Imani zilizokosa ithibati

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
299,611
752,018
Tamaduni mila desturi na imani ni vitu vya kushangaza mno...ni sawa na kuumba roho ambazo hazipo na kuzifanya ziwe live ziishi na kuathiri maisha yetu kwa njia moja au nyingine
Tukianza na wazungu wenzetu hawa wana shida na namba 13 nakumbuka marehemu Michael Jackson aliwahi kufanya kila liwezekanalo mwanae asizaliwe tar 13 kwakuwa si siku nzuri
Kule china kuna namba nne! Kiasili hii si namba nzuri kwakuwa kwenye matamshi kuna tofauti ndogo sana ya kifo na nne.hivyo basi kwa china ya zamani ilikuwa ni jambo la kawaida kukosa ghorofa ya nne
Lakini ni hawa hawa wachina ambao kwao kutembelewa na bundi ni bahati kubwa sana
Ukija kwetu Africa ni balaa kubwa kumuona bundi karibu na nyumbani kwako au hata kusikia sauti yake
Nimetoa mifano hiyo michache ukiacha ile ya wahindi kuabudu ng'ombe na ukimpa mhindu nyama ya ng'ombe anaweza kufa kwakuwa ni kama amemla mungu wake...hii ni imani na imani huumba roho
Cha kujiuliza inakuwaje bundi huyo huyo awe ni baraka kwa wengine na nuksi kwa wengine?
Iweje namba fulani iwe ni mikosi kwa wengine na kwa wengine isiwe na madhara yoyote? ?
Dunia ina mengi ya kujifunza!hata kama huamini kwa dhati ya moyo kabisa kuwa kitu fulani hakipo lakini ukiishi na jamii husika inayoamini uwepo wake..kitu hicho chaweza kukuathiri kwa namna yake
Tujifunze kutomdharau mtu au kitu kuna mengi tusiyoyajua bado na imani huumba na kinachoumbwa ni roho yenye nguvu mno...mtu akikwambia hakuna Mungu mwambie hewala bwana....! Mtu akikwambia hakuna uchawi mwambie tawile...!unajua ni kwa nini? ?? Usibishane naye....amezingwa na nira za ufahamu finyu ...huwezi kwa hakika kumwambia mtu Ladha ya halua kama hajawahi kuila.....!!!!!bali wewe jifunze ili upate ufahamu
b6c0f428067d85305b21fc7f0b709acf.jpg
 
Mungu yupo kw kila mmoja na ndio maana ukienda kw mganga na akakupa dawa ata kwmbia n kw uwezo wa Mungu na kupitia yeye ataweza kufanikisha ata wez na wachawi wanaamin uwepo wa Mungu, ila ukiwaambia KWA JINA LA YESU uwa inakuw n shida kwao maana hapo inakuw n falme mbili tofaut.. kwhyo Mungu yupo na dini n iman ya kile mtu anacho kiamin.
 
Ni kweli kabisa...Nakumbuka kuna mtoto wa ndugu yangu aliugua sana na ugonjwa ulikuwa hauonekani kisa tu alijifanya amesoma mno akagoma kupeleka mtoto kwa babu na bibi ake....Alivyoona mtoto atakufa akampeleka kwa nyumbani ile mtoto kushikwa na bibi na babu ake matatizo yote kwishaa...
 
Ni kweli kabisa...Nakumbuka kuna mtoto wa ndugu yangu aliugua sana na ugonjwa ulikuwa hauonekani kisa tu alijifanya amesoma mno akagoma kupeleka mtoto kwa babu na bibi ake....Alivyoona mtoto atakufa akampeleka kwa nyumbani ile mtoto kushikwa na bibi na babu ake matatizo yote kwishaa...
Huyu alikuwa na maagano na hao wazee... Kujifanya mjuaji Hakuna kitakachifanyika ufanikiwe hadi urudi kwao
 
ndugi mshana ulipotea !!sasa naomba utoe ufafanuzi kuhusu hyo maagani yanakuaje kuaje adi yanamrudia mtoto!!
Zamani mtoto akizaliwa alikuwa anafanyiwa mambo ya kimila haya mambo ya kimila ndio maagano yenyewe ambayo mtoto huishi nayo mpaka anapokuja kuyavunja
 
Zamani mtoto akizaliwa alikuwa anafanyiwa mambo ya kimila haya mambo ya kimila ndio maagano yenyewe ambayo mtoto huishi nayo mpaka anapokuja kuyavunja
so mambo ya kimila yanawez kumuathiri mtoto kama alifanyiwa!!so inatakiwa aendelee kufanyiwa kila mda au ?na je mambo ya kimila nay ni ushirikina?
 
Back
Top Bottom