Igizo la lockdown: CHADEMA inacheza kamari

Igizo la lockdown: CHADEMA inacheza kamari

EZZ CHEZZ

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2011
Posts
1,230
Reaction score
1,356
Takriban wiki mbili zilizopia mwenyekiti wa Chadema Mbowe aliamuru wabunge wa chama chake kuanza lockdown mara moja pale Dodoma na kwamba wasiende majimboni kabla siku 14 hazijaisha ili wasije kupeleka maambukizi majimboni kwao!

Kulikuwa na namna mbili za kuitafsiri hatua hii. Mosi, upinzani kuna kiongozi shupavu asiyetetereka kimaamuzi. Pili, kwamba hiyo ilikuwa kiki tu ya kutafuta airtime na umaarufu hasa kwa mwenyekiti.

Binafsi naiamini zaidi hoja ya pili (kiki) kwani ndani ya wiki moja tu baadhi ya wabunge hao walionekana wakizurura Dar na siyo karantini Dodoma! Mbunge wangu Sugu alipost mpaka picha akijinasibu kuwa yuko Dar anapiga supu ya pweza!

Leo tunaambiwa wamemaliza lockdown na wako tayari kurejea bungeni. Swali, kuna lockdown isiyoambatana na vipimo? Na je, kujiweka karantini na kisha kurudi kujichanganya na waliokuwa kwenye eneo lenye taarifa za maambukizi kama alivyosema katibu wao Mnyika leo, ni kujali afya zao?

Tatizo la kiki ni kuwa isipokuinua itakushusha. Kiki hii tayari imewagharimu chadema majimbo (wabunge) kadhaa. Pia waliotii amri ya mwenyekiti ni 15 tu! Hivyo takribani idadi kama hiyo au zaidi ilikaidi agizo hilo. Hii bila shaka inadhoofisha chadema kuliko kuiimarisha.

Kwa mtazamo wangu, kuelekea uchaguzi mkuu chadema inacheza kamari nyingi na haina muda wa kutafakari karata ipi itupwe na ipi ibaki mkononi. Mambo yatakayotokea mpaka Oktoba ni mengi hivyo Chadema wawe na utashi wa kuangalia lipi la kudandia na lipi la kuacha lipite.

Mathalani. Hivi karibuni vyama vyetu vikubwa zaidi ccm na chadema vyote vimepata kada walau mmoja aliyekamatwa kwa tuhuma za jinai/uhujumu uchumi. Wakati ccm wao wamejitenga na mtuhumiwa wao (silaha & ujangili) kama katiba yao inavyowaagiza chadema wao viongozi wao wako bize mitandaoni (twitter) kujieleza kwa niaba ya mtuhumiwa (mdude), impliedly wakikihusisha chama na tuhuma hizo.

Nawashauri chadema kuachana na kamari hizi na badala yake kujikita na maandalizi ya uchaguzi. Mfano, ccm wao wameanza kujiandalia media platforms kwa kutwaa channel 10 na magic fm. Chadema wana nini? Vipi corona ikiendelea na kampeni zikafanywa kwenye media! Wataitegemea TBC kisha waje kulia nayo baadaye? Huu ni mfano tu wa masuala ya muhimu kuhangaika nayo badala ya kutafuta ligi za kitoto na spika.
 
Mbowe ni muhuni tu kama wahuni wengine. Binafsi nimeelewa Mbowe anatumia Cha Arusha ndiyo maana akili yake haipo sawa sawa.

Nawaambia kweli chadema Kama watapata hata viti vitano vya ubunge washukuru Mungu sana, wanamaamuzi ya kihayawani sana.

Wamekimbia kipindi muhimu na kwenye mijadala muhimu kwa taifa then wanajirudisha wakati mambo yamekwisha.

Mliowafukuza kwasababu hawakutii agizo la bwana wenu mbowe mmewaonea narudia tena mmewaonea kuthibitisha hili subiri adhabu yenu kutoka kwa wapiga kura wenu. Mnyika kibamba hatukutaki tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Achana nao na Haturu
Kwani Idd inakaribia? Naona mnakasi ya kutafuta hizi buku 7 pigeni kazi vijana haya ndiyo maisha mliyojichagulia wenyewe
Achana nao Haturudishi Posho nabungeni tunatinga tunachukua nyngne alafu tunasepa carantin Kula supu ya pweza
 
Keyword kwenye hotuba ya Mnyika :“Wabunge wetu wote waliotekeleza makubaliano na uamuzi wa Chama na Wabunge wa kujitenga kwa siku 14 ambayo yanatokana na maelekezo na ushauri wa Wataalamu wa afya ikiwemo WHO,” Yaani huo ni utetezi tosha mbele ya dunia.


Sent using Jamii Forums mobile app
NGOJA nimuquote mtu hapa #je, kujiweka karantini na kisha kurudi kujichanganya na waliokuwa kwenye eneo lenye taarifa za maambukizi kama alivyosema katibu wao Mnyika leo, ni kujali afya zao? Kule ndani wabunge waliobaki hakuna tishio tena?

kwa hiyo WHO ndivyo ilivyowaelekeza chadema kuwa kama kuna corona bungeni mkijilock down ruksa kurudi kama mazingira yako vile vile kabla ya ku ji lockdown? hii mibunge ya chadema ili yo ji lock down so stupid

kabla ku jilock down na sasa mnaporudi nini kimebadilika bungeni?
 
Keyword kwenye hotuba ya Mnyika :“Wabunge wetu wote waliotekeleza makubaliano na uamuzi wa Chama na Wabunge wa kujitenga kwa siku 14 ambayo yanatokana na maelekezo na ushauri wa Wataalamu wa afya ikiwemo WHO,” Yaani huo ni utetezi tosha mbele ya dunia.


Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna karantini isiyoambatana na vipimo. Ndiyo sababu MwanaFA kwa mfano ilimchukua mpaka siku 28 kutoka. Mpaka pale kipimo cha mwisho kilipoonesha negative. Mtoto wa Mbowe pia jana tumeambiwa imemchukua siku 57 kujiridhisha yuko sawa. Hivyo utetezi huo haujakamilika mbele ya watu makini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbowe ni muhuni tu kama wahuni wengine. Binafsi nimeelewa Mbowe anatumia Cha Arusha ndiyo maana akili yake haipo sawa sawa.

Nawaambia kweli chadema Kama watapata hata viti vitano vya ubunge washukuru Mungu sana, wanamaamuzi ya kihayawani sana.

Wamekimbia kipindi muhimu na kwenye mijadala muhimu kwa taifa then wanajirudisha wakati mambo yamekwisha.

Mliowafukuza kwasababu hawakutii agizo la bwana wenu mbowe mmewaonea narudia tena mmewaonea kuthibitisha hili subiri adhabu yenu kutoka kwa wapiga kura wenu. Mnyika kibamba hatukutaki tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi hudhani kuwa ni rahisi zaidi upinzani kushinda kwenye jimbo ambalo mbunge anayemaliza muda wake ni wa kwao. Bali kutengeneza ombwe na kuacha jimbo kuwa "huru" ni kuisaidia ccm. Sitashangaa ccm wakiwaconvert hao "expendables" wa chadema kuwa wagombea wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NGOJA nimuquote mtu hapa #je, kujiweka karantini na kisha kurudi kujichanganya na waliokuwa kwenye eneo lenye taarifa za maambukizi kama alivyosema katibu wao Mnyika leo, ni kujali afya zao? Kule ndani wabunge waliobaki hakuna tishio tena?

kwa hiyo WHO ndivyo ilivyowaelekeza chadema kuwa kama kuna corona bungeni mkijilock down ruksa kurudi kama mazingira yako vile vile kabla ya ku ji lockdown? hii mibunge ya chadema ili yo ji lock down so stupid

kabla ku jilock down na sasa mnaporudi nini kimebadilika bungeni?
Hiki chama hakina tena stragists na wandhimu calibre ya Prof. Baregu, Safari, Kitila, Slaa na wengineo. Waliobaki akina Lwakatare ndiyo hao wanatukanwa na watanzania wa mitandaoni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NGOJA nimuquote mtu hapa #je, kujiweka karantini na kisha kurudi kujichanganya na waliokuwa kwenye eneo lenye taarifa za maambukizi kama alivyosema katibu wao Mnyika leo, ni kujali afya zao? Kule ndani wabunge waliobaki hakuna tishio tena?

kwa hiyo WHO ndivyo ilivyowaelekeza chadema kuwa kama kuna corona bungeni mkijilock down ruksa kurudi kama mazingira yako vile vile kabla ya ku ji lockdown? hii mibunge ya chadema ili yo ji lock down so stupid

kabla ku jilock down na sasa mnaporudi nini kimebadilika bungeni?
Chadema mazezeta kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Takriban wiki mbili zilizopia mwenyekiti wa Chadema Mbowe aliamuru wabunge wa chama chake kuanza lockdown mara moja pale Dodoma na kwamba wasiende majimboni kabla siku 14 hazijaisha ili wasije kupeleka maambukizi majimboni kwao!

Kulikuwa na namna mbili za kuitafsiri hatua hii. Mosi, upinzani kuna kiongozi shupavu asiyetetereka kimaamuzi. Pili, kwamba hiyo ilikuwa kiki tu ya kutafuta airtime na umaarufu hasa kwa mwenyekiti.

Binafsi naiamini zaidi hoja ya pili (kiki) kwani ndani ya wiki moja tu baadhi ya wabunge hao walionekana wakizurura Dar na siyo karantini Dodoma! Mbunge wangu Sugu alipost mpaka picha akijinasibu kuwa yuko Dar anapiga supu ya pweza!

Leo tunaambiwa wamemaliza lockdown na wako tayari kurejea bungeni. Swali, kuna lockdown isiyoambatana na vipimo? Na je, kujiweka karantini na kisha kurudi kujichanganya na waliokuwa kwenye eneo lenye taarifa za maambukizi kama alivyosema katibu wao Mnyika leo, ni kujali afya zao?

Tatizo la kiki ni kuwa isipokuinua itakushusha. Kiki hii tayari imewagharimu chadema majimbo (wabunge) kadhaa. Pia waliotii amri ya mwenyekiti ni 15 tu! Hivyo takribani idadi kama hiyo au zaidi ilikaidi agizo hilo. Hii bila shaka inadhoofisha chadema kuliko kuiimarisha.

Kwa mtazamo wangu, kuelekea uchaguzi mkuu chadema inacheza kamari nyingi na haina muda wa kutafakari karata ipi itupwe na ipi ibaki mkononi. Mambo yatakayotokea mpaka Oktoba ni mengi hivyo Chadema wawe na utashi wa kuangalia lipi la kudandia na lipi la kuacha lipite.

Mathalani. Hivi karibuni vyama vyetu vikubwa zaidi ccm na chadema vyote vimepata kada walau mmoja aliyekamatwa kwa tuhuma za jinai/uhujumu uchumi. Wakati ccm wao wamejitenga na mtuhumiwa wao (silaha & ujangili) kama katiba yao inavyowaagiza chadema wao viongozi wao wako bize mitandaoni (twitter) kujieleza kwa niaba ya mtuhumiwa (mdude), impliedly wakikihusisha chama na tuhuma hizo.

Nawashauri chadema kuachana na kamari hizi na badala yake kujikita na maandalizi ya uchaguzi. Mfano, ccm wao wameanza kujiandalia media platforms kwa kutwaa channel 10 na magic fm. Chadema wana nini? Vipi corona ikiendelea na kampeni zikafanywa kwenye media! Wataitegemea TBC kisha waje kulia nayo baadaye? Huu ni mfano tu wa masuala ya muhimu kuhangaika nayo badala ya kutafuta ligi za kitoto na spika.
Lummumba mwapata tabu sana. Kuweweska kwingi. Hata mkipiga chafya neno ni CHADEMA.
1589548888199.png
 
Back
Top Bottom