waruhusu tu yule atakayeshinda kura za maoni ipite bila mizengwe ili chama kibaki kimoja. Lakini swali ni je, kama lowassa akipata tiketi ya ccm atawarudisha vipi wale ambao tayari wameshahamia chadema na kuijenga vilivyo? Wengine watasema kirahisi kuwa ni uzushi ila kama upo karibu na viongozi wakuu wa chadema au marafiki wa lowassa watakuambia kwa sasa lowassa yupo karibu sana na chadema na kuna agenda nzito ndani yake. Siku njema
jamaa anataka uraisi kwa nguvu sijui ana nia ya kutatua matatizo yetu au nia ya kupata mali zaidi??
Bila kujali hii habari ni ya kweli au la, hebu wana JF tuonyeshe tunatumia akili zetu kufikiri na sio mbumbumbu wala bendera fuata upepo na tuondokane hii tabia ya kikasuku ya kukimbilia ku-type neno ''source?'' kila habari inapoletwa hapa. Au kwa vile ni neno la kiingereza hatujui lina maana gani? Nadhani wengi wetu tunapodai source ya habari hata hatujui tunadai nini.Imekaa kiudaku zaidi!
Source?