Iko wapi sauti ya wakulima?

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
Takwimu zinaonyesha kwamba zaidi ya asilimia 65 ya watanzania walio masikini wa kutupwa, ni wakulima waishio vijijini. Aidha tafiti zinaonyesha kwamba masikini hao mara kwa mara huwa wakilazimishwa kuchangia miradi ya maendeleo kwa viwango vinavyozidi vyanzo vyao vya mapato. Chukua mfano wa hizi shule za kata, ambazo serikali ya awamu ya nne inajivunia; huku Kagera, kwa viwango vilivyokuwa vimewekwa, familia masikini zililazimishwa kuchangia hadi asilimia 80 ya pato lake la mwaka kifedha. Swali langu ni je kuna chombo chochote katika jamhuri hii kinachowakilisha wakulima? Na kama kipo mbona sauti yake haisikiki? Naomba majibu kutoka kwa wana JF
 
Back
Top Bottom