Nigrastratatract nerve
JF-Expert Member
- Sep 4, 2019
- 1,395
- 3,901
PONGEZI SANA KWA RAIS JOHN MAGUFULI KWA KUFANYA MAAMUZI MAGUMU YA KUHAMISHIA IKULU DODOMA.
Na Fredrick Mmari
+255 717 220707
Ikumbukwe mwaka 1891 Ujerumani iliitangaza Dar es Salaam kuwa makao makuu ya utawala wake.
Baada ya vita vya kwanza vya dunia 1914 -1918, Mjerumani aliondolewa kwenye utawala wa Tanganyika na nchi ikaendeshwa na Muingereza.
Mwaka 1920, Uingereza ilianza ujenzi wa Ikulu yake eneo lile lile walipojenga Wajerumani na kumaliza ujenzi huo mwaka 1922, mwaka ambao Baba wa Taifa letu Mwl. J.K Nyerere alizaliwa.
Mwaka 1956, Mwingereza alijenga jengo lingine pembeni ya eneo la Ikulu hiyo.
AWAMU YA KWANZA. Ilipofika mwaka 1968-1969, Mwl. J.K Nyerere alijenga jengo lingine na kufanya Ikulu kuwa na majengo makubwa manne.
AWAMU YA PILI. Kuanzia utawala wa Mzee Mwinyi miaka ya 1990 ikulu hiyo ilizungushiwa ukuta.
AWAMU YA TATU. Utawala wa Mzee Mkapa kuanzia miaka ya 1995 akaja kujenga makazi ya Rais Ikulu hapo.
AWAMU YA NNE. Enzi za utawala wa Kikwete kuanzia miaka ya 2005, Ikulu palijengwa ukumbi wa mikutano ujulikanao kama Kikwete Hall.
Hiyo ni historia fupi ya Ikulu ya Dar es Salaam.
Wakati wa Mwl. J.K nyerere alipendekeza makao makuu ya nchi yatoke Dar es Salaam na yahamie Dodoma.
Mapendekezo hayo yalitolewa 1971/73 na kushirikisha mikoa yote ya Tanzania.
Ipo mikoa iliyokataa uamuzi wa kuhamishiwa makao makuu mkoani Dodoma na kati ya mikoa iliyokataa Pwani ni mmoja wapo.
Mwaka 1977 maamuzi ya kuhamishia makao makuu Dodoma yaliazimiwa rasmi.
Awamu zote hizo maamuzi ya kuhamishia makao makuu kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma yalikua yanafanyika kidogo kidogo ila AWAMU YA TANO ndio yamefanya kwa haraka zaidi.
Hakika ni ujasiri mkubwa na mgumu ambao unahitaji gharama sana.
Leo 30/5/2020, Rais John Pombe Magufuli ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ikulu ya Chamwino, Dodoma akishirikiana na mama Maria Nyerere kwa niaba ya Baba wa Taifa (Mwl. J.K Nyerere), Rais wastaafu wakiwemo, Mzee Alhasan Mwinyi, Benjamín Mkapa, na Jakaya Kikwete.
Pia Mheshimiwa Rais Magufuli aliambatana na viongozi mbalimbali wa serikali,bunge,mahakama,jeshi na vyama vya siasa kwenye kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Ikulu ya Dodoma ambapo ndani ya miezi mitano Ikulu itakua imekamilika.
Ikulu ya Dar es Salaam na barabara zake ina eneo la hekari 41 na ya Chamwino ina hekari 8473.
Tayari ikulu ya Chamwino imeshazungushiwa ukuta wenye urefu wa kilometa 27.
HAKIKA HIZI NI JITIHADA KUBWA SANA NA ZA KUPONGEZWA ZINAZOFANYWA NA SERIKALI YA AWAMU YA TANO CHINI YA RAIS JOHN MAGUFULI.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
MUNGU NAOMBA UMLINDE NA KUMUONGOZA VYEMA RAIS WETU JOHN MAGUFULI.
Na Fredrick Mmari
+255 717 220707
Ikumbukwe mwaka 1891 Ujerumani iliitangaza Dar es Salaam kuwa makao makuu ya utawala wake.
Baada ya vita vya kwanza vya dunia 1914 -1918, Mjerumani aliondolewa kwenye utawala wa Tanganyika na nchi ikaendeshwa na Muingereza.
Mwaka 1920, Uingereza ilianza ujenzi wa Ikulu yake eneo lile lile walipojenga Wajerumani na kumaliza ujenzi huo mwaka 1922, mwaka ambao Baba wa Taifa letu Mwl. J.K Nyerere alizaliwa.
Mwaka 1956, Mwingereza alijenga jengo lingine pembeni ya eneo la Ikulu hiyo.
AWAMU YA KWANZA. Ilipofika mwaka 1968-1969, Mwl. J.K Nyerere alijenga jengo lingine na kufanya Ikulu kuwa na majengo makubwa manne.
AWAMU YA PILI. Kuanzia utawala wa Mzee Mwinyi miaka ya 1990 ikulu hiyo ilizungushiwa ukuta.
AWAMU YA TATU. Utawala wa Mzee Mkapa kuanzia miaka ya 1995 akaja kujenga makazi ya Rais Ikulu hapo.
AWAMU YA NNE. Enzi za utawala wa Kikwete kuanzia miaka ya 2005, Ikulu palijengwa ukumbi wa mikutano ujulikanao kama Kikwete Hall.
Hiyo ni historia fupi ya Ikulu ya Dar es Salaam.
Wakati wa Mwl. J.K nyerere alipendekeza makao makuu ya nchi yatoke Dar es Salaam na yahamie Dodoma.
Mapendekezo hayo yalitolewa 1971/73 na kushirikisha mikoa yote ya Tanzania.
Ipo mikoa iliyokataa uamuzi wa kuhamishiwa makao makuu mkoani Dodoma na kati ya mikoa iliyokataa Pwani ni mmoja wapo.
Mwaka 1977 maamuzi ya kuhamishia makao makuu Dodoma yaliazimiwa rasmi.
Awamu zote hizo maamuzi ya kuhamishia makao makuu kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma yalikua yanafanyika kidogo kidogo ila AWAMU YA TANO ndio yamefanya kwa haraka zaidi.
Hakika ni ujasiri mkubwa na mgumu ambao unahitaji gharama sana.
Leo 30/5/2020, Rais John Pombe Magufuli ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ikulu ya Chamwino, Dodoma akishirikiana na mama Maria Nyerere kwa niaba ya Baba wa Taifa (Mwl. J.K Nyerere), Rais wastaafu wakiwemo, Mzee Alhasan Mwinyi, Benjamín Mkapa, na Jakaya Kikwete.
Pia Mheshimiwa Rais Magufuli aliambatana na viongozi mbalimbali wa serikali,bunge,mahakama,jeshi na vyama vya siasa kwenye kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Ikulu ya Dodoma ambapo ndani ya miezi mitano Ikulu itakua imekamilika.
Ikulu ya Dar es Salaam na barabara zake ina eneo la hekari 41 na ya Chamwino ina hekari 8473.
Tayari ikulu ya Chamwino imeshazungushiwa ukuta wenye urefu wa kilometa 27.
HAKIKA HIZI NI JITIHADA KUBWA SANA NA ZA KUPONGEZWA ZINAZOFANYWA NA SERIKALI YA AWAMU YA TANO CHINI YA RAIS JOHN MAGUFULI.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
MUNGU NAOMBA UMLINDE NA KUMUONGOZA VYEMA RAIS WETU JOHN MAGUFULI.