Ikitokea kuna Kiongozi ana Macho mazuri, na umeyapenda, je, kuna ubaya kumsifia macho yake? Ni ukosefu wa heshima na adabu?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,722
Wana MMU,

Salaam.

Nina swali, inapotokea wewe unapenda macho, halafu kukatokea kuna kiongozi fulani mwanamke ana jicho hilo!, wewe unapenda jicho, ukimuona huyo mwenye jicho, unafurahi na huchoki kumwangalia.

Je, kuna ubaya wowote ukimsifia huyo kiongozi mwenye hilo jicho kuwa "MashAllah Mungu amekujaalia jicho" au itaonekana huo ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa adabu, heshima na ustaarabu?.

Paskali.
 
Duuhh kwa uzi huu , mkuu Mayalla ni bora ulizaliwa zaman saiz una mke na watoto.

BILA HIVO izi ligi za ujana kwasasa usingeziweza kabisa , na watoto wakali wakali km Jokate, Usingethbutu hata kumshika mkono maana ni kiongozi alafu ni mkaliiii kinyama.

Watoto hawa wanapenda sisi masela, ambao tunajiamin kiasi kwamba hata mbele za vyombo vya habar bado unaweza mwambie "Mkuu wangu umependeza sana nahayo macho yako mimi najikuta ulimi unakua mzito"

Utamuona anacheka cheka kwa aibu alafu anakujibu " hahah Pascal bwanaaaa ,aya nashukuru sana".

Umenikumbusha Mzungu mmoja m'mama alinifundishaga Pathology , sasa huyu mama kila nlipokutana naye namsifia kinyamaa, aiseeee kuna likizo yupo Kwao Ujeruman alivorudi kanilitea Bongee la zawadi .

NASIKITIKA KUKUAMBIA WATOTO WAKALI WAKALI WOTE UNGEWAITA SHEMEJI
 
Umenikumbusha Mzungu mmoja m'mama alinifundishaga Pathology ,
Du!...Mkuu Carlos The Jackal (aka Vladimirovich Putin), umetisha, kumbe umepiga Pathology?. Toka nimejiunga JF, leo ndio nimekutana na mtu wa Pathology, zamani enzi za Nyerere, tulikuwa na ma pathologist wawili tuu, mmoja ni Dr. Shaba alikuwa Muhimbili na mwingine ni Dr. Mkulila alikuwa Bugando. Inasemekana kwenye medical school ya enzi hizo, kabla ya mambo ya neurosurgery, pathology ndio lilikuwa somo gumu sana, jee ni kweli?, Au ugumu wa pathology, ni uoga tuu wa kucheza na zile cadavers?.

Au pathology yako ni somo tuu kwenye mtaala wa MD na sio kusoma pathology ili uwe pathologist?.
P
 
 
Kuna siku sehem alikuwa anasinzia kabisa kama ngamia jukwaani katika wageni rasmi waandishi wa habari kama walishtukia lile jicho basi kila sekunde kamera inammulika kesho yakenikajaona kibonzo cha masoud kipanya kamchora vile vile
Mhh sijui hata, sijui mkuu. Naogopa hata kusema kuhusu hawa watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…