Ikiwa VETA wenyewe ni namna hii...

mtanzania in exile

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
1,335
1,183
Si lengo langu kudhihaki au kukejeli bali ni kuleta mjadala wa maana hapa.

Baada ya kuona watu hapa wanaulizia sana kuhusu VETA nikaona bora nitembelee website yao ambayo baada ya kusearch kwenye internet nimepata anuani yao kama hivi Vocational Education and Training Authority -- VETA --. Hii ni taasisi ya serikali inayolenga juu ya elimu kwa watanzania.

Nimeshitushwa sana na design nzima ya website yao. Na nadhubutu kusema kuwa inaonekana kama imekuwa designed na mtoto wa sekondari. To be honest my nephew who is in year 8 can design better website than that. Sijui ni kiasi gani VETA wametumia kumlipa aliyewatengenezea website hii lakini ni aibu mno, wameibiwa ile mbaya.

Kwanza ni kwa nini kuna script ya krismasi na mwaka mpya hadi hii leo? tena na wala sio clip ambayo wametengeneza wao wenyewe ila wamekopi kutoka kwenye internet. Tuko karibu ya kumaliza februari jamani!!

Halafu kuna suali zima la matumizi ya application waliotumia kudesign na maamuzi ya kutumia tables. Sehemu ya juu iko zaidi upande wa kulia na sehemu ya chini iko zaidi upande wa kushoto, sijui ni kwa nini wameshindwa ku-centre the whole website. Links zimetupwa tupwa tu na nyingi ukigonga hazina lolote.

Suali langu ni kwa nini VETA haioni hili? je hawana watu wa kuwatenegenezea website za uhakika? hii ni website ya serikali na inaonekana duniani kote, ni aibu na inaonyesha kuwa Tanzania hatuna watu wanaoweza kudesign website, jambo ambalo sio la kweli. Ni aibu zaidi ukizingatia zaidi malengo na madhumuni ya VETA, walihitajika kuonyesha mfano mzuri. Je kama pesa ni tatizo kwa nini hawawaliki wanafunzi wa field kwenda kuwafanyia kazi? Kuna watu tele humu wenye IT qualifications wanatafuta kazi za field, na watafurahi mno wakipewa nafasi kama hii.

Ushauri wa bure kwa VETA ni tafuteni wanafunzi wa field, waunde website team hapo ofisini penu na wa-redesign website yote. Naamini wapo vijana wenye uwezo wa kudesin website nzuri hapo Tanzania
 
We kula jiwe tu ndugu ulale, hapo ujue wao ndio wanapenda website hiyo jinsi ilivyo hivyo, na ukae ujue hii ndio Tanzania. Kama huijui sasa ijue kuwa kila jambo siasa na usanii vinachukua nafasi.
 
Veta wamepata authority but wamekosa innovation na uwajibikaji umekuwa mdogo sio kwa issue ya website tu lakini angalia hata course wanazotoa yani ni lowest class ile mbaya ukilinganisha na zile zinazotolewa na maghorofa ya kariakoo
 
nimetembelea website yao,no comment!ama kweli hii ndo Tanzania yenye hari mpya na kasi mpya ya kuelekeaa wap?Usishangae aliyepewa kaz ya kuitengeneza ni mtoto wa mkubwa,haya twede kazi wakuu..............!
 
nimeangalia hiyo website-kwa kweli inatia aibu-hii nchi hakuna aliye serious kabisa
 
Duuh! hii mbona kama ni ya mwanafunzi anayejifunza ku-desgn website aibu tupu
 
ya ngoswe ayo 2mwachie ngoswe!na ruzuku wanapata kila mwaka yan ata colege za kkoo zinawashnda!
 
Mmmh,mi sisemi ,ila nadhani veta wanapokea ushauri,milango iko wazi kwa kila mtu,kupeleka maoni,ushauri,nk ili kuboresha VETA yetu,hayakatazwi maoni,wala ushauri,mi nadhani kwa yeyote mwenye maoni na ushauri wa kuboresha taasisi hii ni vyema akachangia moja kwa moja kwa mkurugenzi mkuu,director general wa veta ni mwelewa,na anapokea maoni kwa kila mtu,na hufanyia kazi.
Tusibaki kuchekana,kwani kama ni aibu basi wa tz wote tutaipata,shime wa tz,TANZANIA NI YETU,VETA NI YETU,MICHANGO YETU YA KUIBORESHA VETA INATAKIWA SANA.
Ni yangu machache tu,kama nipo wrong niwieni radhi.
Ni imani yangu kuwa kwa kila mwenye uchungu na nchi yake atajitahidi kutoa ushauri wa wazi kwa wahusika,ndo maana kuna anwani ambazo zipo wazi,na masanduku ya maoni kila mahali.ila kama umetoa maoni yakapuuzwa labda ndipo ulalamike,japo pia itaangaliwa maoni yenyewe yana uzito gani na mchango gani.
Mi nadhani sote ni wa Tanzania,tuboreshe kwa maoni na ushauri wetu,kwani upeo na elimu pia tunatofautiana.
mwakalingaeli@yahoo.com
 
Mmmh,mi sisemi ,ila nadhani veta wanapokea ushauri,milango iko wazi kwa kila mtu,kupeleka maoni,ushauri,nk ili kuboresha VETA yetu,hayakatazwi maoni,wala ushauri,mi nadhani kwa yeyote mwenye maoni na ushauri wa kuboresha taasisi hii ni vyema akachangia moja kwa moja kwa mkurugenzi mkuu,director general wa veta ni mwelewa,na anapokea maoni kwa kila mtu,na hufanyia kazi.
Tusibaki kuchekana,kwani kama ni aibu basi wa tz wote tutaipata,shime wa tz,TANZANIA NI YETU,VETA NI YETU,MICHANGO YETU YA KUIBORESHA VETA INATAKIWA SANA.
Ni yangu machache tu,kama nipo wrong niwieni radhi.
Ni imani yangu kuwa kwa kila mwenye uchungu na nchi yake atajitahidi kutoa ushauri wa wazi kwa wahusika,ndo maana kuna anwani ambazo zipo wazi,na masanduku ya maoni kila mahali.ila kama umetoa maoni yakapuuzwa labda ndipo ulalamike,japo pia itaangaliwa maoni yenyewe yana uzito gani na mchango gani.
Mi nadhani sote ni wa Tanzania,tuboreshe kwa maoni na ushauri wetu,kwani upeo na elimu pia tunatofautiana.
mwakalingaeli@yahoo.com

Well said!
 
si lengo langu kudhihaki au kukejeli bali ni kuleta mjadala wa maana hapa.

Baada ya kuona watu hapa wanaulizia sana kuhusu veta nikaona bora nitembelee website yao ambayo baada ya kusearch kwenye internet nimepata anuani yao kama hivi vocational education and training authority -- veta --. Hii ni taasisi ya serikali inayolenga juu ya elimu kwa watanzania.

Nimeshitushwa sana na design nzima ya website yao. Na nadhubutu kusema kuwa inaonekana kama imekuwa designed na mtoto wa sekondari. To be honest my nephew who is in year 8 can design better website than that. Sijui ni kiasi gani veta wametumia kumlipa aliyewatengenezea website hii lakini ni aibu mno, wameibiwa ile mbaya.

Kwanza ni kwa nini kuna script ya krismasi na mwaka mpya hadi hii leo? Tena na wala sio clip ambayo wametengeneza wao wenyewe ila wamekopi kutoka kwenye internet. Tuko karibu ya kumaliza februari jamani!!

Halafu kuna suali zima la matumizi ya application waliotumia kudesign na maamuzi ya kutumia tables. Sehemu ya juu iko zaidi upande wa kulia na sehemu ya chini iko zaidi upande wa kushoto, sijui ni kwa nini wameshindwa ku-centre the whole website. Links zimetupwa tupwa tu na nyingi ukigonga hazina lolote.

Suali langu ni kwa nini veta haioni hili? Je hawana watu wa kuwatenegenezea website za uhakika? Hii ni website ya serikali na inaonekana duniani kote, ni aibu na inaonyesha kuwa tanzania hatuna watu wanaoweza kudesign website, jambo ambalo sio la kweli. Ni aibu zaidi ukizingatia zaidi malengo na madhumuni ya veta, walihitajika kuonyesha mfano mzuri. Je kama pesa ni tatizo kwa nini hawawaliki wanafunzi wa field kwenda kuwafanyia kazi? Kuna watu tele humu wenye it qualifications wanatafuta kazi za field, na watafurahi mno wakipewa nafasi kama hii.

Ushauri wa bure kwa veta ni tafuteni wanafunzi wa field, waunde website team hapo ofisini penu na wa-redesign website yote. Naamini wapo vijana wenye uwezo wa kudesin website nzuri hapo tanzania

asante kaka mtz, nilidhani hili swala nililiona peke yangu kumbe tuko wengi eh?? Yaani ni aibu, aibu tupu. Loh!!!!!!!!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom