IGP Sirro siyo mkweli

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Tumemsikia IGP Sirro akijitetea kuhusu tuhuma zinazopewa Jeshi lake la Polisi kuhusu kuwakamata mfululizo wabunge wa chama cha Chadema kuwa ni uonevu. Akijibu tuhuma hiyo amejibu kuwa Jeshi lake la Polisi halina upendeleo na halifanyi uonevu bali linawakamata raia wote waliofanya makosa ya jinai bila kujali nyadhifa zao katika jamii na bila kujali itikadi zao za kisiasa.

Kutokana na kujitetea kwake IGP wetu Sirro nami ningependa kumuuliza maswali yafuatayo:-

1. Jeshi lake limemkamata Tundu Lissu kutokana na Press conference aliyofanya na aliyoeleza kuwa Bombardier yetu imekamatwa nchini Canada kutokana na kudaiwa fidia na kampuni moja ya ujenzi ambayo ilivunjiwa mkataba wake wa ujenzi wa barabara hapa nchini miaka ya nyuma na aliyekuwa Waziri wa ujenzi wa wakati huo ambaye hivi sasa ni Rais wetu.

Katika Press conference iliyoitishwa baadaye na msemaji wa serikali Zamaradi Kawawa na akakiri kuwa kweli Bombardier yetu imezuiliwa huko Canada kutokana na kudaiwa fidia ya shilingi bilioni 87. Je kosa la Tundu Lissu lililosababisha kukamatwa kwake ni lipi iwapo serikali yenyewe imekiri kukamatwa kwa Bombardier yetu?

2. Tukio lingine ni la kukamatwa kwa Mbunge Esther Bulaya wa Bunda kwa kwenda kwenye Jimbo la Mbunge mwenzake wa Chadema John Heche wa Tarime na kushiriki harambee ya ujenzi wa shule ya Nyamongo, ambapo alikamatwa na Jeshi la Polisi kwa madai ni "makosa" kwa mbunge wa Jimbo lingine kwenda kwenye Jimbo lingine la mwenzake na kushiriki harambee kwa ajili ya maendeleo ya eneo hilo husika!

Sasa nimuulize IGP Sirro, mbona hujamkamata Mbunge Kingu wa CCM ambaye alifanya "the same thing" kwa kwenda kwenye Jimbo la Singida Mashariki la Tundu Lissu wa Chadema ba akaendesha harambee ya ujenzi wa shule?

Nimuukize swali jingine IGP Sirro, mbona Jeshi lake la Polisi halijamkamata Mbunge wa viti maalum wa CCM Tulia Ackson ambaye alienda Jimbo la Mbeya mjini la mbunge Sugu wa Chadema kwa kushiriki harambee ya ujenzi wa soko la Sido lililoungua hivi karibuni?

Kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu Jeshi la Polisi linapaswa liwe fair na kuwa neutral na lisijiegemeze kwenye chama chochote cha siasa.

Hata hivyo ni jambo lililo wazi kuwa Jeshi letu la Polisi limejiegemeza upande wa chama tawala katika utekelezaji wa majukumu yake na hilo jambo ni vigumu sana kwa mtu yeyote kulikanusha.
 
Mfano mwingine wa wazi wa namna gani Jeshi letu la Polisi huwa linawapendelea wabunge wa CCM ni tukio lililotokea mwezi July mwaka 2015, ambapo Mbunge Job Ndugai wa Kongwa alimchapa bakora mgombea mwenzake wa CCM kwenye kura za maoni za Jimbo lao, mgombea huyo alikuwa Dr Chilongani hadi akasababisha huyo jamaa azirai na kukimbizwa hospitali ya Kongwa na kulazwa kwa siku kadhaa.

Je ni kwanini Jeshi lake la Polisi halikumkamata Mbunge huyo wa CCM Job Ndugai na kumfikisha mahakamani kwa kosa lake la jinai la kumpiga mgombea mwenzake kwenye kura za maoni hadi akasababisha azirai kama Jeshi hilo haliwapendelei wabunge wa CCM na kuwapa "special status" ya kuwa ni watu untouchables?
 
Huyo mzee ni mwepesi wa kusahau, huoni hata mama kaganda ambaye makonda aliwashutumu wote wawili kupokea rushwa kamsahau itakuwa viongozi wa upinzani
 
Fanya kumbukumbu vizuri, nadhani waziri wa ujenzi wa wakati huo alikuwa mbunge wa jimbo moja katika mkoa wa pwani
Ngoja nikuwekee kumbukumbu vizuri, ni kweli wakati hukumu ya mahakama ilipotolewa ya nchi yetu kutakiwa kulipa fidia mwaka huo 2009, huyo JPM hakuwa Waziri wa Ujenzi na wakati huo alikuwa Shukuru Kawambwa, lakini wakati mkataba huo wa ujenzi wa barabara unavunjwa Waziri wa ujenzi alikuwa Rais wetu.
 
Fanya kumbukumbu vizuri, nadhani waziri wa ujenzi wa wakati huo alikuwa mbunge wa jimbo moja katika mkoa wa pwani
Tatizo hawa Wapinzani hawajitambui halafu ni wasahaulifu sana wameishiwa hoja ss wanaropoka km waliokunywa maji ya chooni Chadema kma kweli wanataka kuongoza Nchi wasingempokea Lowasa aliyemuita Fisadi na Nchi nzima walizunguka kuutangazia umma km El nifisad ss wakati mwingine unashindwa kuwaeleea hawa wtu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfano mwingine wa wazi wa namna gani Jeshi letu la Polisi huwa linawapendelea wabunge wa CCM ni tukio lililotokea mwezi July mwaka 2015, ambapo Mbunge Job Ndugai wa Kongwa alimchapa bakora mgombea mwenzake wa CCM kwenye kura za maoni za Jimbo lao, mgombea huyo alikuwa Dr Chilongani hadi akasababisha huyo jamaa azirai na kukimbizwa hospitali ya Kongwa na kulazwa kwa siku kadhaa.

Je ni kwanini Jeshi lake la Polisi halikumkamata Mbunge huyo wa CCM Job Ndugai na kumfikisha mahakamani kwa kosa lake la jinai la kumpiga mgombea mwenzake kwenye kura za maoni hadi akasababisha azirai kama Jeshi hilo haliwapendelei wabunge wa CCM na kuwapa "special status" ya kuwa ni watu untouchables?
Duuh we kweli kilqza inamaana wakati wakampeni Sirro alikuwa IGP?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngoja nikuwekee kumbukumbu vizuri, ni kweli wakati hukumu ya mahakama ilipotolewa ya nchi yetu kutakiwa kulipa fidia mwaka huo 2009, huyo JPM hakuwa Waziri wa Ujenzi na wakati huo alikuwa Shukuru Kawambwa, lakini wakati mkataba huo wa ujenzi wa barabara unavunjwa Waziri wa ujenzi alikuwa Rais wetu.
Yupi, huyu alieko sasa hivi madarakani?
 
Tatizo hawa Wapinzani hawajitambui halafu ni wasahaulifu sana wameishiwa hoja ss wanaropoka km waliokunywa maji ya chooni Chadema kma kweli wanataka kuongoza Nchi wasingempokea Lowasa aliyemuita Fisadi na Nchi nzima walizunguka kuutangazia umma km El nifisad ss wakati mwingine unashindwa kuwaeleea hawa wtu

Sent using Jamii Forums mobile app
BTW, awali wakati wa utekelzaji wa mradi wapunzani walichafua hali ya hewa bungeni kuwa ujenzi ulikuwa hafifu na umechelewa kukamilika, bila shaka bunge liliweka maazimio ambayo leo wapinzani wanadhani ni dhambi ya waziri
 
Fanya kumbukumbu vizuri, nadhani waziri wa ujenzi wa wakati huo alikuwa mbunge wa jimbo moja katika mkoa wa pwani

Hujui lolote ww, huyo waziri wa Pwani alikuwa wakati tunashindwa kesi, ila alikuta mkataba umeshavunjwa. Jiongeze kwamba jamaa sio mtu anayejali sheria bali anajali matamanio yake. Mfano mrahisi ni sasa, kuna zuio la mahakama lakini kuna bomoabomoa inaendelea
 
Back
Top Bottom