Wana JF,
Nafuatilia siasa za Igunga. Hivi sasa mawaziri wamehamia huko. Hivyo imedhihirika kuwa wapinzani sasa wanapambana na serikali siyo CCM. Hivyo, ni kitu gani kitakachomzuia Waziri wa Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha kukipigia kampeni chama chake kama wanavyofanya mawaziri wengine? Tena, mawaziri wenzake wamejipambanua kabisa kuendesha kampeni hizo kwa kutumia mamlaka waliyonayo ya kiserikali. Imefika wakati wanajisahau hadi wanatoa kauli kama vile tutaweka bajeti maalumu. Kwamba, huyu ndiye nitafanya naye kazi. Serikali ni ya CCM. Kauli hizi siyo tu zinavunja sheria lakini pia, zinachochea uhasama na uadui mkubwa kwani zinaonyesha kuwa serikali inaendeshwa kwa misingi ya kibaguzi kutokana na itikadi ya vyama. Kama serikali inasema kuwa akishinda mpinzani serikali haitoi ushirikiano hapo tumefika wapi? Ama kama serikali inatamka wazi kuwa bajeti iliyopo ni ya chama fulani maana yake kuwa, wananchi wasio wa chama hicho bajeti hiyo haiwahusu? Basi kama hivyo ndiyo, serikali hii itafika wakati itakosa uhalali wa kukusanya kodi wa watu ambao hawatoki chama husika. Lakini, kubwa zaidi kauli hizi ndizo zinasababisha serikali kuchukiwa zaidi.
Hivyo sasa, tujiulize Nahodha kwa nafasi yake, je atajizuia kukisaidia chama chake? Je, yeye ni Malaika wa kuweza kulinda heshima yake ya Uwaziri wa Polisi asiingie kwenye lindi la akina Magufuli na Wasira ambao wametangaza wazi kabisa kuwa nyadhifa zao zipo pale kuitumikia CCM? Ngoja tuone!
Nafuatilia siasa za Igunga. Hivi sasa mawaziri wamehamia huko. Hivyo imedhihirika kuwa wapinzani sasa wanapambana na serikali siyo CCM. Hivyo, ni kitu gani kitakachomzuia Waziri wa Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha kukipigia kampeni chama chake kama wanavyofanya mawaziri wengine? Tena, mawaziri wenzake wamejipambanua kabisa kuendesha kampeni hizo kwa kutumia mamlaka waliyonayo ya kiserikali. Imefika wakati wanajisahau hadi wanatoa kauli kama vile tutaweka bajeti maalumu. Kwamba, huyu ndiye nitafanya naye kazi. Serikali ni ya CCM. Kauli hizi siyo tu zinavunja sheria lakini pia, zinachochea uhasama na uadui mkubwa kwani zinaonyesha kuwa serikali inaendeshwa kwa misingi ya kibaguzi kutokana na itikadi ya vyama. Kama serikali inasema kuwa akishinda mpinzani serikali haitoi ushirikiano hapo tumefika wapi? Ama kama serikali inatamka wazi kuwa bajeti iliyopo ni ya chama fulani maana yake kuwa, wananchi wasio wa chama hicho bajeti hiyo haiwahusu? Basi kama hivyo ndiyo, serikali hii itafika wakati itakosa uhalali wa kukusanya kodi wa watu ambao hawatoki chama husika. Lakini, kubwa zaidi kauli hizi ndizo zinasababisha serikali kuchukiwa zaidi.
Hivyo sasa, tujiulize Nahodha kwa nafasi yake, je atajizuia kukisaidia chama chake? Je, yeye ni Malaika wa kuweza kulinda heshima yake ya Uwaziri wa Polisi asiingie kwenye lindi la akina Magufuli na Wasira ambao wametangaza wazi kabisa kuwa nyadhifa zao zipo pale kuitumikia CCM? Ngoja tuone!