Ilibaki kidogo tu nafsi iuache mwili

Ilibaki kidogo tu nafsi iuache mwili

Dah! Washakufa washikaji wengi kwa tamaa za wanawake kutuchanganya.
Sehemu niliyopo kwa sasa kuna mama akiwaona watu kutoka mtaa fulani anamwaga mvua ya matusi na anawatupia mawe hao watu.Wenyeji wanadai watu wa mtaa huo walimuua mwanae kwa "case" kama hii,kwa nini unamkana mtu?na anafanyiwa vurugu umetulia tuu.Kuna watu wana roho kubwaa.
 
pole sanw mkuu.naona majeraha bado yako moyoni...pole saaaaana
 
pole sanw mkuu.naona majeraha bado yako moyoni...pole saaaaana
Asante sana mkuu,kufika maskani nako ndugu na jamaa wakazungumza vitu vya ajabu sana.
 
Kesi kama yako iliwahi kutokea kwa jamaa mmoja tukiwa Chuo! Jamaa alikuwa na gf wake chuoni, cku moja jamaa kamkuta binti na njemba nyingine room! Yule binti kajifanya hamjui Msela na akaanza kumpigia kelele za mwizi! Jamaa alipigwa xana akaenda kufia hospital baada ya kuokolewa na rais wa Chuo! Inasikitisha Sana hii hali!
 
Hahahaaa...Mkuu hatukucheki ila kuna vitukio vilivyoelezewa (kama kujidai kufa halafu unasikia sauti ya tumchome moto) vinafurahisha, hasa msomaji anapoivuta hisia ya ubonge wako na umeshachezea kichapo kiasi kwamba kufumuka mbio linakuwa ni jambo lisilochagulika! POLE SANA
 
Umenikumbusha mbali sana. ...iliwahi nitokea, ...nilimkuta demu wangu yupo na jamaa wameshiba sana wanakunywa bia maeneo ya jirani na kambi moja ya polisi, kipindi hicho mi nna mwili mwembamba lakini nnajiamini balaa hehehe (changanya na mapenzi), basi nilivyomwona nikasogea mpk pale kisha nikamwomba niongee nae, mshkaji mmoja akamzuia kisha akauliza we nani? Nikamjibu kuwa mi ni mpenzi wake, mpenzi wangu kuulizwa kama ananijua akakana akasema tulishaachana kama miezi mitatu imeshapita wkt jana yake tu tulikuwa pamoja. ......basi ghafla nilijikuta napata ujasiri wa ajabu (kumbuka pale mezani walikuwa wamekaa wanaume wanne wameshiba na wasichana wawili, mmoja ndio huyo mpnz wangu), basi nilimsogelea nikamuuliza unasema tumeachana miezi mitatu nyuma? Akasema ndio, likanitoka kofi moja kali sana, demu akaanguka Chini. ...jamaa mmoja akachukua chupa anipige, wengine nao wakawa wanaamka kwenye vitu, watu nao wakaanza kujaa mmh nikaona hapa nakufa, basi nikawaambia wale jamaa kuwa nyie hapa kama mtanipiga basi mniue lkn mkiniacha hai tu basi mi naenda kusubiri huyu mwanamke getini kwao, mtakuja kwenye msiba wake. .....bahati nzuri kuna jamaa mmoja ni askari alikuwa anapita ananifahamu akaja sehemu nilipo then akaniambia niondoke ila nisiende home kabla ya kwenda police maana wale jamaa wanaweza niwahi.
Nikatoka hapo huku namshukuru Mungu, nilikuwa nimepaki gari mbali hivyo hawakujua kuwa nimekuja na gari, nikaenda mpk police station (ni kama dk 2 kwa gari) nikatoa taharifa ya uongo na kweli pale, wkt naendelea kuongea na police mara naona majamaa nao wanaingia na demu wangu kuja kuripoti hehehehe, waliponiona wakawa wanaambiana, aah nae kaja?
Basi jamaa nao wakasema nimewafanyia fujo kisha nikampiga msichana wao, askari mmoja akawauliza kuwa yaani nyie miili mikubwa hivyo mnaweza fanyiwa fujo na mtu mmoja? Au mmekuja hapa ili kumkomoa baada ya kumchukulia mwanamke wake? ....kesi ikamalizwa kichina mi nikachomoka zangu nikiwa namshukuru mungu kwa mara nyingine. .....yule msichana kwa sasa yupo kitaa choka kweli kweli, nikijaga likizo na nilionana nae huwa ananiuliza kama sijammiss, yaani anaomba tukakumbushie wkt hajui mwenzie nilishafunga ukurasa juu yake
 
Hahahaaa...Mkuu hatukucheki ila kuna vitukio vilivyoelezewa (kama kujidai kufa halafu unasikia sauti ya tumchome moto) vinafurahisha, hasa msomaji anapoivuta hisia ya ubonge wako na umeshachezea kichapo kiasi kwamba kufumuka mbio linakuwa ni jambo lisilochagulika! POLE SANA
Acha mkuu baada ya yule demu kutukana jamaa yangu alipigwa kibao kikali sana.Afu kile kidume kikasema"chuchumaa chini".Jamaa yangu alivochuchumaa tu akavua sandals,ile kuinuka tu mbio nyingi,akaniachia balaa mimi.
 
Hahahaaa...Mkuu hatukucheki ila kuna vitukio vilivyoelezewa (kama kujidai kufa halafu unasikia sauti ya tumchome moto) vinafurahisha, hasa msomaji anapoivuta hisia ya ubonge wako na umeshachezea kichapo kiasi kwamba kufumuka mbio linakuwa ni jambo lisilochagulika! POLE SANA
Hahahahah yaani nilikuwa sijacheka wewe ndo umenilazimisha aiseee
 
nenda bongo movie mkuu kipande cha kuvunga umekufa kinakuhusu!
 
Tarehe kama ya leo mwez kama huu,huyu msichana alitukana na kuapia Miungu yote kuwa hatujui na wala hajawahi kutuona maishani mwake(msichana huyu alikuwa mpenzi wa rafiki yangu)
Wacha jamaa tuliyemkuta nae na washikaji zake waanze kutushushia kipondo.Jamaa yangu akatimka mbio nyingi sana nikabaki mimi na mwili wangu wa ukibonge nikiendelea kusulubiwa vilivyo huku watu wakizidi kuongezeka.Akili ikanituma nijifanye nimekufa,nikawa nawasikia wananchi wakisema "achomwe moto tu huyu" wengine liacheni limeshajifia hili likibaka.
Mungu mwema wakati wale wananchi wanajadiliana nini cha kufanya akatokea msamaria mmoja aliyenitambua na akawaambia huyu dogo sio kibaka mpaka kwao napajua.Na hiyo ndo ikawa salama yangu.
Nilipoteza viatu,simu,miwani,fulana na pesa kiasi.Wapenzi hususani dada zangu jaribuni kuwa na mioyo ya huruma kwenye mazingira kama haya.

Hahahaha..pole mkuu. Juzi tu, nilikuwa nawapa somo marafiki zangu wasiwe na pupa kuingia kwenye vurugu hadi wakiwa na uwakika wakushinda, nimepigana sana high school kufahamu ngumi ni rahisi kuzipanga kichwani lakini ukichezea knuckles unashangaa plan zote zinabadilika.
 
Daudi1 we acha tu rafiki, jamaa tukio lake ni lakuhudhunisha lakini kalielezea kwa "style" fulani inashawishi kucheka!!

Hahahahah yaani nilikuwa sijacheka wewe ndo umenilazimisha aiseee
 
Ha ha ha ha ha mbavu sina jamani, kaka zangu ukiona mwanamke wako yuko na mwingine usimsogelee kama huna kifua.
 
Ila kuna watu hawana akili au kujitoa ufahamu. Yani mwanamke kakukana wanakuanzishia vurugu, sasa wanadhani umemvamia usiemjua?
Upumbavu wao tu, hao mahakamani wanatakiwa kuhukumiwa bila option ya kulipa faini.
 
Umenikumbusha mbali sana. ...iliwahi nitokea, ...nilimkuta demu wangu yupo na jamaa wameshiba sana wanakunywa bia maeneo ya jirani na kambi moja ya polisi, kipindi hicho mi nna mwili mwembamba lakini nnajiamini balaa hehehe (changanya na mapenzi), basi nilivyomwona nikasogea mpk pale kisha nikamwomba niongee nae, mshkaji mmoja akamzuia kisha akauliza we nani? Nikamjibu kuwa mi ni mpenzi wake, mpenzi wangu kuulizwa kama ananijua akakana akasema tulishaachana kama miezi mitatu imeshapita wkt jana yake tu tulikuwa pamoja. ......basi ghafla nilijikuta napata ujasiri wa ajabu (kumbuka pale mezani walikuwa wamekaa wanaume wanne wameshiba na wasichana wawili, mmoja ndio huyo mpnz wangu), basi nilimsogelea nikamuuliza unasema tumeachana miezi mitatu nyuma? Akasema ndio, likanitoka kofi moja kali sana, demu akaanguka Chini. ...jamaa mmoja akachukua chupa anipige, wengine nao wakawa wanaamka kwenye vitu, watu nao wakaanza kujaa mmh nikaona hapa nakufa, basi nikawaambia wale jamaa kuwa nyie hapa kama mtanipiga basi mniue lkn mkiniacha hai tu basi mi naenda kusubiri huyu mwanamke getini kwao, mtakuja kwenye msiba wake. .....bahati nzuri kuna jamaa mmoja ni askari alikuwa anapita ananifahamu akaja sehemu nilipo then akaniambia niondoke ila nisiende home kabla ya kwenda police maana wale jamaa wanaweza niwahi.
Nikatoka hapo huku namshukuru Mungu, nilikuwa nimepaki gari mbali hivyo hawakujua kuwa nimekuja na gari, nikaenda mpk police station (ni kama dk 2 kwa gari) nikatoa taharifa ya uongo na kweli pale, wkt naendelea kuongea na police mara naona majamaa nao wanaingia na demu wangu kuja kuripoti hehehehe, waliponiona wakawa wanaambiana, aah nae kaja?
Basi jamaa nao wakasema nimewafanyia fujo kisha nikampiga msichana wao, askari mmoja akawauliza kuwa yaani nyie miili mikubwa hivyo mnaweza fanyiwa fujo na mtu mmoja? Au mmekuja hapa ili kumkomoa baada ya kumchukulia mwanamke wake? ....kesi ikamalizwa kichina mi nikachomoka zangu nikiwa namshukuru mungu kwa mara nyingine. .....yule msichana kwa sasa yupo kitaa choka kweli kweli, nikijaga likizo na nilionana nae huwa ananiuliza kama sijammiss, yaani anaomba tukakumbushie wkt hajui mwenzie nilishafunga ukurasa juu yake

Yaani huyo demu akikuuliza ememmiss, unatakiwa umwambie umemmiss kinoma, halafu unampotezea! unamwacha kwenye miti nyani wamcheke!!
 
Kumbe hii imewakuta wengi!! Back in 2005, Ilibaki kidogo niuliwe maeneo ya Kihesa Iringa Kisa Ummy!! Mh!! huyu demu kanipa majanga mengi ila Hilo la Kihesa nilipigwa nusu ya kufa, Kama sio defender la Polisi Sijui ..... Na since pale sijakutana na Huyo demu tena? Ila nna Hamu ya kumuona
 
Ha ha ha ha ha mbavu sina jamani, kaka zangu ukiona mwanamke wako yuko na mwingine usimsogelee kama huna kifua.

Yaani hii stori imenikumbusha kisa kimoja kilitokea kijijini kwetu huko Kagera wakati niko shule ya msingi. Kuna demu mmoja alikuwa anashea penzi na jamaa wawili hapo kijijini. Mmoja alikuwa mdogo kiumbo na pia umri na huyu mwigine kajazia kisawasawa na ni mkubwa kiumri na walikuwa hawajuani kuwa wanashea K ileile. Sasa siku ya timbwili ni kwamba kale kajamaa kalikuwa njiani na yule demu wanapiga stori katika pozi la kimahaba.. Huyo jamaa akawa anakuja yuko na mwenzie. Demu kuwaona akashtuka. Walipofika huyo jamaa kamuuliza demu kwa sauti ya ukali kuwa wakoje na hicho kivulana msichana kimya hana la kujibu. Mvulana kaulizwa akadai huyo ni demu wake. Jamaa likafura kwa hasira likakaamuru hako kavulana: " Nataka unisikilize vizuri, kuanzia muda huu nisikuone tena ukiwa karibu na huyu msichana wangu umesikia? Kama unataka kunifahamu mimi ni nani nikukute tena na huyu demu na sasa nahesabu hadi 5 nikimaliza uwe umeishapotea nisije nikakuharibu sasa hivi. Haya moja.......mbili.......tatu...... nne...." Kabla hajafika tano kajamaa kalitimua mbio na kupotea haraka sana kwa hofu na hakakumrudia tena huyo msichana kwa sababu ya usalama wake na pia kusaliitiwa na huyo demu.
 
Back
Top Bottom