Prof Koboko
JF-Expert Member
- Aug 15, 2020
- 350
- 2,549
IGP Siro ni tatizo?
Huyu IGP watu wanalamamika wanabambikiwa kesi na polisi yupo kimya, huyu IGP Rais analalamika watu wanabambikiwa kesi yeye yupo kimya, sasa anafanya kitu gani?
Kama mkuu wa nchi analalamika zaidi ya mara 1 kua kwenye jeshi la polisi kuna tatizo kubwa yeye anachukua kawaida, sijui anaona kua ni maneno ya wanasiasa tu.
Sikutegemea kua IGP angemnanga mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kua ni mtu mbaya kiasi kile kisha baadaye mahakamani ikaonekana ameshtakiwa kwa makosa ya hovyo na yasiyoeleweka kabisa. Yaani IGP mzima anajiapiza kabisa kua kuna ushahidi mkubwa ambao unamhusu Mbowe kisha eti ni mipango ya ugaidi wa laki 6? Huyu mzee wetu angestaafu tu kama alivyosema Mbatia alishaomba kustaafu siku nyingi apewe tu nafasi hiyo akae pembeni, ameshindwa kabisa kulijenga jeshi hili, lawama ni nyingi sana.
IGP kabla ya uchaguzi mkuu 2020 alikua anatembea na CD za vurugu za nyuma kwenye mikutano ya CHADEMA akionyesha yaliyotokea, baada ya hapo niligundua kua huyu mzee kuna mahali ana shida. Rais akimwacha kiongozi mkubwa kama IGP yupo biased na jamii kiasi hiki, iko siku atamstaafisha haraka.Kazi zimemshinda kwakweli.
Kuhusu tukio la Hamza Mohamed, kwa wengi tivyomwangalia kupitia video clips za tukio la juzi yule kijana alivyokuwa akiongea kabla ya kupigwa risasi na polisi, utakugundua ni kama mtu ambaye alijaa kisasi na kudhulumiwa akijuacho yeye. Kwanini polisi wasiendelee kutafakari hizo kauli zake? Sasa IGP yeye kauli yake ni bahati mbaya kuzaa kijana Kama Hamza, Wazazi wake walipenda au walijua kua watazaa mtu aina ya Hamza?
Huyu IGP watu wanalamamika wanabambikiwa kesi na polisi yupo kimya, huyu IGP Rais analalamika watu wanabambikiwa kesi yeye yupo kimya, sasa anafanya kitu gani?
Kama mkuu wa nchi analalamika zaidi ya mara 1 kua kwenye jeshi la polisi kuna tatizo kubwa yeye anachukua kawaida, sijui anaona kua ni maneno ya wanasiasa tu.
Sikutegemea kua IGP angemnanga mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kua ni mtu mbaya kiasi kile kisha baadaye mahakamani ikaonekana ameshtakiwa kwa makosa ya hovyo na yasiyoeleweka kabisa. Yaani IGP mzima anajiapiza kabisa kua kuna ushahidi mkubwa ambao unamhusu Mbowe kisha eti ni mipango ya ugaidi wa laki 6? Huyu mzee wetu angestaafu tu kama alivyosema Mbatia alishaomba kustaafu siku nyingi apewe tu nafasi hiyo akae pembeni, ameshindwa kabisa kulijenga jeshi hili, lawama ni nyingi sana.
IGP kabla ya uchaguzi mkuu 2020 alikua anatembea na CD za vurugu za nyuma kwenye mikutano ya CHADEMA akionyesha yaliyotokea, baada ya hapo niligundua kua huyu mzee kuna mahali ana shida. Rais akimwacha kiongozi mkubwa kama IGP yupo biased na jamii kiasi hiki, iko siku atamstaafisha haraka.Kazi zimemshinda kwakweli.
Kuhusu tukio la Hamza Mohamed, kwa wengi tivyomwangalia kupitia video clips za tukio la juzi yule kijana alivyokuwa akiongea kabla ya kupigwa risasi na polisi, utakugundua ni kama mtu ambaye alijaa kisasi na kudhulumiwa akijuacho yeye. Kwanini polisi wasiendelee kutafakari hizo kauli zake? Sasa IGP yeye kauli yake ni bahati mbaya kuzaa kijana Kama Hamza, Wazazi wake walipenda au walijua kua watazaa mtu aina ya Hamza?