Ifahamu nguvu ya kutokata tamaa kupitia Thomas Edison, mvumbuzi wa balbu za umeme

bigmukolo

JF-Expert Member
Mar 6, 2012
597
2,225
Mvumbuzi mkubwa kuliko wote katika historia ya ulimwengu. Ubora wa maisha ya binadamu wa sasa una deni kubwa na kazi ya Edison. Elimu yake ya darasani ilikuwa ndogo, lakini aliweza kujipatia haki miliki (patents) 1,093 za vumbuzi kubwa mbalimbali huko Marekani, zikiwemo zile za balbu ya umeme, kamera ya picha za sinema na kinasa sauti. Alipovumbua kinasa sauti mwaka 1877 wananchi walimwita mchawi.

Sifa yake kubwa iliyomletea mafanikio ni kwamba alikuwa king’ang’anizi. Uwezekano wa kushindwa hakuupa nafasi katika akili zake. Kila alipofikiria kuvumbua kitu aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kuwaeleza nia yake. Hakuogopa kuwa akishindwa watu watamcheka. Kila alipofanya jaribio likashindikana aliendelea kufanya jingine na jingine na jingine mpaka alipofanikiwa. Idadi ya majaribio aliyofanya kabla ya kufanikiwa kuvumbua balbu ya umeme ni zaidi ya elfu moja.

Tunajifunza nini? Uking’ang’ania mafanikio una nafasi kubwa ya kufanikiwa. Lakini ukibweteka na kungoja bahati una nafasi ndogo ya kufanikiwa. Hapa kwetu tunahimiza watu kulima vanilla, zao ambalo linaota vizuri na ambalo bei yake katika soko la dunia ni dola za Marekani 500 na zaidi kwa kilo. Ni dhahiri kuwa zao hili ni jawabu la umaskini katika jamii maskini.

Mkulima mmoja kutoka kata jirani ameweza kujipatia Tshs 150 milioni kutoka kwenye shamba lake dogo katika msimu mmoja. Watu wanaomzunguka ni maskini, lakini hawavutiwi kulima vanilla kama yeye. Sababu ni changamoto ya wezi.

Hawajui kuwa changamoto ikikukatisha tamaa itaua maendeleo yako. Aidha hawajui kuwa hakuna changamoto isiyo na jawabu.

Wakulima wa vanilla wenye mafanikio ni wale wanaong’ang’ana. Ni wale wanaochemsha bongo kutafuta jawabu la changamoto wanazokabiliananazo. Kama Thomas Edison asingechemsha ubongo na kung’ang’ana, maisha mazuri tuliyonayo yangechelewa sana. Labda hadi leo tungekuwa tunatumia kibatari wakati wa usiku.

Sumu ya maendeleo yoyote ni kukata tamaa.
 
Post-Valentine Psychosis hii. Umetoka kwa Thomas Edson, ukaelezea hisa zake 1000+ alizokuwa nazo. Ukatoka hapo ukaenda kwenye ubishi wake.

Ukaja kwenye uvumbuzi wake wa bulb. Kumbe lengo lako uje utupeleke kwenye kilimo tena cha vanila.

Sasa mkuu kilimo cha vanilla umesema kinalipa, kuliko kuzunguka kwa akina Thomas Edson kwa nini usingetuelezea tuu kilimo chake kinaendeshwa vp? Mahitaji na changamoto zake, bila kusahau faida ya zao hili!

Unforgetable
 
Post-Valentine Psychosis hii. Umetoka kwa Thomas Edson, ukaelezea hisa zake 1000+ alizokuwa nazo. Ukatoka hapo ukaenda kwenye ubishi wake.

Ukaja kwenye uvumbuzi wake wa bulb. Kumbe lengo lako uje utupeleke kwenye kilimo tena cha vanila.

Sasa mkuu kilimo cha vanilla umesema kinalipa, kuliko kuzunguka kwa akina Thomas Edson kwa nini usingetuelezea tuu kilimo chake kinaendeshwa vp? Mahitaji na changamoto zake, bila kusahau faida ya zao hili!

Unforgetable
Kabisaaaaa ni tangazo la vanilla

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Thomas bila Nicolá Tesla si kitu..
Ashukuru Tesla was humble and never mind person..
Tesla alikua kaajiliwa kwenye kampuni ya Thomas Edison. Hawakuishia tu kutumia ideas zake lakini pia wakati anafariki walichukua Kazi zake nyingi.
 
Ajabu sana! Bado kuna hizi hadithi za vanilla, kumtajirisha mkulima (kumfanya milionea)? Huko mkoani Kagera 'back in early 2000s' watu waling'oa mibuni na kupanda vanilla, hapo kilo ya vanilla kavu, ilinunuliwa kwa tsh. Laki moja na zaidi, na mbichi ilinunuliwa kilo kwa tsh.elfu sitini. Baada ya wakulima kuwa wengi bei ikaporomoka, na bei ya kahawa ikapanda. Ikawa majuto mjukuu, kipya kinyemi. Asante kuwatangazia vijana fursa ("kupigwa" ruksa).
 
Thomas bila Nicolá Tesla si kitu..
Ashukuru Tesla was humble and never mind person..
Tesla alikua kaajiliwa kwenye kampuni ya Thomas Edison. Hawakuishia tu kutumia ideas zake lakini pia wakati anafariki walichukua Kazi zake nyingi.
Mimi hua nawashangaa sana mnaosema sifa za Edson zote ni za Tesla! Kwamba yeye hakuna alichovumbua au? mara Tesla alikua disminder sijui nini.
Hamuoni kua Tesla kuajiriwa na Edson alikua ameshazidiwa vingi mno namna kutumia akili vizuri?
Alikua Genius ndio hatukatai lakini business wise alikua chini ya Edson!
 
Ajabu sana! Bado kuna hizi hadithi za vanilla, kumtajirisha mkulima (kumfanya milionea)? Huko mkoani Kagera 'back in early 2000s' watu waling'oa mibuni na kupanda vanilla, hapo kilo ya vanilla kavu, ilinunuliwa kwa tsh. Laki moja na zaidi, na mbichi ilinunuliwa kilo kwa tsh.elfu sitini. Baada ya wakulima kuwa wengi bei ikaporomoka, na bei ya kahawa ikapanda. Ikawa majuto mjukuu, kipya kinyemi. Asante kuwatangazia vijana fursa ("kupigwa" ruksa).
Nimefikiri kama wewe, kiukweli sijui chochote kuhusu kilimo cha Vanilla.

Lakini naona imeanza kupigiwa promo sana. Mimi kitu kikiwa na promo nyingi huwa naanza kupata mashaka nacho, huwa naona kama upigaji tu unatengenezwa.

Cheki kama huyu kutoka Thomas Edison hadi kilimo cha Vannila.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom