EEX
JF-Expert Member
- Oct 19, 2014
- 4,312
- 13,966
Tarehe kama ya leo mwezi kama huu, huyu msichana alitukana na kuapia Miungu yote kuwa hatujui na wala hajawahi kutuona maishani mwake(msichana huyu alikuwa mpenzi wa rafiki yangu).
Wacha jamaa tuliyemkuta nae na washikaji zake waanze kutushushia kipondo.
Jamaa yangu akatimka mbio nyingi sana nikabaki mimi na mwili wangu wa ukibonge nikiendelea kusulubiwa vilivyo huku watu wakizidi kuongezeka.Akili ikanituma nijifanye nimekufa,nikawa nawasikia wananchi wakisema "achomwe moto tu huyu" wengine liacheni limeshajifia hili likibaka.
Mungu mwema wakati wale wananchi wanajadiliana nini cha kufanya akatokea msamaria mmoja aliyenitambua na akawaambia huyu dogo sio kibaka mpaka kwao napajua.
Na hiyo ndo ikawa salama yangu.
Nilipoteza viatu,simu,miwani,fulana na pesa kiasi.Wapenzi hususani dada zangu jaribuni kuwa na mioyo ya huruma kwenye mazingira kama haya.
Wacha jamaa tuliyemkuta nae na washikaji zake waanze kutushushia kipondo.
Jamaa yangu akatimka mbio nyingi sana nikabaki mimi na mwili wangu wa ukibonge nikiendelea kusulubiwa vilivyo huku watu wakizidi kuongezeka.Akili ikanituma nijifanye nimekufa,nikawa nawasikia wananchi wakisema "achomwe moto tu huyu" wengine liacheni limeshajifia hili likibaka.
Mungu mwema wakati wale wananchi wanajadiliana nini cha kufanya akatokea msamaria mmoja aliyenitambua na akawaambia huyu dogo sio kibaka mpaka kwao napajua.
Na hiyo ndo ikawa salama yangu.
Nilipoteza viatu,simu,miwani,fulana na pesa kiasi.Wapenzi hususani dada zangu jaribuni kuwa na mioyo ya huruma kwenye mazingira kama haya.