Ichunguzwe Mikakati ya Kuvuruga Taifa,Uchumi

mwanamichakato

JF-Expert Member
Mar 20, 2015
889
707
Tuna kila sababu ya kuchukua tahadhari dhidi ya maadui wa kijamii,kiuchumi na kiutamaduni wanaolinyemelea taifa letu.Utajiri uliokithiri kila pembe ya nchi yetu vimewafanya majirani wenye husuda kupanga mbinu nyingi za kudhoofisha mipango ya maendeleo hivyo kulifanya taifa letu kuwa ombaomba na maskini sana duniani.

Pamoja na unyonyaji unaofanywa na mabepari wa kutoka mataifa ya mbali,Tunazungukwa na marafiki wa mashaka ambao wamekuwa wakiwinda nyendo zetu waziwazi na kwa kificho kupitia mapandikizi ya mamluki katika sekta nyeti hivyo kutimiliza matakwa yao kwa urahisi..Fitina zao,Husuda zao,Faraka zao,Chuki zao,...Havifichiki vikichunguzwa na kubainishwa.

Kama nchi hatupaswi kubweteka kabisa na kujisahau,Wazalendo thabiti Idara nyeti zinazohusiana na masuala ya ulinzi na usalama wa taifa letu wapaswa kufungua jicho la 3,4,5,6,7 ili kubaini janja,mbinu na mikakati ya kudhoofisha uhai wa taifa kiuchumi {Biashara,Viwanda,Kilimo,Elimu,Mazingira ya uwekezaji,Sera na Sheria}.

Yapo madhara mengi yatakayolikumba taifa kwa mdororo endelevu ambao utalifanya taifa kuendelea kuburuta mkia katika vigezo vya kujikwamua toka ktk lindi la ufukara,maradhi,umaskini,Upumbavu,bonde la kipato kati ya walio nacho na wasio nacho....
 
Adui mkubwa wa TANZANIA ni uoga wa wanancha na viongozi wakuu wa Serikali kujifanya wajuaji wa kila kitu ilhali uhalisia unapingana na mienendo yao..
 
Tuna kila sababu ya kuchukua tahadhari dhidi ya maadui wa kijamii,kiuchumi na kiutamaduni wanaolinyemelea taifa letu.Utajiri uliokithiri kila pembe ya nchi yetu vimewafanya majirani wenye husuda kupanga mbinu nyingi za kudhoofisha mipango ya maendeleo hivyo kulifanya taifa letu kuwa ombaomba na maskini sana duniani.

Pamoja na unyonyaji unaofanywa na mabepari wa kutoka mataifa ya mbali,Tunazungukwa na marafiki wa mashaka ambao wamekuwa wakiwinda nyendo zetu waziwazi na kwa kificho kupitia mapandikizi ya mamluki katika sekta nyeti hivyo kutimiliza matakwa yao kwa urahisi..Fitina zao,Husuda zao,Faraka zao,Chuki zao,...Havifichiki vikichunguzwa na kubainishwa.

Kama nchi hatupaswi kubweteka kabisa na kujisahau,Wazalendo thabiti Idara nyeti zinazohusiana na masuala ya ulinzi na usalama wa taifa letu wapaswa kufungua jicho la 3,4,5,6,7 ili kubaini janja,mbinu na mikakati ya kudhoofisha uhai wa taifa kiuchumi {Biashara,Viwanda,Kilimo,Elimu,Mazingira ya uwekezaji,Sera na Sheria}.

Yapo madhara mengi yatakayolikumba taifa kwa mdororo endelevu ambao utalifanya taifa kuendelea kuburuta mkia katika vigezo vya kujikwamua toka ktk lindi la ufukara,maradhi,umaskini,Upumbavu,bonde la kipato kati ya walio nacho na wasio nacho....
hizo ngonjera kamwimbie Mkapa ndo aliuza nchi
 
IMG_20170327_200411.jpg
 
Upuuzi wa viongozi wetu kufuatilia raia ambao hawana hata chembe ya kitu ndo unasababisha wajisahau hadi majukumu yao wanayopaswa kufanya.
 
Adui mkubwa wa ustawi wa kiuchumi,kisiasa na kijamii wa Nchi hii hivi sasa ni Malaika Mkuu Sizonje.
 
Adui mkubwa wa ustawi wa kiuchumi,kisiasa na kijamii wa Nchi hii hivi sasa ni Malaika Mkuu Sizonje.
 
Utajiri uliokithiri kila pembe ya nchi yetu vimewafanya majirani wenye husuda kupanga mbinu nyingi za kudhoofisha mipango ya maendeleo hivyo kulifanya taifa letu kuwa ombaomba na maskini sana duniani.
Kweli kabisa majirani zetu walaaniwe maana escro, epa, richmond, mikataba mibovu kwenye kila idara, na takataka zote za rushwa tunazozikumbatia wametusababishia wao.
 
Elimu yetu Kizungumkuti {Sera,Miradi},Siasa zetu zimeingiliwa,Chaguzi zetu zinaingiliwa,Uchumi wetu umeingiliwa {Unadororeshwa},Mifumo ya utumishi,Uwekezaji .....
 
Back
Top Bottom